Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Hivi hii mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya kuna shida gani?
Mbona kila siku maambukizi yako huku tu?
Akiwa anazungumza hivi karibuni ambaye ni Naibu Waziri-Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera Bunge na uratibu alisema:
"Bado kuna mikoa ina ushamiri mkubwa wa VVU kwa mfano Njombe, Iringa na Mbeya ina ushamiri mkubwa zaidi lakini mkoa wa Kigoma una ushamiri mdogo zaidi"
Pia amesema kiwango cha Maambukizi ya VVU kwa watu wenye umri kuanzia Miaka 15 - 45 kimepungua kidogo, kutoka asilimia 4.7 Mwaka 2017 hadi asilimia 4.4 Mwaka 2023.
====================================
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Ummy Deriananga amesema bado kuna mikoa yenye ushamiri mkubwa wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU), ametoa mfano Njombe una Asilimia 12.7, Iringa 11.1%, Mbeya 9.6%, upande wa Kigoma una maambukizi ya kiwango cha chini ambacho ni chini ya 1.7%.
Pia amesema kiwango cha Maambukizi ya VVU kwa Watu wenye umri kuanzia Miaka 15 - 45 kimepungua kidogo, kutoka 4.7% Mwaka 2017 hadi 4.4% Mwaka 2023.
Upande wa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania TACAIDS, Dkt. Catherine Joachim amesema Watu Milioni 1.7 wanaishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI Nchini na takribani Watu elfu 60 wanapata maambukizi hayo kila mwaka.
Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa TIMIZA MALENGO awamu ya tatu unaotekelezwa katika Halmashauri 36 katika mikoa 10 ya Tanzania Bara ambayo ni Dodoma, Geita, Lindi, Mara, Morogoro,Njombe, Ruvuma, Singida,Tabora na Tanga.
Hivi hii mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya kuna shida gani?
Mbona kila siku maambukizi yako huku tu?
Akiwa anazungumza hivi karibuni ambaye ni Naibu Waziri-Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera Bunge na uratibu alisema:
"Bado kuna mikoa ina ushamiri mkubwa wa VVU kwa mfano Njombe, Iringa na Mbeya ina ushamiri mkubwa zaidi lakini mkoa wa Kigoma una ushamiri mdogo zaidi"
Pia amesema kiwango cha Maambukizi ya VVU kwa watu wenye umri kuanzia Miaka 15 - 45 kimepungua kidogo, kutoka asilimia 4.7 Mwaka 2017 hadi asilimia 4.4 Mwaka 2023.
====================================
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Ummy Deriananga amesema bado kuna mikoa yenye ushamiri mkubwa wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU), ametoa mfano Njombe una Asilimia 12.7, Iringa 11.1%, Mbeya 9.6%, upande wa Kigoma una maambukizi ya kiwango cha chini ambacho ni chini ya 1.7%.
Pia amesema kiwango cha Maambukizi ya VVU kwa Watu wenye umri kuanzia Miaka 15 - 45 kimepungua kidogo, kutoka 4.7% Mwaka 2017 hadi 4.4% Mwaka 2023.
Upande wa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania TACAIDS, Dkt. Catherine Joachim amesema Watu Milioni 1.7 wanaishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI Nchini na takribani Watu elfu 60 wanapata maambukizi hayo kila mwaka.
Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa TIMIZA MALENGO awamu ya tatu unaotekelezwa katika Halmashauri 36 katika mikoa 10 ya Tanzania Bara ambayo ni Dodoma, Geita, Lindi, Mara, Morogoro,Njombe, Ruvuma, Singida,Tabora na Tanga.