mabuba
Senior Member
- Dec 5, 2006
- 133
- 90
Waasisi wamesalitiwa
afrika nakulilia.
Afrika umekuwa mtumwa wa wb
afrika umekuwa kuhadi wa imf
afrika zobe la usa,
afrika umekuwa simango la watu wako
nakulilia afrika.
Afrika ndoto iwapi,
matumbo yetu yamepoteza ndoto afrika,
viongozi wetu wamekuwa wasaliti wetu,
wametutwisha zigo,
zigo la umasikini na ufukara zamivu,
nyerere, kwame amukeni,
azikiwe, ben bella njoo,
hubert maga na maurice yameogo sijawasahau,
njooni mchape wazandiki wafikra zenu
pia mwambieni mwami mwambusta asikose
ahamadou ahidjo huko mtafute david dacko,
mwambie francois tombalbaye ninalilia afrika,
fulbert youlou usichelewe, njoo na minyororo,
gamal abdel nasser sijakusahau, nyumbi kwako hapakaliki,
njooni muone fikra ufisadi zimetanda.
Haile selassie mfalme, jirani zao wauana,
leon m'ba nakwambia ninalia,
viongozi wetu wametusaliti hakuna umoja tena,
afrika imebaki jina, naumia.
Nakulilia afrika.
Sekou toure uko wapi, houphouet boigny anakutafuta,
william tubman ninaumia, njoo upesi,
king ldris nakupasha, gaddafi amesalitiwa,
philibert tsiranana, dj kachukua nchi wananchi wanacheza muziki,
modibo keita na kenyatta sisemi uongo,
mokhtar 0uld daddah nakulilia,
king hassan pale kwa jirani yako hapakariki,
hamani diori usimcheke, burundi sasa amani imerejea,
nakuambia wewe groire kayibanda,
leopold sedar senghor nazani umeumia,
mwambie milton margai akufute machozi,
abdella osman mwambie obote,
museveni sio yyle tena,
marshal farik lbrahim abboud hapa ninafikia,
msalimie habib bourguiba,pia sylvanus olympio.
Afrika huna jipya,
umekuwa mlalamikaji,
mwenye kujipendekeza,
ukiambatatana na fikra mfu,
huna mashiko tena.
Nawalilia waasisi,
walifikiri kwa akili,
walifanya kwa utashi mantiki,
waliona katika maono,
walibeba wafrika
viongozi leo wanafikri ki imf,
wanaona ki wb,
wanasikiliza ki usa,
wanaonja ki ulaya,
wanahisi kichina
uafrika leo ni,
ubeberu,
umangimeza,
unyonyaji,
ufisadi
upapa
unyangumi
naililia afrika nakupenda afrika
afrika nakulilia.
Afrika umekuwa mtumwa wa wb
afrika umekuwa kuhadi wa imf
afrika zobe la usa,
afrika umekuwa simango la watu wako
nakulilia afrika.
Afrika ndoto iwapi,
matumbo yetu yamepoteza ndoto afrika,
viongozi wetu wamekuwa wasaliti wetu,
wametutwisha zigo,
zigo la umasikini na ufukara zamivu,
nyerere, kwame amukeni,
azikiwe, ben bella njoo,
hubert maga na maurice yameogo sijawasahau,
njooni mchape wazandiki wafikra zenu
pia mwambieni mwami mwambusta asikose
ahamadou ahidjo huko mtafute david dacko,
mwambie francois tombalbaye ninalilia afrika,
fulbert youlou usichelewe, njoo na minyororo,
gamal abdel nasser sijakusahau, nyumbi kwako hapakaliki,
njooni muone fikra ufisadi zimetanda.
Haile selassie mfalme, jirani zao wauana,
leon m'ba nakwambia ninalia,
viongozi wetu wametusaliti hakuna umoja tena,
afrika imebaki jina, naumia.
Nakulilia afrika.
Sekou toure uko wapi, houphouet boigny anakutafuta,
william tubman ninaumia, njoo upesi,
king ldris nakupasha, gaddafi amesalitiwa,
philibert tsiranana, dj kachukua nchi wananchi wanacheza muziki,
modibo keita na kenyatta sisemi uongo,
mokhtar 0uld daddah nakulilia,
king hassan pale kwa jirani yako hapakariki,
hamani diori usimcheke, burundi sasa amani imerejea,
nakuambia wewe groire kayibanda,
leopold sedar senghor nazani umeumia,
mwambie milton margai akufute machozi,
abdella osman mwambie obote,
museveni sio yyle tena,
marshal farik lbrahim abboud hapa ninafikia,
msalimie habib bourguiba,pia sylvanus olympio.
Afrika huna jipya,
umekuwa mlalamikaji,
mwenye kujipendekeza,
ukiambatatana na fikra mfu,
huna mashiko tena.
Nawalilia waasisi,
walifikiri kwa akili,
walifanya kwa utashi mantiki,
waliona katika maono,
walibeba wafrika
viongozi leo wanafikri ki imf,
wanaona ki wb,
wanasikiliza ki usa,
wanaonja ki ulaya,
wanahisi kichina
uafrika leo ni,
ubeberu,
umangimeza,
unyonyaji,
ufisadi
upapa
unyangumi
naililia afrika nakupenda afrika