EmmilyPM
Member
- Nov 14, 2018
- 56
- 65
Habari za majukumu wakuu, mimi ni kijana wa miaka 29. Nina shida moja ambayo nahisi imekuwa kama "addiction."
Nimejipata nikiwa na tabia ya kufuatilia (track) simu za kila mpenzi ninayeingia naye kwenye mahusiano, iwe nina mipango ya baadaye naye au hata kama ni uhusiano wa muda mfupi. Ilimradi tu tunakuwa na uhusiano wa kimapenzi, lazima nifuatilie mawasiliano yake. Pia, sijawahi kuwa na mahusiano mafupi; karibu mahusiano yangu yote nimekuwa nikifanya hivi.
Hua nahisi kama nafurahia kufuatilia mawasiliano ya mpenzi wangu, ingawa tangu nianze kufanya hivi ni mara moja tu, mwaka 2020, nilipokutana na ujumbe uliothibitisha kuwa mpenzi wangu alikuwa amenisaliti. Wapenzi wengine wote, pamoja na huyu niliye naye sasa, sijawahi kuona dalili yoyote ya usaliti.
Natamani niache hii tabia, lakini nahisi nashindwa. Najikuta natoa "tracker," lakini baada ya muda mfupi nairudisha tena. Nahitaji ushauri wenu juu ya hili. Nitashukuru sana.
Nimejipata nikiwa na tabia ya kufuatilia (track) simu za kila mpenzi ninayeingia naye kwenye mahusiano, iwe nina mipango ya baadaye naye au hata kama ni uhusiano wa muda mfupi. Ilimradi tu tunakuwa na uhusiano wa kimapenzi, lazima nifuatilie mawasiliano yake. Pia, sijawahi kuwa na mahusiano mafupi; karibu mahusiano yangu yote nimekuwa nikifanya hivi.
Hua nahisi kama nafurahia kufuatilia mawasiliano ya mpenzi wangu, ingawa tangu nianze kufanya hivi ni mara moja tu, mwaka 2020, nilipokutana na ujumbe uliothibitisha kuwa mpenzi wangu alikuwa amenisaliti. Wapenzi wengine wote, pamoja na huyu niliye naye sasa, sijawahi kuona dalili yoyote ya usaliti.
Natamani niache hii tabia, lakini nahisi nashindwa. Najikuta natoa "tracker," lakini baada ya muda mfupi nairudisha tena. Nahitaji ushauri wenu juu ya hili. Nitashukuru sana.