Naibu Waziri Denis Londo Awaita Waliosoma JItegemee Kupiga Jeki Shule Yao

Naibu Waziri Denis Londo Awaita Waliosoma JItegemee Kupiga Jeki Shule Yao

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301


Kuelekea miaka 50 ya Shule ya Sekondari Jitegemee, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Denis Londo amewataka wananchi wakiwemo viongozi mbalimbali waliowahi kusoma katika shule hiyo ya jeshi kuunganisha nguvu kuwezesha maboresho ya miundombinu ya shule hiyo inayoonekana kuwa chakavu.

Naibu Waziri, Mhe. Denis Londo ametoa rai hiyo mkoani Dar es Salaam ambapo amesema Jitegemee imekuwa na mchango mkubwa katika Taifa, sio tu katika kutoa elimu ya nadharia bali kuwajenga vijana kuwa wakakamavu wakiwemo viongozi wenye uzalendo na nchi yao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule hiyo, Kanali Robert Kessy amesema shule itandelea kuwa mfano bora katika kutoa elimu inayolenga kumkomboa mtoto wa Kitanzania, sio tu kitaaluma bali hata kimaadili.

"Baadhi ya viongozi waliopo katika utumishi serikalini na sehemu mbalimbali ya nchi wametokana na maelezi yanayotolewa kwenye shule za jeshi ikiwemo hii ya Jitegemee," amesema Kanali Kessy.

Kilele cha Maadhimisho hayo ya Miaka 50 ya Jitegemee Sekondari kinatarajiwa kuwa Novemba Mosi, 2024 katika sherehe ambazo zitaambatana na harambee ya kuchangia maboresho ya miundombinu ya shule hiyo.
 
Huyu mwamba anaheshimiwa sana Scandinavia. Wale wote aliwafundisha vyuo mbali mbali Denmark, Sweden na Finland yani wanampenda na kumkubali kupita maelezo as one of their best lecturer ever.

Kuna mdada flani mrembo wa kizungu alipojua mimi ni mtanzania akamwaga mfulululizo wa sifa kuhusu Denis Londo.

Huyo mdada ni social worker kwenye taasisi flani ya kiserikali na anahodhi cheo cha juu.

Alikuja kushangaa Dinis kawa mbunge. Nadhani sasa atashtuka mwamba ni wazir.

Ina aminika ni kati ya watanzania wachache wakufunzi na wenye IQ za hatarii kuwahi kutokea nchini mwetu.

Halafu ana keep low profile tu.
 
Kumbe ni lecture huyu Londo, sikufahamu hilo.
Mkuu huyu jamaa hapendi kujikuza na kujionesha. Aliowafundisha wote nchi za skendinevia wana career za uhakina. Ni super lecturer anaheshimika sana. Jamaa ni scholar wa kipekee.
 
Kifaru kimoja cha jeshi kinatosha kuigeuza hiyo shule kuwa kama paradiso.
Ada za wanafunzi zinaendaga wapi
Fabian Massawe ndio akiiwezeaga hii shule
 
Ni wakati sasa kuigeuza hiyo shule kuwa chuo cha kati kuliko kuendelea kubakia kuwa sekondari. Maisha, mazingira na mahitaji ya shule za sekondari yamebadilika sana hapa Tanzania, uhitaji wa shule ya Jitegemee kuendelea kuwa shule ya sekondari haupo tena, kwa sasa inakufa kifo cha asili (nature death). Hiyo taasisi inapaswa kupigwa jeki ya kimawazo na sio pesa (Jeshi lina pesa nyingi na kupitia hiyo shule kwa miaka 50 imevuna pesa nyingi mnoo).

Neno JITEGEMEE lina maana kubwa katika falsafa ya kuanzishwa kwake, na waanzilishi wake walibeba maono haya, ijiendeshe (asiwe omba omba) na wahitimu wake waje kuishi kwa kujitegemea.
 
Back
Top Bottom