Naibu Rais Mh Rigathi Gachagua: Tunaingia ofisini Kenya ikiwa na serikali imefilisika kifedha na kiuchumi

Naibu Rais Mh Rigathi Gachagua: Tunaingia ofisini Kenya ikiwa na serikali imefilisika kifedha na kiuchumi

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
13 September 2022
Nairobi, Kenya

HOTUBA MARA BAADA YA KUAPISHWA NAIBU RAIS MH. RIGATHI GACHAGUA



Naibu wa Rais wa Kenya Mh. Geoffrey Rigathi Gachagua amewaelezea raia wa nchi hii ya Kenya kuwa hali si hali pamoja ya kuwa ni nchi inayohesabika ina uchumi mkubwa na utajiri katika eneo hili la Afrika ya Mashariki lakini awamu hii mpya chini ya rais William Ruto imepokea serikali ambayo imefilisika na naibu rais Geoffrey Rigathi Gachagua bila kupepesa macho amewaambia wananchi waelewe kuwa huo ndiyo ukweli.

Pia pamoja na pigo hilo kukuta fuko la fedha la nchi likiwa tupu huku nchi inadaiwa madeni makubwa lakini chini ya uongozi wa rais wa tano William Ruto watafanya kazi usiku na mchana kuirudisha nchi katika uchumi mzuri na hifadhi ya kutosha ya akiba ya fedha kama ilivyokuwa wakati wa rais Mwai Emilio Kibaki miaka kumi iliyopita yaani 2012.

Anaongeza makamu wa rais Geoffrey Rigathi Gachagua kuwaambia ukweli kuwa wananchi kuwa pia kwa hali ya raia mmoja mmoja kwamba anaelewa hali yao ya kiuchumi ni mbaya, watu milioni 6 hawana ajira huku raia milioni 14 ni wakopaji sugu wenye madeni ya kutisha wanayoshindwa kuyalipa kiasi wameingizwa ktk rejista kuwa hawafai tena kuaminika, lakini kuanzia siku ya kwanza ofisini Rais William Ruto na wasaidizi wake watafanya kila juhudi kurekebisha hali hiyo ngumu na mbaya iliyopo serikalini na kwa wananchi wa kawaida.

Hotuba hiyo ya Naibu wa rais katika awamu hii mpya inayoingia ya rais William Ruto mbele ya maelfu ya watu katika uwanja wa kisasa wa Kasarani jijini Nairobi huku rais anayemaliza muda wake Mh. Uhuru Kenyatta akiwa mita chache akisikiliza kwa makini hotuba hiyo inayochambua awamu iliyopita ya Uhuru Kenyatta.
 
Reciprocity with equality, I thank you Mr Gachagua for being straight and realistic. He went through hell under the outgoing regime chair, Those who don't know Gachagua should observe the highest order of silence. I insist he went through real hell, his feeling of relief is awesome, am happy he showed it with zeal, vigour and with sincerity.
 
Gachagua amsifu Rais Ruto akimtaja kama kiongozi atakayeimarisha Kenya


Gachagua Amsifu Rais Ruto Akimtaja Kama Kiongozi Atakayeimarisha Kenya​


NA SAMMY WAWERU

NAIBU wa Rais Rigathi Gachagua amemmiminia sifa Rais William Ruto, akimtaja kama kiongozi mchapakazi.


Akihutubu Jumanne katika uwanja wa Kasarani, Nairobi baada ya wawili hao kuapishwa, Bw Gachagua amesema Dkt Ruto ametekeleza vilivyo majukumu aliyopewa katika serikali za awali.

Bw Ruto amewahi kuhudumu kama Waziri wa Elimu na Kilimo, wakati wa utawala wa Rais mstaafu Mwai Kibaki ambaye kwa sasa ni marehemu.

Katika serikali ya Jubilee 2013 – 2022, iliyoongozwa na Rais ambaye ameondoka, Uhuru Kenyatta, alihudumu kama naibu wa rais.

“Ninaomba Wakenya msiniweke kwenye mizani mnilinganisha na rekodi ya utendakazi wa Rais William Ruto,” Gachagua akasema.

