Nahitaji kujifunza Martial Art

Nahitaji kujifunza Martial Art

bafetimbi

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2018
Posts
1,085
Reaction score
1,741
Wasalaam wazee.

Ni kwa muda mrefu sana nimekuwa nikipenda kujifunza sanaa za mapigano.

Sasa wadau naamini humu kuna wakongwe na wajuzi wa mambo haya mnaweza kunipa ushauri.

Je, ni sanaa ipi ya mapigano iko strong kwa maana ya self defence, sihitaji kuwa mkorofi ila mtu akijichanganya vibaya hilo pigo atakalopewa akasimulie ukoo wao wote.

Nipo Mbeya. Kwa wanaojua mkoa wa mbeya mafunzo hayo nitayapata wapi naomba anijuze.

Kuna ishu iliniitokea juzi siku ya iddi mosi, nikaenda pub moja hivi matata sana kwajili ya kupata ulabu na mbuzu choma kidogo

Sasa nikiwa mule ndani kuna jamaa mmoja tukazinguana vikali tu nikasimama kwajili ya mpambano maana naye alionesha wazi anataka tupigane, nikajipanga mkao wa vita sasa. Eebwanaeeee nilikula pigo moja hivi la ajabu kisha akanimalizia na teke moja hivi nikaona sasa huyu simuwezi maana anaonekana anamafunzo ya kupigana wakati mimi sina. Nikataka kumtwisha chupa la kvant wadau wakaja kuzuia pale.

Na mimi nataka kujua kupigana maana sasa tunakoelekea sio kuzuri.
 
Bado mnawaza kupigana? Mwili wa binadamu ni complicated sana. Unaweza anguka toka ghorofa ya pili na usife ila ukapigwa kibao nyuma ya sikio ikawa ndiyo nitolee.

Baba aliniambia "Kuna namna mbili za kupigana, aina ya kwanza ni mnazipanga one two, bob and weave basically unataka kuwavutia wanawake aina ya pili ni kupigana kwa kung'ata, kufinya, mawe, chupa na kila silaha. Atakayetumia aina ya pili ni lazima atashinda na hata hivyo hakuna mwanamke anayevutiwa na mwanaume anayejua kupigana so stick na aina ya pili"
 
Bado mnawaza kupigana? Mwili wa binadamu ni complicated sana. Unaweza anguka toka ghorofa ya pili na usife ila ukapigwa kibao nyuma ya sikio ikawa ndiyo nitolee.

Baba aliniambia "Kuna namna mbili za kupigana, aina ya kwanza ni mnazipanga one two, bob and weave basically unataka kuwavutia wanawake aina ya pili ni kupigana kwa kung'ata, kufinya, mawe, chupa na kila silaha. Atakayetumia aina ya pili ni lazima atashinda na hata hivyo hakuna mwanamke anayevutiwa na mwanaume anayejua kupigana so stick na aina ya pili"
Kuna situation itakutokea utaona umuhimu wa kujua mapigano kama mimi ilivyonutokea
 
Kwa wanaohitaji kujifunza Martial arts,
Self - defence
Wanaweza kunicheki

Tuma neno "Martial arts"
0693322300

Uwe Dar es salaam.

Dojo lipo Upanga karibu na ubalozi wa uswizi,
Jingine Mikocheni Pale Azura.

Tsh 15,000 Kwa kipindi,
Kwa mwezi 140,000/=
mimi nipo mbeya man,
 
hivi karate mpaka ukifika level gani ndiyo unakuwa fit haswa haswa.
Karate Haina mwisho, wewe jifunze kiwango unachohitaji nenda kazini. Kuhusu kuwa fit itategemea unakutana na nani boss unaweza kupata mafunzo mwaka ukajiamini ila ukakutana na jamaa kabla hujaapply ulichojifunza muda wote huo ukawa chini tayari Tena taabani.
 
Karate Haina mwisho, wewe jifunze kiwango unachohitaji nenda kazini. Kuhusu kuwa fit itategemea unakutana na nani boss unaweza kupata mafunzo mwaka ukajiamini ila ukakutana na jamaa kabla hujaapply ulichojifunza muda wote huo ukawa chini tayari Tena taabani.
vipi sasa kama umejifunza ukawiva alafu hakuna mtu anaekuchikoza si utashindwa pakwenda kuapply ujuzi au inakuaje hapo
 
Back
Top Bottom