Nahisi nimemeza vipande vya chupa

Milale

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2013
Posts
494
Reaction score
189
Habari zenu ndugu zangu,naombeni msaada wenu kwa hili.

Jana nilienda kununua soda nikanyw ila baada ya kumaliza nikagundua kuw chupa ilipasuka mdomo na kuhisi kuwa nitakuwa nimemeza vipande vya chupa.naombeni kuuliza ni madhara gani nitakayoyapata iwapo nitakuwa nimemeza hivyo vipande.na itachukua muda gani kuanza kupata hayo madhara?

Naombeni sana mnisaidie kwa hili maana nimekosa amani kabisa, asanteni.
 
Hizo ni object tu, jitahidi uende haja kubwa mara kwa mara itakusaidia kuflush,, lakini kwa msaada zaidi pata ushauri wa madaktari. Pole sana!
 
Nadhani kama ulizimeza basi leo usingepata hata bahati ya kuhisi kuwa ulimeza chupa,
bali ndugu na jamaa zako ndiyo wangekuwa wanahisi hivyo wakati huo wewe ungekuwa Mochwari..
Ninaamini hukumeza, na chupa nyingi za soda zina hii hitilafu ya kuwa na midomo iliyomeguka.
 
Pole sanaaaa
 
Kama umeweza kuanzisha thread basi endelea kula raha... Vinginevyo ungekua mahututi..
Ila wanywaji wa soda mna ujinga mwingi mnywa gambe hawezi fanya hiyo mistake hata kama hajitambui....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuingia tumboni sio ishu (kunywa kwa soda/maji), ila wenye kuvitoa ndio mziki (kupata haja). Hapo damage unaweza ukaipata ya kutosha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…