Pre GE2025 Naibu Spika Mussa Zungu awaasa wabunge wasiogope kurudi majimboni. Awataka wapange maneno ya kwenda kusema majimboni

Pre GE2025 Naibu Spika Mussa Zungu awaasa wabunge wasiogope kurudi majimboni. Awataka wapange maneno ya kwenda kusema majimboni

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Naibu Sipika wa Bunge, Mussa Zungu amewataka wabunge wasiogope kurudi majimboni kwani kuna miradi mingi ya kuzungumzia na kuwa wameonyesha wana sifa za kurudi bungeni 2025.

“Niwapongeze wabunge kwa kazi nzuri mliyofanya kipindi hiki chote ambacho tuko bungeni, mmeonyesha umahiri wenu na mmeonyesha mna sifa za kurudi tena ubunge 2025.

Msiogope kwenda majimboni, nendeni majimboni hiki ni kipindi cha kwenda kuzungumzia faida ambayo tumeipata kutokana na uongozi mahiri wa Rais Samia Suluhu Hassan.

“Mpange maneno ya kwenda kusema jimboni, msiogope. Msiogope wajumbe, msiogope wagombea, mnayo maneno ya kusema msirudi na unyonge, na neno la mwisho ukiishi mbinguni usiogope radi,” amesema Zungu.
 
Hawana cha kuwaeleza wananchi zaidi ya kwenda kumsifia Rais!
 
Zungu anajua Mbinguni ni Wapi lakini?

Asiingize Mbingu kwenye Siasa zao 🐼
 
Waje wafanye wakati kazi amefanya Samia wao wasibiri mchamchaka wa kuteuliwa toka kwa kamati kuu na wajumbe maana sisi wenye Nia ya kumsaidia Samia tumeshajiandaa. *****
 

Naibu Sipika wa Bunge, Mussa Zungu amewataka wabunge wasiogope kurudi majimboni kwani kuna miradi mingi ya kuzungumzia na kuwa wameonyesha wana sifa za kurudi bungeni 2025.

“Niwapongeze wabunge kwa kazi nzuri mliyofanya kipindi hiki chote ambacho tuko bungeni, mmeonyesha umahiri wenu na mmeonyesha mna sifa za kurudi tena ubunge 2025.

Msiogope kwenda majimboni, nendeni majimboni hiki ni kipindi cha kwenda kuzungumzia faida ambayo tumeipata kutokana na uongozi mahiri wa Rais Samia Suluhu Hassan.

“Mpange maneno ya kwenda kusema jimboni, msiogope. Msiogope wajumbe, msiogope wagombea, mnayo maneno ya kusema msirudi na unyonge, na neno la mwisho ukiishi mbinguni usiogope radi,” amesema Zungu.
Swali fikirishi je kuna dalili za kukataliwa wakirudi majimboni? Ila sawa ni wabunge wa viti maalum na toka kule maporini
 
Duniani Kuna mambo!!

Kwamba wapange maneno🤔
 
Back
Top Bottom