Nahitaj mwanamke awe rafiki sana na ikiwezekana awe mke kabisa

Seek

Member
Joined
Oct 26, 2013
Posts
27
Reaction score
6
Awe rafiki sana:
-Niweze kumuamini na kumtegemea pale inapobidi
-Niweze kuzungumza naye hisia zangu bila kificho
-Tushirikiane katika hali mbalimbali inapofaa
-etc..

Ikiwezekana awe mke kabisa:
-Sio lazima awe mke wangu maana kuoa/kuolewa ni mchakato
-Ikishindikana kuwa mke nitalinda na kuheshimu mipaka ya uhusiano wetu
-Ikitokea nikamuoa itakuwa ni ridhaa yetu mimi na yeye. Hata hivyo atakuwa amenifaa kwa kiasi kikubwa maana sio mrahisi ktk maamuzi hayo.


Mimi:
-Nina udhaifu wa kuchelewa kugundua asiyenipenda (asiye nitakia mazuri/mema) maana siku zote natanguliza kumfikiria/kumchukulia mtu kwa uzuri.
-Pia nina udhaifu wa kujitolea kwa rafiki/watu mbalimbali
-Halafu nina udhaifu wa kusema ukweli au kutosema kabisa, lakini sio kudanganya
[Nimeamua kuita udhaifu maana wapo watu ambao kuna wakati maisha huwalazimu kuwa tofauti na hivyo]

-Kwa anaye jali umri;nina miaka zaidi ya 30 na ni pungufu ya 40 (just around 30 yrs)
-Kwa wale wa maumbile; kimo cha wastani (around 5'5"), umbo la kawaida pia (si mnene si mwembamba), rangi nyeusi kiasi.
-Male, never married, and without children
-Na kwa wanaozingatia elimu; nina shahada moja na nitasoma zaidi nitakapo pata wasaa.
-Yes! nafanya kazi, na ninaishi D'salaam

Yeye:
-Nafasi iko wazi kwa kila mwanamke mtu mzima mwenye akili timamu
-Anaweza hata kuwa nje ya nchi (Tanzania), lakini nitaweza kumvumilia kwa muda tu nione kama ni uhusiano wenye mashiko (Nachelea ya wahenga "fimbo ya mbali.......")
-Akiwa mke, ajitahidi kujua kuwaelewa ndugu jamaa na marafiki kama sio kuwapenda au kuwavumilia.... zaidi ni ikitokea wametembeleana
-etc

Karibuni!
...........................
 
Salaam!
Usisahau kutuletea mrejesho hapa hapa!
Salaam!
 
Kuwa na imani utampata umtakae na mwenyewe sifa unazoitaji....
Mtangulize Mungu Kwanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…