Nahitaji ushauri wa kisheria

mushisg

Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
18
Reaction score
1
habari za majukumu wana jamii forum; naomba ushauri kadri inavyowezekana, mm ni mtaalamu wa miamba yaani mjiolojia nilipata mteja akiomba kuandikiwa ripoti ya kijiolojia katika eneo lake!

haikuwa rahisi maana hajawahi kuwa na andiko lolote lilowahi fanyiwa utafiti kwenye eneo hilo, kweli nilienda kwenye eneo la kazi nikapata taarifa kadri ilivyowezekana japo haikuwa rahisi maana awali alinieleza kuna mashimo 2 wanayafanyia kazi kitu ambacho ingekuwa rahisi kupata taarifa za kutosha ili kufanya "pit development" nilipofika sikukuta chochote "abandoned pits" nikawaeleza wasafishe likasafishwa shimo 1 ambalo kwa siku 3 then nilichukua taarifa zake nikajumuisha na ambazo nilikusanya kuzunguka eneo lote wanalomiliki. nikakabidhi taarifa ya kijiolojia.

Mjadala uliopo: mara baada ya kukabidhi nakuipeleka wanakohitaji wakanieleza kuwa taarifa nilowapa haitoshelezi kutengeneza plan ya mgodi sasa nimejaribu kutoa maelezo ya kuwa hiyo ni hatua inayofuata phase II yatakiwa waandae utaratibu wameng'ang'ana kuwa yote yalitakiwa yakamilishwe ndani ya ripoti moja.

Kitaalam: utafiti wa madini una hatua tofauti na kila hatua moja kutoa mwanga kwa hatua inayofuata.nimeonesha kwenye hitimisho la ripoti nilowapatia.
Mzozo: yaonekana umekuwa ni wa kisheria zaidi maana wamenieleza nikutane nao twende kwa mwanasheria tukafanye kikao...
Naomba ushauri wenu nini nifanye.

Natanguliza shukrani
 
Kabla ya kazi mliandikishiana?
Uliwaeleza habari za phase ll kabla ya kuanza hiyo phase l?
 
hatuandikisha na wala hakuna namna unayoweza kushauri hatua inayofuata pasipo kufanya utafiti na kuandika ripoti
 

Weka report hapa tuongee
 
hatuandikisha na wala hakuna namna unayoweza kushauri hatua inayofuata pasipo kufanya utafiti na kuandika ripoti

kwahiyo hata hujui ni nani uliingia nae kwenye "makubaliano"

aidha huyo mtu uliyejadiliana nae ama kampuni unayowakilisha.
unadocument gani hata kwa baadae kuthibitisha ulimfanyia/uliwafanyia kazi?


tafuta msaada wa kisheria karibu nawe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…