Naibu Waziri Mkuu, Dotto Biteko: Serikali ya Rais Samia Imefuta Tozo 370 Ili Kukuza Biashara na Uwekezaji

Naibu Waziri Mkuu, Dotto Biteko: Serikali ya Rais Samia Imefuta Tozo 370 Ili Kukuza Biashara na Uwekezaji

The Sunk Cost Fallacy 2

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2022
Posts
9,436
Reaction score
10,944
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati bwana Dotto Biteko amesema Serikali inayoongozwa na Rais Samia Imefuta zaidi ya tozo na kero 370 Kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji Nchini.

Bwana Biteko amesema hatua hiyo imechochea kukua Kwa biashara na uwekezaji Nchini akitolea mfano ongezeko la mahitaji ya umeme ya zaidi ya megawatt 400 ndani ya mwaka mmja Kwa na kufanya mahitaji kuongeza kutoka megawatt 1400 Hadi 1900 Kwa sababu ya uhitaji mkubwa wa umeme kwenye sekta ya viwanda.

==

Biteko.jpg
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko, alisema hayo jana Dar es Salaam alipokuwa akifungua Kongamano la Majadiliano ya Biashara na Uwekezaji Kati ya Serikali na Sekta Binafsi na Mkutano Mkuu wa 49 wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA).

Alisema kufutwa kwa tozo hizo kumepunguza Sh. bilioni 35 kwenye mapato ya serikali kwa mwaka na kwamba imefanya hivyo baada ya kusikiliza kero za wafanyabiashara.

Pia alisema serikali imepunguza muda wa kutoa huduma kutoka simu 14 hadi tatu na usajili wa hospitali binafsi, kutoka miezi 12 hadi siku tatu.

Alisema lengo la serikali kufanya hivyo ni kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, ili kuchochea ukuaji wa uchumi.

Dk. Biteko alisema serikali imefanya hivyo ili kuongeza mzunguko wa biashara ambao utaongeza mapato ya kodi, itakayotumika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na huduma za kijamii.

Alisema mbali na maboresho hayo, serikali imeimarisha bandari na miundombinu mingine, ikiwamo ujenzi wa barabara, meli, reli ya kisasa na ununuzi wa ndege ya mizigo.

Maboresho hayo, alisema yameongeza mahitaji ya umeme kutoka megawati 70.8 mwaka 2017/18, hadi megawati 420 mwaka huu.

“Mahitaji ya juu ya umeme Agosti mwaka jana yalikuwa megawati 1,410 lakini leo ni MW 1,888, ongezeko hili limekuja kwa sababu viwanda vingi vinajengwa na uchumi unachangamka,” alisema.

Dk. Biteko alisema serikali inatambua mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya nchi na kuwashauri wanachama wa TCCIA, kutumia malighafi za ndani katika kuzalisha bidhaa zenye ubora, zitakazoweza kushindana sokoni.

“Mchango wa sekta binafsi ni mkubwa na hauwezi kupuuzwa. Vijana zaidi ya milioni 12 wanaingia kwenye soko la ajira kila mwaka, asilimia 25 ndio wanapata ajira katika sekta rasmi. Asilimia 75 wanaingia katika sekta isiyo rasmi mkiwamo ninyi," alisema Dk. Biteko.

Rais wa TCCIA, Vicent Minja, alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuifungua nchi na kutatua changamoto za biashara.

Hata hivyo, aliomba mchakato wa kuandika sera ya sekta binafsi uharakishwe ili kuiweka kwenye mpangilio unaohitajika.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alisema dhamira ya serikali ni kuendelea kuifungua nchi na kuendeleza uhusiano mzuri na sekta binafsi ili kukuza uchumi wan chi.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa TCCIA, Oscar Kissanga, alitia saini mikataba minne ya ushirikiano na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Wakala wa Usalama Mahala pa Kazi (OSHA), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Kongani ya Viwanda Kibaha.

TCCIA ina zaidi ya wanachama 30,000 na katika mkutano wa jana, wawakilishi 350 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara walikuwapo.

Chanzo: Nipashe

My Take: Hongera sana Rais Samia,hakika wewe ni pro Business Leader,na bila shaka mambo yatakuwa Mazuri zaidi pindi Jopo la mapitip ya kero za Kodi na tozo ulilounda likitia ripoti yake.

Hakika yajayo yanafurahisha.
 
Ukiwa Mkandarasi unalipa service levy 5% kama Ushuru wa huduma.

Ila Kwa biashara ya Lodges nashangaa tunalipa Ushuru wa huduma 10% ya Mapato ghafi

Yaani hujalipa watu mishahara, Umeme,Maji, taka n.k

Lakini Halmashauri inataka 10% yao ya huduma.

Hii ni kero aisee 🙌
 
Ukiwa Mkandarasi unalipa service levy 5% kama Ushuru wa huduma.

Ila Kwa biashara ya Lodges nashangaa tunalipa Ushuru wa huduma 10% ya Mapato ghafi

Yaani hujalipa watu mishahara, Umeme,Maji, taka n.k

Lakini Halmashauri inataka 10% yao ya huduma.

