Naibu Spika: Bunge litapitia Kanuni za Tozo za Miamala zilizoandaliwa na Waziri wa Fedha kuona kama hazikiuki Sheria!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Naibu Spika Dr Tulia Ackson amesema bunge litazipitia kanuni za sheria ya tozo za miamala ya simu zilizoandaliwa na waziri wa fedha ili kujiridhisha kama hazikinzani kazi itakayofanywa na kamati ya sheria ndogo ya bunge.

Endapo itaonekana kanuni ziko sawa basi sheria itapelekwa kwenye bunge zima

Source: ITV habari
 
^kuona kama hazikiuki sheria^ au kutafuta namna ya kuziondoa kwa vile ni kero kwa wananchi wote kwa ujumla, na wapiga kura wao kimahususi!???
 
Bunge linajiondoa kwenye hili la tozo, linamrushia mpira waziri kuwa ndiye aliyetunga
 
Yaani walikuwa wap kuzipitia kabla ya mnyonge kufikia hali ya kuwa hoi kiasi hiki[emoji116]??
 
Nchi haiwezi kwenda bila ya VYANZO VIPYA VYA MAPATO.....


#KaziIendelee
 
Dr Tulia amekurupuka kufunga lango la banda baada ya farasi kutimka. Kazi kweli kweli.
 
Issue siyo kukinzana, issue ni kwamba TOZO NI KUBWA kuliko uwezo wa watu kifedha. Tozo zilipandishwa kwa 100%, hiyo siyo sawa kabisa.
 
Bunge linajiondoa kwenye hili la tozo, linamrushia mpira waziri kuwa ndiye aliyetunga
Tulia yupo sawa. Sheria hutungwa na bunge, ila kununi/Sheria ndogo hutungwa na waziri wa wizara husika
 
Tuombe Mungu na uzima,, kama mambo yatakuwa hivi hivi na NEC itasimamia haki jiandaeni chama langu CCM kuwa wapinzani__________?
 
Bunge linapitishaje sheria inayokiuka sheria ?

Kazi ipo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…