tindikalikali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 4,854
- 1,129
- Thread starter
-
- #21
nilikuwa sina raha siku nzima, ila umenifanya nicheke, kamba ishakatika hiyo.Umependa pasipopendeka kaka,imekula kwako na itaendelea kula kwako kama utaendelea kumwazia huyo binti ambaye anaonyesha kabisa hana mapenzi. Yanini kujipa maradhi ya moyo mkuu? uamuzi uliochukua ndio sahihi kuliko kitu kingine. umefanya vizuri kuimwagia tindikali hiyo kamba ya mapenzi inayokutesa.
mi najua akili mwake, kashajiwekea dhana kwamba nampenda sana na lazima nitamtafuta tu. Kiukwel upendo unazid kupungua kama siyo kwisha kabisa.Tafuta kiburudisho upotezee mawazo huku ukiendelea kumfuatilia, then akiingia line 'kamua' halafu mpotezee mazima. Ukimfuatilia sana atakuja kujua kuwa unampenda kweli na kama hana mtu atakukubalia, ila na wewe mfanyizie umafya atakapokukubalia. Kwa kuwa amekusumbua muda mrefu, basi akiiingia 'king' kula mzigo halafu mpotezee mazima ili na yeye atie akili kama alivyokusumbua.
ni chungu kumeza lakin sina altenative nyingine.iyo ilishawahi kunitokea sema nikaamua kumpotezea but after a period alijirudi ila na mm nikamwekea ukauzu, yan mpaka kesho ajaamini kama ni mm... samtyms to give up is strong enough to let samthin go..! ka ukijua sio ww unakosa bahati but ni yeye mwenyew ndo kakosa bahati ya kuwa na ww .. be real
ni kweli dada angu, nadhan hili halihitaji hata kusoma "pure adv maths" kuelewa. Ila ni ubish 2 unaoponza akili na mwili.Kaka hapo haupendwi. Yaani ukiona unajitahidi kuwasiliana na mwenzio halafu yeye haoneshi ushirikiano ujue umepotea njia.
Mkuu kuna mara niliwahi kupenda binti lakini yeye alikuwa mguu moja ndani moja nje,sili silali bila kumuona au kuongea nae,nikafanya uamuzi mgumu nikakata mawasiliano,iliuma saana.Masaa,siku,miezi mpaka sasa ni miaka saba.Yeye alidhani utani na alikuwa kisha waeleza shoga zake bila yeye sipumui, alipoona wiki zinazidi akaanza kutuma watu,mara apite home na kuacha barua,mara aende viwanja vyangu(nami nilibadili),simu nilibadili laini kwa kifupi aliteseka sana zaidi ya alivyonitesa.Umeongea mambo ya msingi, hapa nazidi kugundua kwamba mambo mengine ni kujiendekeza, mwanzo nilimfanya oxygen>kumbe nilikuwa najidanganya, hata siamin kama nimemaliza wik 3 pasipo kuwasiliana naye.
Habari zenu wadau! Nimefanya maamuzi magumu ambayo nilidhani yatanisaidia, lakini yanaishia kuniumiza. Ni kuhusu binti ambaye nimemfatilia kwa muda mrefu, nilijitahidi kwa kila hali kumuonesha kwa vitendo kwamba nampenda. Nilijitahidi kuwa karibu naye hasa kwa upande wa mawasiliano ya simu, muitikio wake ulikuwa mzuri japo alisema mapenzi na mimi no. Niliukubali urafiki japo kwa shingo upande, niliendelea kuwasiliana naye, lakin ilikuwa mpaka mimi nimtafute, nikikaa kimya naye anapotea, nikirudi anarudi. Kama mnavyojua kuwa kamba ikivutwa sana hukatika pabovu, ilifika muda nikachoka na nikaamua kukaa kimya. Sasa ni wiki ya 3 toka nimchunie, naye yuko kimya. Wadau hali hii inanitatiza, nataka nimpotezee mazima lakini naona naelekea kushindwa, moyo unaniuma kumuacha aende. Naomba ushauri wenu.
nimekusoma mkuu, hakika mnanipa nguvu ya kusimamia kile nilichokiamuaKaka tafuta life hawa viumbe ni bahati tu kuwapata. Hata ufanye juhudi gani kama hajakudondokea utapoteza muda na kamwe hatokwambia hana feelings na wewe. Just be a man akupendaye atakuja tu. Usipende kupoteza muda wako kumfikiria kuna siku atakuletea kadi ya harusi na utapoteza mwelekeo wa life kabisaa. Akupendaye hata sekunde moja hakiachi upumue bila kubip japo hata kwa kukosea.
nilishamwambia na yeye alikiri kwamba anajua kwamba nampenda, anadai hajapanga kuwa kuwa na mpenz kwa sasa, labda amalize chuo na kupata kazi, ndiyo anaingia mwaka wa kwanza sasa.je umewahi kumtamkia dhahiri lengo lako la kumpenda au ni hizo dalili tu? Ebu mtamkie kidhati jibu lake ndilo litakudhirihishia kama anakupenda au la.
Bora angekuwa na mtu, anadai hajawai kuwa na wala hana mtu. Kingine sipo iddle kama unavyofikiri, bado nafikir haya mambo hayakwepeki.hayo ndiyo madhara ya kuwa na iddle mind. Keep your brain bussy hata kwa kusoma vitabu. Kwani mwanamke ni yeye tu. Inawezekana na mtu wake anayempenda kwa dhati unataka amsaliti, na ingekuwa wewe ndiyo unasalitiwa??
<br />Huyo anakupenda ila ana tabia ya woga na ukimya anaona akikutafuta utamwona ni mhuni, .
<br />ni kweli dada angu, nadhan hili halihitaji hata kusoma "pure adv maths" kuelewa. Ila ni ubish 2 unaoponza akili na mwili.