Hii ni kero aisee 🙌
Toa maoni Yako kwenye Jopo alilounda Rais Ili wakitoa ripoti ije ku address hizo kero.

Samia ni pro Business so mkifeli kurekebisha awamu yake wanakuja wale wa upande ule hakuna rangi mtaacha kuiona.
 
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati bwana Dotto Biteko amesema Serikali inayoongozwa na Rais Samia Imefuta zaidi ya tozo na kero 370 Kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji Nchini.

Bwana Biteko amesema hatua hiyo imechochea kukua Kwa biashara na uwekezaji Nchini akitolea mfano ongezeko la mahitaji ya umeme ya zaidi ya megawatt 400 ndani ya mwaka mmja Kwa na kufanya mahitaji kuongeza kutoka megawatt 1400 Hadi 1900 Kwa sababu ya uhitaji mkubwa wa umeme kwenye sekta ya viwanda.

View: https://www.instagram.com/p/DDQ8wmPI98n/?igsh=ZnhhcGd2bWV6ZTh4

My Take
Hongera sana Rais Samia,hakika wewe ni pro Business Leader,na bila shaka mambo yatakuwa Mazuri zaidi pindi Jopo la mapitip ya kero za Kodi na tozo ulilounda likitia ripoti yake.

Hakika yajayo yanafurahisha.

Amezitaja?
 
Imefuta lini kabla ya bunge la bajeti kukaa??
 
Kati ya hizo tozo 370 ni ngapi ziliwekwa na serikali ya Samia?
 
Toa maoni Yako kwenye Jopo alilounda Rais Ili wakitoa ripoti ije ku address hizo kero.

Samia ni pro Business so mkifeli kurekebisha awamu yake wanakuja wale wa upande ule hakuna rangi mtaacha kuiona.
Nafikiri hiyo timu bado haijaanza kupita mitaani kukusanya maoni ya Wadau

Kama wangeweza wangetoa room ya kutoa maoni Kwa njia ya mtandao kama ilivyokuwa dira ya maendeleo ya Taifa.
 
Nafikiri hiyo timu bado haijaanza kupita mitaani kukusanya maoni ya Wadau

Kama wangeweza wangetoa room ya kutoa maoni Kwa njia ya mtandao kama ilivyokuwa dira ya maendeleo ya Taifa.
Imeshaanza kazi ,uwe unafuatilia matangazo Yao,wanazunguka Mikoani kukusanya maoni.
 
Kila mtu na kazi yake, wakati wengine tukiamka kupambania maisha aidha shambani, ofisi ama kwenye biashara, yeye Chawa wa Mama yupo nyuma ya keyboard kupalilia kibarua cha uchawa apate mkate wa siku.. huyu jamaa ni zaidi ya Mabhore Matinyi,ana akaunti nyingi hapa JF .
 
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati bwana Dotto Biteko amesema Serikali inayoongozwa na Rais Samia Imefuta zaidi ya tozo na kero 370 Kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji Nchini.

Bwana Biteko amesema hatua hiyo imechochea kukua Kwa biashara na uwekezaji Nchini akitolea mfano ongezeko la mahitaji ya umeme ya zaidi ya megawatt 400 ndani ya mwaka mmja Kwa na kufanya mahitaji kuongeza kutoka megawatt 1400 Hadi 1900 Kwa sababu ya uhitaji mkubwa wa umeme kwenye sekta ya viwanda.

View: https://www.instagram.com/p/DDQ8wmPI98n/?igsh=ZnhhcGd2bWV6ZTh4

My Take
Hongera sana Rais Samia,hakika wewe ni pro Business Leader,na bila shaka mambo yatakuwa Mazuri zaidi pindi Jopo la mapitip ya kero za Kodi na tozo ulilounda likitia ripoti yake.

Hakika yajayo yanafurahisha.

Hizo TOZO nani aliziweka? Walioumizwa na TOZO hizo wamefidiwa? Kufuta kitu ulichoweka wewe mwenyewe inahitaji kusifiwa kweli?
 
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati bwana Dotto Biteko amesema Serikali inayoongozwa na Rais Samia Imefuta zaidi ya tozo na kero 370 Kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji Nchini.

Bwana Biteko amesema hatua hiyo imechochea kukua Kwa biashara na uwekezaji Nchini akitolea mfano ongezeko la mahitaji ya umeme ya zaidi ya megawatt 400 ndani ya mwaka mmja Kwa na kufanya mahitaji kuongeza kutoka megawatt 1400 Hadi 1900 Kwa sababu ya uhitaji mkubwa wa umeme kwenye sekta ya viwanda.

View: https://www.instagram.com/p/DDQ8wmPI98n/?igsh=ZnhhcGd2bWV6ZTh4

My Take
Hongera sana Rais Samia,hakika wewe ni pro Business Leader,na bila shaka mambo yatakuwa Mazuri zaidi pindi Jopo la mapitip ya kero za Kodi na tozo ulilounda likitia ripoti yake.

Hakika yajayo yanafurahisha.

