Nahitaji msaada wa kisheria juu ya hii kesi

Kwa sheria ipi hii hii ya civil law na contract law acha bhasi labda kama kudaiwa huko kumesababishwa na jinai
Daktari! (Utanisamehe kama wewe ni kati ya wapuuzi wa kujiita Dr wakati hujakisomea), ingawa mimi siyo Mwanasheria, lakini nina uzoefu na hili jambo. Kesi ya Madai ikihukumiwa na isipotekelezwa baada ya hukumu kwa muda fulani, hugeuka na kuwa ya jinai ambapo mdaiwa hukamatwa na kuswekwa lupango. Hata Diamond hiki kitu karibu kimtokee
 
Duh hapa sijui msaada gani wa kisheria unataka mkuu, Badilisha heading iwe 'MSAADA JINSI YA KUFANYA DENI LIPOTEE JUU KWA JUU" ila dawa ya deni ni kulipa tu
 
Umeona nilichoandika hapo juu nimesema labda kama kudaiwa huko kumesabaishwa na jinai na itambulike kwamba Pale unapoweka ahadi na usiitimize na ulikuwa unaweza kuitimiza hizo sio madai tena ni Umeignore kutimiza sheria na ndo hapo Madai huwa Jinai...

Lakini haiwi jinai bila kuchukua Sura ya jinai kamwe lazma iingie ujinai (Yaaani ivunje sheria za jinai ndo iitwe jinai vinginevyo kesi ya madai haiwezi kusabisha mtu akafungwa nakazia msimamo wangu)

NB: Jifunze kujadili kwa hoja bila personal Attack au Character assasination nafikir utakuwa bora Vingenevyo vutanifanya niamini alichosema Rais kwamba vijana wa siku mmekosa maadili
 
Kitu hujui myamaza tu
 
Kitu hujui myamaza tu
Kuna vitu kama hujui usidhani wote hawajui na hiinndo shida ya kuwa online wanahisi wote mko sawa ....

OK Sawa kama utapata muda Nenda pitia Sheria ya mwenendo wa mashauri Ya madai...

sas kwa mfano umepelekwa Mahakamani kwa kesi ya madai ya fedha fulani na mahakama ikahukumu kuwa unapaswa kulipa deni hilo kwa muda fulani l,Kitendo cha kukaidi kulipa deni hilo huchukua sura mpya ya kisheria ambayo ni kukaidi amri ya mahakama na hali hii ya kisheria sio madai tena bali ni jinai n inatakiwa ukamatwe au mali zako zikamatwe.....Sasa kifungu cha 44 (1) cha sheria Ya mwenendo wa mashauri ya jinai kinasema mdaiwa anaweza kukamatwa kwa muda wa siku yoyote kama atashindwa kufata amri ya mahakama

Na akikamatwa akafungwa Deni litakuwa limeisha? jibu ni No;kifungu cha 46 kinaeleza kuwa Utafungwa ukimaliza kifungo deni linaendelea pale pale kwa sababi kilichokufunga sio Deni ni ukaidi

Sasa siku nyingine uwe unajua sio kila mtu anayejibu anajua na sio kila mtu asiyejibu hajui Shida kubwa ya vijana ni Akili mnakosa sana na hekima mmeipoteza...Kilichomi kichwani ni Nywele na maji kwwnye ubongo tu akili hamna
 

Hapa kila njia ina gharama yake. Tatizo ameshatanguliza kutokuwa mwaminifu. Labda kama wewe kama ndugu na una uwezo wa kuongezea uaminifu pia.

1: Kupimana ubavu na kuangalia weakness kwenye njia za kupewa mkopo dhidi
ya kampuni kwa kupeleka kesi mahakamani.

Vitu vinavyoweza kuvipata ni kutizama marejesho yake yawe ndani ya taratibu za kisheria au kampuni kama inajua kuna weakness huomba majadiliano nje ya mahakama.

Hapa awe na uhakika kama taratibu hazikufuatwa au kampuni hazifuati taratibu za uendeashaji wake kwa mujibu wa sheria husika , ingawa pia hela itamtoka kwa wanasheria, stress na muda wake.

Hii itoke kwa wanasheria baada ya upembuzi yakinifu wa mazingira yake yote.

