Naishi na mke ambaye sina mapenzi nae nifanyeje?

Hii thread ngumu aisee..
But mimi ningekuwa ndo wewe ninge'onja' sumu kwa kuilamba..
I mean ningeishi na mtu kwa kusikiliza HISIA zangu kuliko za wanakijiji..
Mfanye na yeye ajue kwamba hamuendani..sio wewe ndio ujue tu hakufai..kisha from there mtadiscuss the way forward..
 
Blind wife and a deaf husband.

usiwe blind ama deaf, mfundishe ili muendane, ajue unataka awe vipi, wewe hata ukimpata mwingine mwenye matatizo sio mwanamke ni wewe, mshape awe kama utakavyo. bucher kibao nyama ile ile wewe, acha upumbavu wako
 
Pole sana huwa inakuwa hivyo, kama vp tupa kule ila mwangalie sana mwanao.
 
The only disability in life is bad attitude..wewe ni disable; umeamua kumchkulia in a negative attitude, use ur common sense mambo yataenda. Nani amekwambia watu wote waliooana mapenz yao ni yale yale kama wakiwa wachumba? What i see from you, your expectations surpassed reality
 
alifel form two ndo ukatoa posa, then ukaenda chuo kikuu. sasa ni kwanini usimwendeleze ili awe kama wewe.
 
mkuu, umeshawahi kusoma kitabu cha 'song of Lawino song of Ocol'?
 
Naona unakua kama mshumaa unafurahisha watu kwa mwanga na huku wateketea,vp unaridhisha watu wakati roho yako haipendi? je unasababu yamsingi kama vile hatii sheria hakuhesimu anaigawa kwa wengine,hawaheshimu wazee wako anataka kila kitu kiende kwao au mlevi mchafu? au sababu unaupeo kidogo wakutafautisha vitu ndio mana unamuona mwenzio mshamba au hajui kuvaa vimini na mchuchumio ndio unamuona hafai?
Kumbuka hii ni dunia na wewe unamtoto pia unapomfanyia mtoto wa mwenzio na wewe wakwako yatamkuta.
 
yani sijui hata nikwambie nini.............pole weee
 

Niunganishe nae kwakua humpendi,ntakusaidia vitu vingi sana
 

Mh, ngoja nikapate mdudu kwanza akili yangu ikae sawa then ntakuja kukushauri, pole sana mkuu
 
Hii thread ni ngumu aise, anyway hakuna kitu kizuri duniani kama kuwa na furaha ya moyo na ni ngumu sana kishi na mtu usiyempenda, kweli ni ngumu, kwa sababu hujafunga nae ndo bado unaweza kufanya mchakato wa kuachana nae but ni vizuri ukimshirikisha, ongea nae na umueleweshe kwanini unataka kuchukua uamuzi huo wa kumuacha na kama kuna vitu tayari mmeshachuma pamoja ni vizuri ukamuachia na usiache kumunza mtoto wako hata kama atarudi kijijini (zingatia ushauri wa The Boss)
 
Mkuu mimi yalinikuta makubwa baada ya kuchukua uamuzi kama ulouchukua. Be careful
 

Ulikosea toka mwanzo hadi mwisho, na kadiri unavoishi naye ndivyo unavyozidi kukosea.
 
inatia huruma sana hasa kwa huyo dada maskini!!!! sasa kaka funguka zaidi katika hayo mapungufu yaliyokufanya umkinai mwana wa mwenzio, ili ushauriwe maana hapo hatutakiwi kuangalia upande mmoja tu (wako) bali tuwe fair tuangalie na kwa huyu dada...
 
This is what I wanted to tell this guy!! Hujaweka jitihada za makusudi za kumuweka katika level unayotaka. Usimfungie tu ndani tena mbali sijui kimara bonyokwa huku au bunju au kitunda! mtafutie kashule ka-computer aanze nako taratibu huku ukimtengenezea mazingira hata hapo nyumbani ya kujiendeleza zaidi kama kununua computer ya nyumbani. Maujanja yatamwingia tu na utafurahi zaidi. Ukimuacha, hayo matatizo utakayoyapata huko ni sawa tu na haya unayopata hakuna tofauti.
 
Hapana Mkuu, hebu ajaribu kumpa shule kidogo! afanye hata certificate in computer au Zile form four za miaka 2 then atakuwa anafanya mipango mingine ya kumweka katika hali ya kujitegemea.
 
Mkuu nafikiri tatizo lako umeanza kufanya compare and contrast.itakusumbua sana hiyo attitude uliyoitengeneza kichwani mwako baada ya kutoka chuo.ila waulize kwanza wenye wake walioenda shule na mkwanja na stutus yao iko juu wakuambie.inshort kuna watu wanatamani miaka irudi nyuma akajiolee kabint ka kijijini awe anakaa nyumbani na kumlelea wanae tu kutokana na maisha ya ndoa anayoishi. ninachoweza kukushauri ni kuwa jitahidi kumweka mwenzio hiyo level unayofikiri kwako ndio sahihi na ndio kigezo cha mwanamke unayemwazia kwa sasa.
 
Hapana Mkuu, hebu ajaribu kumpa shule kidogo! afanye hata certificate in computer au Zile form four za miaka 2 then atakuwa anafanya mipango mingine ya kumweka katika hali ya kujitegemea.

wa ukenyege unajua hawa vijana kabla ya kuoa huwa kunakuwa na expectation sasa wakizikosa wanaanza kulalamika.no perfect marriage in this world.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…