Nahitaji kuongezeka mwili kidogo

BRO SANTANA

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2015
Posts
1,845
Reaction score
2,248
Heshima kwenu wakuu.

Mimi ni kijana mwanaume ambaye nina miaka 2 toka nianze kazi.

Lakini nilioanza nao kazi wametoka mashavu balaa ila mimi ndo kwanza nazidi kupungua wakati nakula vizuri ila pombe situmii.

Ushauri wenu tafadhali na kama kuna njia mbadala ya mimi kuweza kujazia.
 
Kawaone John Mnyika na Salumu Mwalimu. Watakusaidia shida yako kwani na wao walikuwa na shida kama hiyo.

Mandla.
 
Kijana Tiba au suluhisho lako limeshakufikia wewe niPM upate virutubisho vitakavyokufanya ufurahie maumbile yako.
 
Msaada na mm wakuu nataka niongezeke kama jamaa
 
Wengine tunatamani kupunguza uzito kwa angalau 25% wewe unatamani uongezeke, kila la kheri mkuu ila ni vyema ukajaribu kuangalia BMI yako kwanza, kama ipo normal basi usiongeze uzito zaidi kwani unakuwa umejiweka kwenye risk kubwa ya kupata magonjwa ya moyo na kisukari.


Mimi naomba mwenye mbinu za kupunguza uzito mbali na madawa ya viwandani anisaidie. Nitashukuru.
 
Tafuta majani ya mlonge, kama utapata yaliyokaushwa na kusagwa itakuwa nzuri, changanya kujiko kimoja cha chai kwenye juice or maziwa or uji na unywe kwa siku Mara mbili, asubuhi na usiku unavyolala.
 
Watu wanahangaika kupungua we we unataka kuongezeka....
Kabla ya kutafuta kuongezeka Pima urefu wako na uzito then calculate body mass index BMI kama IPO chini tafuta unene ila kama average tulia na mwili wako....

Kwa ushauri wa kunenepa tumia kitimoto na bia (kuna bia zisizo na kilevi)....
 
Piga ugali kitimoto kutwa mara tatu

Halafu uwe unashushia na bia baridi. Hapo mwezi tu utakua kama sumo

Uwe hukosi kamfuko ka chips kila uendako
 
kama unataka shavu kunywa gongo mixer msosi was manati
 
yaani unene naupinga kwa nguvu zote plus kitambi, doh!!!!! ni hatari sana, am proud of my slim body
 
Punguza uzito na kubaki kwenye figure ya kuvutia kwa kutumia G2 CONTROL Asili.
Kwa Maelezo Zaidi Tuwasiliane 0719 252523
 

Attachments

  • G2 CONTROL MEAL REPL.jpg
    21.5 KB · Views: 249
  • TESTIMONY MEAL REPL.jpg
    57.4 KB · Views: 251
Mkuu hebu kama unaweza naomba unifafanulie kuhusiana na hiyo picha jinsi jamaa alivyokuwa awali na baada ya kupungua.

Je ina uhalisia wowote au mfano tu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…