“Huenda nikazoa kati ya asilimia 60 – 70, na tunaposonga mbele ninahimiza Wakenya tufanye kazi kwa bidii,” akaelezea.

Naibu wa Rais vilevile amewataka Wakenya kupenda na kuthamini familia zao, akidai alipohangaishwa na serikali ya Jubilee mkewe na wanawe walisimama naye kidete.

“Mchunge familia zenu…Familia haiwezi ikakuacha unapopitia changamoto,” akasihi.

Bw Gachagua amekuwa akinyooshea kidole cha lawama serikali ya Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, akisema imekuwa ikimhangaisha.

Katika awamu ya pili ya Jubilee, alihudumu Gachagua alikuwa Mbunge wa Mathira

Source : Gachagua amsifu Rais Ruto akimtaja kama kiongozi atakayeimarisha Kenya – Taifa Leo
 
18 September 2022
Nairobi, Kenya

Many Kenyans are allergic to truth- DP Rigathi Gachagua



Source : KTN News
 
18 September 2022
Nairobi, Kenya

You cannot borrow money to subside consumption, that’s foolish, Rigathi Gachagua on cost of Fuel


Source : KTN News
 
Reciprocity with equality, I thank you Mr Gachagua for being straight and realistic. He went through hell under the outgoing regime chair, Those who don't know Gachagua should observe the highest order of silence. I insist he went through real hell, his feeling of relief is awesome, am happy he showed it with zeal, vigour and with sincerity.
Alifanywa aje? Tuelezee!
 
18 September 2022
Nairobi, Kenya

You cannot borrow money to subside consumption, that’s foolish, Rigathi Gachagua on cost of Fuel


Source : KTN News
Dadadeq. Hivi ndio kitu serikali ya samia wanafanya
 
19 September 2022
Nairobi Kenya

Gavana wa Benki Kuu, Deni la Taifa Ni Kubwa, Halihimiliki. Aliomba Bunge kutimiza wajibu wake kuishauri serikali



Patrick Njoroge, Gavana wa benki kuu ya Kenya CBK ameonyo hali ipo mbaya nchi imeelewewa na deni kubwa la Taifa.

Afananisha ugumu wa hali ya sasa na kuwa ikiwa serikali ikaamua kugeuka mwana-wa-mazingaombwe anayecheza sarakasi kwa kupita ktk kamba nyembamba iliyotundika juu sana baina ya ghorofa mbili, mazingira hayo ni ya hali ya hatari lolote linaweza kutokea ikiwa serikali itataka kukopa zaidi.


Gavana Patrick Njoroge aliyasema hayo mbele ya semina maalum elekezi kwa wabunge wanaotarajia kuingia ktk bunge la 13 baada ya uchaguzi mkuu wa August 2022 katika hoteli ya Safari Park jijini amelishauri mhimili huo muhimu wa dola yaani Bunge kuisaidia serikali kwa ushauri kila inapotaka kukopa. Katika kila makusanyo ya serikali ya shilingi Mia, shilingi 40 inaenda kulipia madeni huku bado kuna matumizi muhimu kama mishahara, huduma za afya, ulinzi pia usalama, elimu nayo yanakula sehemu kubwa ya bajeti ya nchi. Hivyo miradi ya maendeleo inaweza kushindwa kupatiwa bajeti.

Awamu ya tano chini ya Rais William Ruto nayo kama alivyosema Gavana wa Benki Kuu tayari nayo ilitoa taarifa na ufafanuzi juu ya hali mbaya waliyoikuta mara baada ya kuapishwa ktk viwanja vya Kasarani jijini Nairobi kuwa wamepokea serikali toka mikononi mwa awamu ya tano chini ya Rais Uhuru Kenyatta ikiwa imefilisika kwa fuko kuu la fedha idara ya hazina likiwa limeachwa tupu .

