nahitaji, sina wazo nifanye biashara gani kwa mtaji wa laki 8 mpaka 1 m

Mr worldwide

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2017
Posts
348
Reaction score
740
Habari wajuvi wa Jf

nimekuwa na matamanio ya kufanya biashara yoyote halali ili niweze kujikomboa kiuchumi na kupiga hatua kimaisha kama kijana

katika harakati za kupambana kutafuta kianzio, nimejitahidi sana kwa hali ya juu zaidi kuaccumulate kiasi cha pesa kinachorange kuanzia laki 8 hadi milion 1 kama mtaji wa biashara.

Mtaji ninao sasa, nahitaji na ninatamani kuwa na biashara itakayonipa faida ya kupiga hatua kimaisha kimaendeleo
naombeni mnipe mawazo yenu ya biashara gani nifanye kwa nyakati hizi, kwa location napatikana jijini Dar es salaam Pugu

nawasilisha
 
Ngoja waje mkuu.
Ila binafsi naona uwekeze kwenye chakula yaan nafaka (mpunga, mchele)..,unanunua kwa wakulima kipindi cha mavuno afu ww unauza bei pungufu na ile ya dukani. Utapata wateja weng sana ila tu mzigo uwe mzuri.

Wengne wanasema M-PESA, TIGOPESA, n.k
 
Kumbe upo dar bhna fanya biashara ya chakula pika chakula kitamu uza....
Wateja utapata tu na iyo laki nane inatosha kabisa, pikia nyumbani tafuta fremu na kitambulisho Cha 20000 Kodi viti vya plastic kwa Bei nafuu baadae nunua vyako pika mchana na asubuhi supu chapati chai maandazi tafuta msaidizi pamoja na wewe mfanye iyo kazi.... Ukiaachi mtu kazi hupati faida utafunga mwezi haujaisha..
 
Mkuu nunua daa nyama(mchele), kwa bei ya jumla kisha kauze minadani kama reja reja.
 
asante sana mkuu
 
asante kwa mawazo yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…