Nahitaji zaidi ya msaada!

Mwendabure

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2011
Posts
2,138
Reaction score
1,044
Waungwana salam! Mimi ni kijana mwenye elimu ya darasa la saba nipo Dar. Napenda TEKNOHAMA (Teknolojia ya habari na mawasiliano) kiasi nimeweza kujifundisha kutumia kompyuta si haba! kwa msaada wa kibarua mwenzangu na juhudi binafsi nilifanikiwa kununua kompyuta (laptop)kuukuu ambayo inaonyesha dalili zote za kuchoka kabisa. Basi waungwana naomba mnifahamishe ni aina gani ya kompyuta itanifaa na ikiwezekana na mahali muafaka ambapo nitapata pia maelekezo na ushauri wa ziada kwa kuzingatia uchanga wangu ktk ulimwengu wa kompyuta na elimu ya kutosha ya darasani. Kwani kila ninapoenda sipati msaada ninaohitaji zaidi ya wahusika kuwaka tamaa na uchu wa fedha zangu na kutaka kunibambika 'kimeo' hasa baada ya kuwaeleza wazi kuwa sina weledi sana ktk mambo ya kompyuta. Nahitaji msaada wenu na natanguliza shukrani za dhati!!
 
Mkuu, ili tuweze kukusaidia unge tuambia bajeti yako ikoje ili tuweze kukushauri kulingana na kiasi cha pesa ulicho nacho....


Mkuu, hata siku moja usifanye kitu ulicho kifanya cha kuwaeleza wafanya biashara kiwango chako cha elimu, wao wako kibiashara zaidi, wanaweza kutumia mapungufu yako kujinufaisha kibiashara...

Siku nyingine ukihitaji vitu kama hivi unapaswa kumtafuta mtu ambaye anaujuzi navyo, ambaye unaweza kuenda nae kuchagua...
 
ningekushauri uende chuo kuna vyuo vingi sana vya kufundisha computer na kutengeneza hapo utapata elimu ya kutosha kabisa kuanzia hapo utaweza kupata ufahamu ata wa laptop unayoitaji kwa ss vumilia na hicho kmeo walichokupiga nacho ucwe na papara ss tulia kasome kisha utakuwa na ufahamu na utoweza kudanganywa tna
 
Bajet yangu kaka ni laki 4 kwa laptop iliyotumika (mtumba)
 
Nina mpango huo kaka ila nadhani itakuwa vema kama nitakuwa na kimeo changu cha kufanyia mazoezi japo. Asante kwa ushauri.
 
1.6 ghz intel celeron,1Gb of ram,40 or 80 hdd,nadhan kwa hyo bei unaeza ukapata,heb chek jukwaa la matangazo madogo madogo mkuu..
 
1.6 ghz intel celeron,1Gb of ram,40 or 80 hdd,nadhan kwa hyo bei unaeza ukapata,heb chek jukwaa la matangazo madogo madogo mkuu..

Nhmekusoma.. Aksante sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…