Huwa nafikili sana hivi ,Watu wa Mungu tz tupo mil 60 hivi mfano tukasema kila mtu alipe elfu kumi kwa Mwaka tena bila shuruti , ( kidogo kidogo) huu ni wastani elfu moja kwa kila kaya , hivi hatwezi ondokana na manyanyaso TRA hasa kwa wenzetu wafanyabiasha wa chini wanaonza kujitafuta?

Kwa nini tusiwe na mfumo ulio sawa kwa kila ngazi ya biashara , mfano bodaboda nchi nzima lipia elf 20 kwa mwaka na asisumbuliwe , hivyo hivyo kwa makundi mengine katika jamii zetu ,naona serikali itapata mapesa mengi tu.

Leo TRA imekua shida ,ubunifu zero, kazi kunyanya watu , mtu anaanzisha kiduka mtaji laki moja ,kesho wapo mlangoni , hii sio sawa.

Itungwe sheria pia ya kuwabana TRA pale wanapo yakoroga
 
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati bwana Dotto Biteko amesema Serikali inayoongozwa na Rais Samia Imefuta zaidi ya tozo na kero 370 Kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji Nchini.

Bwana Biteko amesema hatua hiyo imechochea kukua Kwa biashara na uwekezaji Nchini akitolea mfano ongezeko la mahitaji ya umeme ya zaidi ya megawatt 400 ndani ya mwaka mmja Kwa na kufanya mahitaji kuongeza kutoka megawatt 1400 Hadi 1900 Kwa sababu ya uhitaji mkubwa wa umeme kwenye sekta ya viwanda.

==

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko, alisema hayo jana Dar es Salaam alipokuwa akifungua Kongamano la Majadiliano ya Biashara na Uwekezaji Kati ya Serikali na Sekta Binafsi na Mkutano Mkuu wa 49 wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA).

Alisema kufutwa kwa tozo hizo kumepunguza Sh. bilioni 35 kwenye mapato ya serikali kwa mwaka na kwamba imefanya hivyo baada ya kusikiliza kero za wafanyabiashara.

Pia alisema serikali imepunguza muda wa kutoa huduma kutoka simu 14 hadi tatu na usajili wa hospitali binafsi, kutoka miezi 12 hadi siku tatu.

Alisema lengo la serikali kufanya hivyo ni kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, ili kuchochea ukuaji wa uchumi.

Dk. Biteko alisema serikali imefanya hivyo ili kuongeza mzunguko wa biashara ambao utaongeza mapato ya kodi, itakayotumika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na huduma za kijamii.

Alisema mbali na maboresho hayo, serikali imeimarisha bandari na miundombinu mingine, ikiwamo ujenzi wa barabara, meli, reli ya kisasa na ununuzi wa ndege ya mizigo.

Maboresho hayo, alisema yameongeza mahitaji ya umeme kutoka megawati 70.8 mwaka 2017/18, hadi megawati 420 mwaka huu.

“Mahitaji ya juu ya umeme Agosti mwaka jana yalikuwa megawati 1,410 lakini leo ni MW 1,888, ongezeko hili limekuja kwa sababu viwanda vingi vinajengwa na uchumi unachangamka,” alisema.

Dk. Biteko alisema serikali inatambua mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya nchi na kuwashauri wanachama wa TCCIA, kutumia malighafi za ndani katika kuzalisha bidhaa zenye ubora, zitakazoweza kushindana sokoni.

“Mchango wa sekta binafsi ni mkubwa na hauwezi kupuuzwa. Vijana zaidi ya milioni 12 wanaingia kwenye soko la ajira kila mwaka, asilimia 25 ndio wanapata ajira katika sekta rasmi. Asilimia 75 wanaingia katika sekta isiyo rasmi mkiwamo ninyi," alisema Dk. Biteko.

Rais wa TCCIA, Vicent Minja, alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuifungua nchi na kutatua changamoto za biashara.

Hata hivyo, aliomba mchakato wa kuandika sera ya sekta binafsi uharakishwe ili kuiweka kwenye mpangilio unaohitajika.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alisema dhamira ya serikali ni kuendelea kuifungua nchi na kuendeleza uhusiano mzuri na sekta binafsi ili kukuza uchumi wan chi.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa TCCIA, Oscar Kissanga, alitia saini mikataba minne ya ushirikiano na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Wakala wa Usalama Mahala pa Kazi (OSHA), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Kongani ya Viwanda Kibaha.

TCCIA ina zaidi ya wanachama 30,000 na katika mkutano wa jana, wawakilishi 350 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara walikuwapo.

Chanzo: Nipashe


My Take
Hongera sana Rais Samia,hakika wewe ni pro Business Leader,na bila shaka mambo yatakuwa Mazuri zaidi pindi Jopo la mapitip ya kero za Kodi na tozo ulilounda likitia ripoti yake.

Hakika yajayo yanafurahisha.

View: https://www.instagram.com/reel/DDP4OINPc0S/?igsh=OG9zbDU3YWR4enNp

Kazi nzuri 👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/DDURPH-KlF_/?igsh=MXExM2c0MWR5ZzNsZA==
 
Back
Top Bottom