Source : Citizen TV Kenya

More info :
Dr. Patrick Njoroge PhD
mfumkobei / inflation, juhudi endelevu za kudhibiti mfumkobei, kuimarisha uthabiti wa kiuchumi, kuimarisha imani ya wawekezaji na kuchochea kuimarika kwa upatikanaji wa mtaji kwa wafanyabiashara
Sifa na weledi wa gavana wa banki kuu ya Kenya, Dr. Patrick Njoroge :
GAVANA wa Benki Kuu ya Kenya (CBK) Patrick Njoroge ametawazwa kama Gavana Bora wa benki katika mataifa ya Kusini mwa Jangwa la Sahara, wakati wa tuzo ya mwaka huu ya watungaji sera bora, maarufu kama ‘2019 Global Markets Award’.

Bw Njoroge alitambuliwa na jarida la GlobalMarkets .... SOMA ZAIDI : WASIFU / BIO source : Njoroge Gavana Bora wa benki katika mataifa ya Kusini mwa Jangwa la Sahara – Taifa Leo
 
Gavana wa kaunti ya Kisii awa mbogo baada ya kugundua ufisadi wa kutisha



Gavana Simba Arati aitisha gwaride la utambuzi (roll call) la madereva na kugundua kuwa kuna madereva 256 wameajiriwa na kutiwa ktk payroll ya mishahara kwa kazi ya kuendesha gari za serikali ya kaunti ya Kisii wakati ofisi hiyo ina magari 82 tu.

Akiongoea mbele ya viongozi wenzake, gavana anatia shaka kwa hali hiyo kuna idadi kubwa ya wafanyakazi mahurani / ghost workers. Pia anaelewa kuwa madereva hao shifti zao siyo za masaa 24 kwa siku.

Pia bima / Insurance kwa madereva wamekatiwa kwa third party huku nyaraka za ofisi zikionesha ni comprehensive insurance ndiyo inayolipwa na wizara.

Gavana Simba Arati huyo aliyechaguliwa mwezi August 2022 anahoji, je ni ungwana kweli kufanya wizi huku hospitali zinahitaji fedha ili kuhudumia wananchi na madereva halali kukingwa kwa kupata bima inayowalinda.


Gavana Simba Arati amewashukuru watu waliompenyezea taarifa hizo na kuwataka waendelee kumpa taarifa ili aweze kufanya kazi yake sawasawa aliyotumwa na wananchi .

Source : citizen TV Kenya
 
28 September 2022
Nairobi, Kenya

Ruto : raia milioni 4 Kenya waliotiwa katika madeni buku (book) chechefu kiasi ya kushindwa kulipa, sasa kusaidiwa kutolewa ktk buku jeusi CRB



Rais William Ruto amebainisha kuwa hali hiyo imewafanya raia hao kushindwa kukopeshwa na taasisi zinazotambulika zilizosajiliwa.

Kwani raia hao milioni 4 wenye madeni sugu yasiyolipika wanaenda kukopa kwa wajanja mitaani hivyo kutozwa riba ya asilimia mpaka 1000%

Kuwa katika buku hilo jeusi la CRB linawatenga kiasi hata waajiri huwakwepa pale wanapobaini kuwa waajiriwa watarajiwa ni wadaiwa sugu hivyo mshahara watakaowapatia hautawatosha kufanya kazi kwa weledi na ufanisi pia waweza kushawishika kuomba rushwa, kuwa wadokozi au jakamoyo, mfadhaiko, wasiwasi, muwako na fukuto ktk nyonyo zao wakiwa kazi hivyo kutoa taswira hasi kwa wateja wa kampuni iliyowaajiri.

Rais Ruto amesema kuwa serikali yake ina mkakati wa kuwatoa ktk buku la aibu ikifika mwezi November 2022.

Ruto aliyasema hayo alipokuwa anazungumza na wadau wa taasisi za kifedha Safaricom, KCB, NCBA kuhusu kuwasaidia raia wote waweze kupata nafasi ya kufaidi huduma za kifedha ikiwemo mikopo, kutoa likizo ya siku tatu zisizo karibisha riba, overdraft n.k kutoka taasisi hizo rasmi.
 
Back
Top Bottom