Nahitaji ufafanuzi wa kodi ya biashara

Nahitaji ufafanuzi wa kodi ya biashara

Blauzi mbovu

Member
Joined
Oct 30, 2021
Posts
39
Reaction score
35
Habari zenu wakuu !

Leo nakuja kwenu nikihitaji ufafanuzi wa masuala kadhaa yanayohusisha kodi ya biashara.

Ni kiasi cha miaka minne sasa tangu niingie ktk ulingo wa kutafuta maisha kupitia biashara.
Nimekuwa nikihangaika na biashara tofauti tofauti za kila namna lengo niingizie kipato ambacho kitaendesha maisha yangu na ya familia yangu.

Nimewahi kufanya biashara ya kuuza viatu vya mtumba mtaani, nimeuza mchele, pumba, madagaa nk.

Lakini katika mihangaiko yangu yote sijawahi kujua ni nani ktk wafanya biashara anapaswa kulipa kodi.

Nilipkuwa nikiuza viatu niliambiwa nikate kitambulisho cha mlipa kodi (20,000/-) kwa mtendaji, nikaenda nikakata, Nikifahamu sababu ya kuambiwa hivyo ni udogo wa mtaji wangu ambao ulikuwa chini ya milioni 4.

Kwa sasa nimeshaacha hiyo biashara baada ya kuona hailipi,
Nimeamua kutafuta frem na kufungua biashara ya vitu vya kupima ambayo pia mtaji wake hauvuki milioni 4.

Haikuchelewa wakaja TRA kunihoji kama nina TIN# na kama nimeshakadiriwa kodi. Nikawaambia mie huwa natumia kitambulisho cha mjasiria mali kwa kuwa mtaji wangu ni mdogo. Wakasema hapana hatuangalii mtaji, wakanambia ukifanya tu biashara kwenye "FREMU" tayari unaingia tk walipa kodi wa biashara.
Hili likanishangaza ! Lkn kwa kuwa wao ndio wataaluma wa mambo hayo nikakubaliana nao nikaenda ofisini kwao wakanikadiria kodi ambayo mpaka sasa nalipa.

Leo nakuja kwenu wanajamii forum mniondolee ule mshangao kwa kuwauliza;

Hivi ni kweli "FREMU" ya biashara ndio kipimo cha mtu kulipa kodi ya biashara ?
Pili, uelewa wangu wa kuwa ili ulipe kodi ya biashara ni lazima uwe na mtaji unaoanzia mioni 4 ? Na kama sio, basi ni kuanzia mtaji kiasi gani utalazimu mtu aingie ktk kodi ya biashara ?


Ni hayo tu ndugu zangu, niwatakie siku njema.
 
Ulifanikiwa kupata jibu la swali lako?
Habari zenu wakuu !

Leo nakuja kwenu nikihitaji ufafanuzi wa masuala kadhaa yanayohusisha kodi ya biashara.

Ni kiasi cha miaka minne sasa tangu niingie ktk ulingo wa kutafuta maisha kupitia biashara.
Nimekuwa nikihangaika na biashara tofauti tofauti za kila namna lengo niingizie kipato ambacho kitaendesha maisha yangu na ya familia yangu.

Nimewahi kufanya biashara ya kuuza viatu vya mtumba mtaani, nimeuza mchele, pumba, madagaa nk.

Lakini katika mihangaiko yangu yote sijawahi kujua ni nani ktk wafanya biashara anapaswa kulipa kodi.

Nilipkuwa nikiuza viatu niliambiwa nikate kitambulisho cha mlipa kodi (20,000/-) kwa mtendaji, nikaenda nikakata, Nikifahamu sababu ya kuambiwa hivyo ni udogo wa mtaji wangu ambao ulikuwa chini ya milioni 4.

Kwa sasa nimeshaacha hiyo biashara baada ya kuona hailipi,
Nimeamua kutafuta frem na kufungua biashara ya vitu vya kupima ambayo pia mtaji wake hauvuki milioni 4.

Haikuchelewa wakaja TRA kunihoji kama nina TIN# na kama nimeshakadiriwa kodi. Nikawaambia mie huwa natumia kitambulisho cha mjasiria mali kwa kuwa mtaji wangu ni mdogo. Wakasema hapana hatuangalii mtaji, wakanambia ukifanya tu biashara kwenye "FREMU" tayari unaingia tk walipa kodi wa biashara.
Hili likanishangaza ! Lkn kwa kuwa wao ndio wataaluma wa mambo hayo nikakubaliana nao nikaenda ofisini kwao wakanikadiria kodi ambayo mpaka sasa nalipa.

Leo nakuja kwenu wanajamii forum mniondolee ule mshangao kwa kuwauliza;

Hivi ni kweli "FREMU" ya biashara ndio kipimo cha mtu kulipa kodi ya biashara ?
Pili, uelewa wangu wa kuwa ili ulipe kodi ya biashara ni lazima uwe na mtaji unaoanzia mioni 4 ? Na kama sio, basi ni kuanzia mtaji kiasi gani utalazimu mtu aingie ktk kodi ya biashara ?


Ni hayo tu ndugu zangu, niwatakie siku njema.
 
