Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Serikali imeweka mazingira rafiki kwa wanafunzi wenye watoto wachanga kupitia elimu nje ya mfumo rasmi, ili kuwawezesha kunyonyesha watoto wao kwa wakati wanapoendelea na masomo.
Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Najma Giga bungeni leo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omari Kipanga, amesema kuwa wanafunzi wanaorejea shule baada ya kujifungua hawaruhusiwi kwenda na watoto wao, bali wazazi wao wanapaswa kusaini makubaliano ya kuwalea watoto hao.
Katika swali lake la msingi, mbunge huyo alitaka kujua Serikali imejipangaje kuhakikisha watoto wachanga wa wasichana wanaoendelea na masomo wananyonya maziwa ya mama zao kwa wakati.
Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Najma Giga bungeni leo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omari Kipanga, amesema kuwa wanafunzi wanaorejea shule baada ya kujifungua hawaruhusiwi kwenda na watoto wao, bali wazazi wao wanapaswa kusaini makubaliano ya kuwalea watoto hao.
Katika swali lake la msingi, mbunge huyo alitaka kujua Serikali imejipangaje kuhakikisha watoto wachanga wa wasichana wanaoendelea na masomo wananyonya maziwa ya mama zao kwa wakati.