Nahisi haya ni matende, lakini hospitali wamesema sio

Tatemahunda

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2013
Posts
232
Reaction score
91
Wakuu salaam!

Siku chache zilizopita nilikuja humu kuomba ushauri kuhusu mguu kuvimba, ulianza kuvimba tu bila maumivu na ulianzia chini kwenye vidole hadi kwenye goti, sijawahi kuumiza, nilishauriwa humu ndani Mara moja kuwahi hospital, nikafanya hivyo.

Cha kwanza dokta aliniandikia nikapimwe matende, nikalazimika kulala hospitali. Usiku wakaja wahusika na kuchukua damu, ila ilionekana sina vimelea vya matende. Nikarudi tena kwa Mara nyingine nikaandikiwa kupima figo, ini pamoja na X-ray kwenye maeneo yaliyovimba, ila pia ilionekana niko salama.

Hofu inakuja kwamba isije ikawa ni matende, maana unafanana kabisa na muathirika wa matende, naogopa isije ikaja kugundulika muda ambapo ishakua sugu tayari, kuna wakati nawaza labda ningejua dawa za matende ningenunua nijinywee tu sasa.

Naombeni ushauri wenu tena kwa mara nyingine., natanguliza shukurani
 
Pole sana ulikwenda hospital gani maana hizi hospital zetu za mtaani si zakuziamini sana..
 
Pole sana ulikwenda hospital gani maana hizi hospital zetu za mtaani si zakuziamini sana..
Ni hospital ya wilaya mkuu, ilikua ikimilikiwa na kanisa ila kwa sasa sina hakika kama inaendelea kumilikiwa na kanisa, ila ni ya wilaya...
 
Last edited:
Mkuu nakushauri nenda hospital kubwa zaidi ya hiyo ya wilaya!
Signature yako inaniambia uko mkoa wa Tanga??
 
Hiyo miguu huvimba kwa kiwango kile kile asubuhi na usiku unipolala? Kuvimba kunabonyezeka kama godoro na kuacha kishimo kwa muda? Unapata dalili zingine zozote mwilini mbali na Kuvimba miguu? Wewe me au ke? Nenda hosp kubwa
 
Hiyo miguu huvimba kwa kiwango kile kile asubuhi na usiku unipolala? Kuvimba kunabonyezeka kama godoro na kuacha kishimo kwa muda? Unapata dalili zingine zozote mwilini mbali na Kuvimba miguu? Wewe me au ke? Nenda hosp kubwa
kuvimba hakuna tofauti ya usiku na mchana, yani hakuongezeki, ukibonyeza panaacha kishimo kwa muda, Mimi ni me! hospital ambayo walinipima ni ya mkoa wa tanga (bombo), walinipima figo na ini., wakaniambia nirudi tena, ndo najiandaa kurudi tena next week,tofauti na uvimbe huu kwenye mguu sina tatizo lingine kabisaa.
 
Wahi pale Mombo - Kwalukonge kuna hospitali ya wakatoliki inaitwa Rosemini!
Watakufanyia vipimo kwa undani na kukupa ushauri ufanye nini Kama wao watashindwa!!
Ahsante mkuu, nitafika napo.
 
Isije ikawa cancer ya mguu God forbid, ,Mungu akusaidie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…