Nahitaji kuanza ujenzi naombeni ushauri

Twinawe

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2016
Posts
2,431
Reaction score
5,336
Panapo majaliwa mwaka huu nataka nianze ujenzi mkoani kwetu .

Namjengea mama yangu kama zawadi ya shukurani kwake kwa malezi mazuri .

Sina pesa nyingi ya kujenga kwa mkupuo ila ujenzi wangu nimegawa kwenye phase zifuatazo.
1.kununua materials kama mchanga,kokoto,mawe,tofali,cement

2.msingi
3.boma usawa wa dirisha
4.boma na kumaliza zege kabisa.
5. Kupaua
6.plasta
7.milango na madirisha
8.choo
9.rangi
10.tiles.

Nafanya hivi sababu kipato changu kidogo (tgs c)

Hii ndo design nayoiwaza kwa kuanzia ili mama asiendelee kupanga

Naombeni ushauri wa vipimo natamani sebule iwe kubwa na vyumba vikubwa.

Naombeni estimation ya cost kiwanja ni kikubwa m² 600. Kina nature ya slope japo sio sana .

Ahsanteni nawakaribisha.


 

Attachments

  • 20230510_093538.jpg
    41.4 KB · Views: 39
Tafuta ramani nzuri yenye muonekano mzuri wa kuvutia... Achana na raman za vijijini, sikuhiz kuna raman nyingi nzuri sana ila zipo simple hazina complications na gharama nafuu... Ingia Google
ANGALIZO kwasabab unamjengea mama jitahid iwe simple sana ikiwa na mambo mengi utashindwa jujenga kumaliza
 
Sawa mkuu nadhani hata hii design niliyoiwaza haina mambo mengi
 
Ahsante sana dada
 
Hongera sana,
Mungu azidi kukubariki.
 
Mkuu karibu nikuuzie ramani iliyo na kira kitu 4bedroom Kwa bei simple Sana ,haizid 100k na ina mhuri kabisa wa kukusaidia kuombea kibar Cha ujenzi
 
Chukua ramani aliyo kutumia mdau hapo chini.
Na kwakua unataka kujenga kijijini sikushauri uanze mambo ya kununua ramani kama mdau mmoja alivyo anza kukushawishi hapa.
Kwa mtazamo nimeona eneo unalo taka kujenga halina slope kubwa sana na hata aina ya udongo sio mbaya sana mkuu.
Mwisho nikukumbushe kwamba ulitakiwa uwajengee wazazi wako (sio mama yako), hata kama wazazi wako walizinguana usiingilie ugomvi wao tafadhali.
Nikutakie kila lakheri na Mungu akufanikishie mipango yako.
mkuu, nimesoma uzi wako nilikuwa nipo idle nikaona nikupe plan hii imekaaje?View attachment 2616450View attachment 2616450
 
Uko sahihi mkuu ila wazazi wangu wametengana nikiwa na 1 year baba ana maisha yake mazuri tu na mahusiano yangu na baba mazuri tu mi najenga tu hata yeye akija kuishi sio vibaya ila ni mtu na familia yake na ana maisha yake mamangu toka nazaliwa bado anapanga
 
Mungu akusimamie, akuongoze na ufanikiwe kwenye jambo lako...🙏
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…