Je akiba katika mifuko hifadhi ya jamii inakubalika kama corateral au ikoje? Tufafanulie kiongoziNenda ECO bank kuna masharti nafuu ila kwa hiyo M1 na mkataba wako wa 1year huo ndo shida wanaweza wakakupa 5mil also depends hifadhi ya jamii Una bei gani.
thanksNenda ECO Mkuu utapata utaratibu mzima but hela ya hifadhi ya jamii inahusika wewe kupata mkopo.
sijawacheki TIB. niliwasomasoma wanaanzia 30m na nasikia kuna urasimu sana na hadi business plan yako ipite na upate mkopo unakuta mwaka umekatika. nataka nianze kidogo na niiikisha kuwa fresh ndo ntaanza na watu kama TIB for big money.umejaribu kuwaona TIB?
Malila mnapataga wapi mitaji ya kilimo?
ahsante sana kwa ushauri mkuu. nitaufanyia kaziMimi ningekushauri hivi:
Mosi, kama kilimo unchokiongelea kinaanza msimu wa mwakani usiwaze mkopo. Jipangie malengo ya unatarajia kulima kiasi gani na bajeti kwa makisio itakuwa kiasi gani kisha anza kufanya saving kwa ajili ya kilimo. Kama kweli unaweza lipa laki sita mkopo kwa mwezi, makadirio ya hadi kufikia mwezi wa kumi na mbili ni zaidi ya Tshs 4m. Hii pesa inatosha kwa kuanza kilimo na gharama zitakazoongezeka utazicover na mshahara wako wa mwezi. Kumbuka njia hii inafaa zaidi kwa kilimo kidogo na cha kati (chini ya ekari 30).
Pili, kama unalenga kufanya kilimo kikubwa fanya yote niliyokuambia hapo juu uhakikishe angalau una pesa kiasi ya kuanzia kilimo. Kisha mtafute rafiki, ndugu au jamaa ambaye mnaweza unganisha nguvu na kulima angalau ekari 50 na kuendelea na mlimie pamoja. Mambo muhimu ya kuzingatia kwenye hii njia ni kumpata mtu mwenye commitment ya kweli na malengo yayofanana au kuelekeana. Hii ni nzuri sana mkiifanya kisasa na ikiwa na matokeo chanya utafurahia kilimo lakini pia ikitokea ukapata matokeo hasi shambani basi hautaumia peke yako.
Mwisho, kilimo ni zaidi ya kupata mkopo benki, Kuna mambo mengine muhimu ya kuzingatia na mojawapo ni usimamizi thabiti wa mradi wako wa kilimo. Hii ni changamoto kubwa sana kwa wakulima walioajiriwa, jipange sawia kwenye hili pia sambamba na kupata mtaji wako wa kilimo.
kweli wakulima wanatabu sana. mi mwenyewe najitahidi kusave na nimejiunga kwenye saccos fulani hivi. vipi, siku hizi unakopesheka?Mimi nilianzia zero kabisa, baada ya kugundua kuwa sikopesheki ilibidi nifanye homework yangu vizuri.
Ilibidi nibadili tabia yangu, ilibidi vyeti vyangu vya shule nifungie kabatini ( niliwahi kuotesha maua nyumbani kwa mtu hapo Bongo, mpaka leo binti wa yule mzee huniita gardener wao, huwa sijisikii vibaya kwa sababu nilikuwa choka mbaya).
Kwa kukudokeza tu, bia ya mwisho nilikunywa 1998 pale Matumbi Bar Tabata, Siku alipokuja Pat Shange Uwanja wa Taifa ndio ulikuwa mziki wangu wa mwisho kushiriki. Elimu yangu ya juu haikunisaidia kusaka mtaji ila ilichangia kidogo. Nilichofanya, ni kwamba ilibidi nirudie utalaam niliopata secondary, yaani shule ya kilimo, na E/K enzi ya primary school.
Nikajitolea sana( miaka kama mitatu hivi,natangaza jina tu,niliwahi kufundisha hadi tuition), na mimi nikashusha vitu ninavyovijua kichwani mpaka vikaonekana. Wakati nafanya yote hayo, vision yangu ilikuwa clear kabisa mbele yangu, yaani picha ya matarajio yangu ilikuwa kubwa na iko wazi.
Sasa, baada ya vitu vyangu kuonekana, nilianza kupata michango ya mawazo toka kwa Watz mbalimbali, wengine nikawa nafanya nao partnership,wengine tunafanya pamoja lakini kila mtu kivyake.
Naomba nikwambie, juu ya yote; niliboresha afya yangu sana,nikaongeza uaminifu kuanzia kwangu mwenyewe na kwa jamii inayonizunguka ambavyo vilipandisha pr yangu. Nikafanya kazi kwa juhudi na maarifa sana mfululizo wa miaka mitano. Walau nikaanza kupata mwanga.
Juu ya yote, Mungu amenisaidia sana.
mkuu umechanganua kitaalamu sana nimevutika sana japo naona profit kama ni too good to be true. lakini inaonyesha ni bonge la business. vipi kuhusu mbolea?. shamba lako liko wapi? kwa huko msimu wa kulima matikiti unaisha mwezi gani?.niko interested sana na ngoja nifanye research. pia naomba tutumiane namba za simu.Kwakuwa matikiti ya hybrid ni makubwa kwa umbo, tutaweza kuuza kwa bei ya jumla sh 2000/= kila tunda.
Hivyo kwa awamu ya kwanza tutapata gross profit: 26664*2000=53328000
NET PROFIT:
Cost of production: sh1170,000 + (usafiri chakula na n.k sh 100,000)=1,270,000
Netprofit 53328000-1270000=TZS52,058,000/=
Assume uncertainties incurred during WIP leading to extreme Loss of the expected yield approximately Tsh 20,000,000!
Bado tutarealize faida nzuri ambayo hakika haitatufanya tujutie au kukata tamaa kusonga mbele.
Na ikumbukwe kuwa Water melon huchukua maximum siku 75 tu kutoka kupandwa mpaka mavuno.
Kama unawoga wa kufanya project hiyo, nikopeshe mimi mtaji hapo juu dhamana yangu ni shamba langu na academic certificates zangu zote.
Kwakuwa matikiti ya hybrid ni makubwa kwa umbo, tutaweza kuuza kwa bei ya jumla sh 2000/= kila tunda.
Hivyo kwa awamu ya kwanza tutapata gross profit: 26664*2000=53328000
NET PROFIT:
Cost of production: sh1170,000 + (usafiri chakula na n.k sh 100,000)=1,270,000
Netprofit 53328000-1270000=TZS52,058,000/=
Assume uncertainties incurred during WIP leading to extreme Loss of the expected yield approximately Tsh 20,000,000!
Bado tutarealize faida nzuri ambayo hakika haitatufanya tujutie au kukata tamaa kusonga mbele.
Na ikumbukwe kuwa Water melon huchukua maximum siku 75 tu kutoka kupandwa mpaka mavuno.
Kama unawoga wa kufanya project hiyo, nikopeshe mimi mtaji hapo juu dhamana yangu ni shamba langu ambalo ni ekari 17 ambalo 70% limezungukwa na mto. Ikitokea nimevuna vizuri ntakupa 30% ya ROI na ntakuomba uwe unafanya thoroughly visits kuona maendeleo ya project.
Nikishindwa, awamu ya kwanza na ya pili kama utaniwezesha basi nitalazimika nikuachie shamba.