Cha kwanza kabisa kodi huwa inatozwa katika vitu vikuu viwili. Turnover (mauzo) na profit (faida).
Kodi inayotozwa kupitia mauzo kwa mwaka. Kama mauzo yako yapo chini ya 4M kwa mwaka ww unapewa NIL Assesment (makadirio ya sifuri) kwa maana hulipi kitu. Na una sifa za kutumia kitambulisho cha wale machinga. Km mauzo yko ni kuanzia Million 4 na kuendelea ww unashathili kulipa kodi kulingana na mauzo yako yatavyokuw kwa mwaka.
Na wale wanaokadirio kupitia faida ni huwa wanaandaa mahesabu hivyo kodi hutozwa kupigia faida inayopatikana.
Na kwa mawakala wao huwa hawalipi kodi kodi huwa ndo zile zinazokatwa kwny miamala japo wanastahili kufanya makadirio ya sifuri kila mwaka unavyopinduka.
 
Sio mtaji ni mauzo
Kifupi
1. Kama una mauzo chini ya 15,000 kwa siku yaani mauzo ya chini ya 4mil kwa mwaka basi wewe ni WA KITAMBULISHO
3. Kama una mauzo ya zaidi ya 15,000 kwa siku yaani mauzo ya zaidi ya mil 4 kwa mwaka wewe ni WA kodi na leseni ya halmashauri.

Kuhusu mtaji:
Hili swala ndio Magu alizingua, aliwalisha machinga matango pori ya kuangalia mtaji wakati sheria inasema mauzo.

#YNWA
 
Shukran sana kwa majibu yenu, ingawa
Cha kwanza kabisa kodi huwa inatozwa katika vitu vikuu viwili. Turnover (mauzo) na profit (faida).
Kodi inayotozwa kupitia mauzo kwa mwaka. Kama mauzo yako yapo chini ya 4M kwa mwaka ww unapewa NIL Assesment (makadirio ya sifuri) kwa maana hulipi kitu. Na una sifa za kutumia kitambulisho cha wale machinga. Km mauzo yko ni kuanzia Million 4 na kuendelea ww unashathili kulipa kodi kulingana na mauzo yako yatavyokuw kwa mwaka.
Na wale wanaokadirio kupitia faida ni huwa wanaandaa mahesabu hivyo kodi hutozwa kupigia faida inayopatikana.
Na kwa mawakala wao huwa hawalipi kodi kodi huwa ndo zile zinazokatwa kwny miamala japo wanastahili kufanya makadirio ya sifuri kila mwaka unavyopinduka.
Shukran ndugu nimeelewa.
 
Asa
Sio mtaji ni mauzo
Kifupi
1. Kama una mauzo chini ya 15,000 kwa siku yaani mauzo ya chini ya 4mil kwa mwaka basi wewe ni WA KITAMBULISHO
3. Kama una mauzo ya zaidi ya 15,000 kwa siku yaani mauzo ya zaidi ya mil 4 kwa mwaka wewe ni WA kodi na leseni ya halmashauri.

Kuhusu mtaji:
Hili swala ndio Magu alizingua, aliwalisha machinga matango pori ya kuangalia mtaji wakati sheria inasema mauzo.

#YNWA
Asante kwa ufafanuzi
 
Cha kwanza kabisa kodi huwa inatozwa katika vitu vikuu viwili. Turnover (mauzo) na profit (faida).
Kodi inayotozwa kupitia mauzo kwa mwaka. Kama mauzo yako yapo chini ya 4M kwa mwaka ww unapewa NIL Assesment (makadirio ya sifuri) kwa maana hulipi kitu. Na una sifa za kutumia kitambulisho cha wale machinga. Km mauzo yko ni kuanzia Million 4 na kuendelea ww unashathili kulipa kodi kulingana na mauzo yako yatavyokuw kwa mwaka.
Na wale wanaokadirio kupitia faida ni huwa wanaandaa mahesabu hivyo kodi hutozwa kupigia faida inayopatikana.
Na kwa mawakala wao huwa hawalipi kodi kodi huwa ndo zile zinazokatwa kwny miamala japo wanastahili kufanya makadirio ya sifuri kila mwaka unavyopinduka.
Samahani mkuu, kwa nini hapa TZ hata biashara yenye business name au kikundi kipo kwenye category ya Corporate tax sawa na makampuni?
 
Samahani mkuu, kwa nini hapa TZ hata biashara yenye business name au kikundi kipo kwenye category ya Corporate tax sawa na makampuni?
Corporate tax ni kwa kampuni tu iliyokuw registered na Brela. Kikundi iyo ni Association. Unaweza ukawa mtu wa kawaida na biashara yko ina ina business name na usiwekwe kwny category ya kampun
 
Corporate tax ni kwa kampuni tu iliyokuw registered na Brela. Kikundi iyo ni Association. Unaweza ukawa mtu wa kawaida na biashara yko ina ina business name na usiwekwe kwny category ya kampun
Tulishawahi kuonba kupewa TIN ya kikundi tukaishia kuingia kwenye corporate tax, sasa sijui walitumia kigezo kipi kutuweka hapo wakati bafo hatujaanza operations.
 
Sijajua alitumia kigezo gan lakn vikundi ni association japo kwny ulipaji wa kodi inaiandikwa CIT lkn haina maana km iyo ni kampun
 
Back
Top Bottom