2: Wewe kama sehemu ya mhusika kwenda na kukaa na wakopeshaji pande zote mbili, kila mmoja kwa wakati wake. Kuangalia kama mnaweza ku-adjust return za mikopo kwa kuongeza muda wa kurejesha (muda wa maisha ya mkopo) na kupunguza kiasi anajorejesha kwa mwezi ili hela anayopata iweze kukidhi kuhudumia mikopo yote miwili. Ingawa kiasi cha jumla ya return kitaongezeka (pesa ya marejesho kwa ujumla).

Hapa tatizo ni uaminifu aliokwisha uvunja, labda dhamana iongezeke ikijumuisha wewe ndugu au vyovyote iwavyo.

3: Nyinyi ndugu kumdhamini ndugu yenu na kumlipia deni mojawapo au yote. Mbaki kudaiana binafsi bila riba.
Jitafakarini kwa manandugu mwenye uwezo au kwa kuchanga pamoja.
 
Huyo Mpwa wako ndio wewe mwenyewe,

Dawa ya deni ni kulipa,unataka ushauri wa kukwepa deni?
Maisha hayajawahi kua rahisi kihivyo,tafuta hela ukalipe deni lako,
Hapa JF utapata kila aina ya maelezo But at the end ni deni lilipwe tu that's all.
Hamuijui tu pesa x nyie
 
Mdaiwa hafungwi.... misemo ya kiswahili
 
Au huyu jamaa namuonaga kidimbwi hapa
Kazungukwa na pisi kali wakila kamnyweso
Kumbe alikopa kudadeki [emoji3061][emoji3061][emoji3061]🦥
 
Unapenda ligi tu. Suala lilikuwa ni deni halimfungi mtu. Nikasema si sawa. Hapo juu umezungumza nini sasa? Au ndugu yetu unasoma kama kasuku hiyo sheria? Kwanza hukueleza kuwa anapopelekwa (mdaiwa aliyekaidi amri ya mahakama), anatakiwa kuwekewa mazingira, huko gerezani sawa na maisha yake ya kila siku. Kama huwa anaangalia TV ya inchi 120 lazima mdai ahakikishe inawekwa gerezani: kama anakula pilau kila siku, mdai anatakiwa agharamie hiyo pilau gerezani. Hapo ndipo huwa mdaiwa huwa anachomoka na kifungo husika. Upo hapo
 
Kuomba msamaha na kumaliza moja na kuanza kulipa jingine inwezekana, na kulipa kidogo kidogo kote inawezekana pia, sijui Sheria ya benki kuu inasemaje kwenye hilo. All debts are online be careful
 
Deni dogo hilo ata halivuki 4m...Hapo wakimbana sana anaweza kulimaliza kwa miaka miwili tu na wakati huo anabakia na robo ya mshahara wake.

Hawawezi mfunga sema wanamtikisa tu, atulie tu hao kausha damu waliochukua kadi ya benkinwasubilie hadi wenzao walio enda kwa mkurugenzi wake kupata kibari cha kukopeshwa wamalize mkopon wao ndipo nao wachukue chao.

Ila jamaa ndiyo atasugua benchi mno atafute kazi ya kufanya kumuongezea kipato.....hakuna deni juu ya deni.
 
Kwenye uchumi debt servicing ni option pia.

Shida yetu wengi hua ni kwamba tunakopa ili kutumia siyo kuzalisha. So hata debt servicing tukiifanya ni tunakua tunaharibu zaidi.
 
Hiyo ndo njia peke hamna micro finance inao taka kuenda mahakamani ata iwe benki wanaogopa gharama na sheria nyingi wanazo ruka, kwa hiyo asiogope kukaa cell kwa mda mwezi au mwezi miwili.
 
Deni halimfungi mtu hata waende mahakamani bado ataambiwa alipe hata ikibidi kulipa 2500 kila siku ni sawa, mwambie asiogope kukamatwa tena wampeleke mahakamani kesi itakua rahisi zaidi
 
Huyo mkapaji jinsia yake tafadhali?
Kama ni KE atapata msaada wa fedha chap kwa haraka vigezo na masharti kuzingatiwa ila kama ni ME kwakweli akaze mattyakko tu there is no way.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…