Pre GE2025 Nahitaji Peter Msigwa auambie umma wa Watanzania ataufanyia nini baada ya kuhama CHADEMA, siyo CHADEMA imefanya nini!

Pre GE2025 Nahitaji Peter Msigwa auambie umma wa Watanzania ataufanyia nini baada ya kuhama CHADEMA, siyo CHADEMA imefanya nini!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2018
Posts
2,345
Reaction score
6,970
Screenshot_20240721-070949_1.jpg

Mchungaji Msigwa

Ukihitaji salamu subiri kwanza Utopolo wamkung'ute, Kolo 5 - 1 hiyo tarehe 8, tofauti na hapo utaula wa chuya!

Bado nashangazwa sana na Siasa anayoifanya mtu mzima Peter Msigwa, sababu ya yeye kuhama CHADEMA alisema ni uminywaji wa Demokrasia huku lawama kibao akimtupia aliyekuwa Mwenyekiti wa chama chake cha zamani Freeman Mbowe.

Nadhani sasa ni muda huyu jamaa akatuambia baada ya kuihama CHADEMA atakuja na mikakati gani ya kuisaidia CCM kushinda uchaguzi na kuwasaidia Watanzania kuondokana na Lindi la Umasikini kuliko kila siku kuisema CHADEMA kana kwamba alihama huko ili aiseme!

Mimi binafsi nataka anieleze ni namna gani ataisaidia CCM kutatua tatizo la AJira kwa watu wake.

Mimi binafsi nataka anieleze ni kwa namna gani ataisaidia serikali ya CCM kutatua tatizo la vijana kutekwa, kuuawa na kupotezwa na hao wanaojulikana kama "Watu wasiojulikana".

Mimi binafsi nataka kuona ni namna gani anaweza kuwasaidia wana Iringa kuondokana na kero ya muda mrefu ya ukosefu wa maji salama ya kunywa!

Mimi binafsi nataka kuona anawanadi wana Iringa kwenye chama chake kipya ili watu wengi waunganishwe kwenye Umeme!

Mimi binafsi nahitaji kuona anawapigia kelele Watanzania na wana Iringa kuhusu Barabara ambazo zimekuwa kikwazo kwao.

Yangu ni hayo tu leo.

PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Mchungaji Msigwa: Nitazunguka Nchi nzima kuelezea Uongo wa CHADEMA

- Kuelekea 2025 - Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa ahamia CCM
 
Msigwa kajimaliza sana. Hakuna anayemsikiliza, Wangapi wanahama wanaisema chadema lakini wapi hili li chama sasa hivi limekomaa dr Slaa msikilizeni hoja zake anakifahamu chama na mifumo yake. Si rahisi kukivuruga nyie kuleni hiyo pesa mliyopewa na pesa pia.
 
Mchumia tumbo huyo hana jipya. Uchungaji umemshinda ndio atakuwa na la maana lipi sasa!!
 
Anafanya ujinga tu.
Yani amekata chadema zaidi ya miaka 25, chadema hawakumfanyia jambo jema hata 1.
Wamempa Jimbo akawa mbunge, akawa kiongozi wa Chama hayo madhaifu hayakosi na mtu mwenye busara si vyema kusema madhaifu ya ulipotoka.
Na CCM watamwogopa wanaamini siku akihama atawapaka tope.
Aige Kwa Lowasa, Sumaye, Nyarandu
 
Back
Top Bottom