wakuu,
nawapongeza sana wote waliotoa michango yao katika thread hii na walioonesha juhudi katika harakati za kumsaidia ndugu yetu huyu mwenye wazo bora la kuanzisha biashara.
wakuu, nami najitokeza kwenu nikiwa na biashara ambayo tumeianza sisi vijana watatu ambao tumeamua kushikana mikono na kujikwamua na tatizo la ajira. Tatizo tu ni kwamba tumepungukiwa na mtaji mzito upatao Tshs milioni 2!
Gharama nyingine ya uanzishwaji wa biashara tumeshalipia, ikiwemo kodi ya eneo, na ununuzi wa eneo lenyewe. Kwa kifupi biashara ishaanza karibu wiki 2 sasa, ila tunapungukiwa na kiasi hicho kikubwa cha pesa ambacho kama kingepatikana, basi tungeweza kupata faida mara 3 zaidi na marejesho yangeweza kuwa bora zaidi.
Wakuu, nisiwe mtu wa kuficha ficha, biashara hii inahusiana na nyama katika machinjio ya vingunguti.
Tumeamua kuanza kama wanunuzi wa nyama tu wadogo, lakini lengo letu kuu hasa mpaka mwishoni mwa mwaka huu (ama hata ikiwezekana tukawezeshwa mtaji zaidi wa kubeba ng'mbe wetu wenyewe sasa) ni kuwa tunanunua ng'ombe kutoka mikoani kanda ya ziwa na kuja kuwachinja sisi kama sisi badala ya kununua kwa watu.
wakuu tunaombeni sana msaada wenu japo kwa hili.
Natanguliza shukurani.
mawasiliano: 0683011003