Nahodha wa Aston Villa katika mchezo wa kufuzu kucheza EPL avaa viatu chakavu akidai ni vitu vyake vya bahati!

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Mchezaji na nahodha wa timu ya Aston Villa iliyofanikiwa kupanda daraja baada ya kuifunga Derby County goli 2-1, Jack Grealish aeleza sababu za kuvaa viatu vilivyochakaa kwenye mchezo huo

Amesema "Baada ya kupata majeraha kwa muda na kurejea uwanjani nilivitumia vikiwa vipya kabisa, wakati huo nilipata kufunga magoli kadhaa na kutoa pasi kadhaa za magoli."

Ameongeza kuwa "Niliona hivi ni viatu vyangu vya bahati, hivyl nikaamua kuvihifadhi. Leo katika mchezo wa kupanda daraja tulihitaji bahati ili kushinda kwa ajili hiyo nikavivaa."

Aston Villa msimu ujao itakuwa ikicheza Ligi Kuu ya England. Jack ana kowango bora sana ila bado nawaza kama viatu hivyo vitamsaidia kuwa mchezaji bora au hata kuwa miongoni mwa wafungaji bora
 
Asije navyo
Asije navyo Bongo, ataombwa au watapora
 
Daah sipati picha angevaa mchezaji wa Simba............ yani mpaka ambaye hafuatilii mpira angejua. 😐😐
 
Hilo tukio lingetokea bongo hapa,sijui ingekuwaje
 
Hakukaguliwa kabla ya game? Dah tuendapo kampuni kubwa za vifaa vya michezo kama Adidas, na Nike watakuja na huo ubunifu.
 
Hicho hata Adam Salamba na Pasco Wawa hawaombi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…