Nairobi: Kamishna Mkuu wa TRA atembelea Ubaloz wa Tanzania nchini Kenya

TRA Tanzania

Senior Member
Joined
Jul 16, 2022
Posts
128
Reaction score
370


Baada ya kikao cha Wakuu wa Mamlaka za Mapato za Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki #EARACGs, mjini Nairobi, Kamishna Mkuu TRA Bw. Yusuph Mwenda ametembelea ubalozi wa Tanzania nchini humo na kuwashukuru watumishi wa ubalozini kwa kazi ya uwezeshaji wa shughuli za kibiashara.


Kamishna Mkuu pia amekitembelea Himaya moja ya Forodha (Single Customs Territory- SCT) upande wa TRA na kuwataka Watumishi kufanya kazi ya kutathmini bidhaa (valuation) Kwa haraka, umakini na weledi ili kurahisisha biashara Kati ya Tanzania na Kenya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…