Nashukuru sana mkuu kwa msaada,ila risiti niliyonayo inasema mali ikushauzwa hairudishwi akimaanisha samani anazouza huyu jamaa
Kama nimekuelewa vizuri ni kwamba, makubaliano yalikua utoe Advance (malipo ya awali) kisha atengeneze hiyo furniture yako na hapo ulitakiwa umalizie pesa iliyobaki.
Kilichofuata ikawa huyo jamaa afanye wajibu wake wa kutengeneza hiyo bidhaa ili umalizie malipo na wewe uchukue mzigo wako, hapo ndipo dana dana zilipoanza, huyo fundi pesa anaitaka lakini hajamaliza kutengeneza bidhaa, hizo chenga zikaendelea hadi ulipohamia mbali na umekata tamaa unaona bora pesa yako irudi (Hapo ni kama nimekuelewa maelezo yako)
Mimi sio mwanasheria ila kimsingi mambo mawili yanatakiwa yatokee hapo, akukabidhi mzigo wako umpe pesa yake iliyobaki au akurudishie ile pesa uliyompa awali. Hiyo risit kuandikwa mali ikiuzwa haina nguvu kwako kwa sababu hajauza mali bado, hakuna kitu alichokupatia wewe.
Nafikiri inabidi ifike mahali tuanze kuwekeana mikataba kwenye mambo yetu mbalimbali, hapo kinackosekana kipengele cha alitakiwa atimize wajibu wake ndani ya muda gani na kama angeshindwa nini kifanyike na kama angetengeneza furniture kisha ukashindwa kulipa nini kifanyike.
Haya matatizo yanatukumba wengi sana na tumeshaumia sana. Ila pakiwa na maandishi mtu hakuoni mbaya, kanuni zinatawala.
Hapo akina
Dragoon wachangamkie fursa ya kuelimisha jamii kujua umuhimu wa kuandikishana kwenye mikataba hata kwenye mambo tunayofikiri ni madogo, itaweka nidhamu na kupunguza usumbufu usio wa lazima.