Najivunia katiba yangu ya mwaka 1977

article

Senior Member
Joined
Sep 10, 2016
Posts
186
Reaction score
344
Nawasilimu wote!

Wana Jf nimepitia mijadala ,Maoni na uzi mbalimbali zinazohusu Katiba ya URT ya mwaka 1977 humu ndani na nimeguswa kusema kitu.

Nafahamu Katiba husika ina mapungufu mbalimbali lakini mapungufu husika hayaendani na uzito yanayopewa kwa maoni yangu.

Katiba hii ni miongoni mwa katiba bora zaidi ulimwenguni ukizingatia mafanikio ambayo nchi yetu imeyapata chini ya mwongozo wake pia kwa jinsi ambavyo Katiba husika imeandikwa kimaono na kwa utaalamu mkubwa na wa kipekee.

Naomba nitoe mfano mdogo kwenye upande wa uandishi wa katiba husika kimaono.Katiba hii imeweka katazo la kumshitaki Rais kwa lolote utakalolitenda kama Rais wa URT katika kipindi chote cha uongozi wake.Kwa wale wanaotaka haki bila ya kuongozwa na busara na maono watataka sehemu husika ifutwe ili kuwepo nafasi ya kumshitaki Rais.Siku ikifika ya kuondoa sehemu hii nawashauri wahusika warejee kiini cha Machafuko yanayoendelea kwa sasa nchini Afrika ya Kusini baada ya mashtaka dhidi Rais wa zamani wa nchi hiyo kwa matendo aliyoyafanya akiwa Rais wa nchi hiyo.

Mafanikio ni mengi ambayo nchi na watu wake wamepata chini ya katika ya mwaka 1977 na kubwa zaidi ni udumishaji wa Amani,Utulivu ,upendo na mshikamano miongoni mwetu pamoja na ushirikiano na nchi nyingine ulimwenguni bila ya kuhatarisha uhuru wa nchi yetu tokea mwaka 1977. Mambo haya tokea mwaka 1977 yameenda sambamba na ongezeko la watu,ukuaji wa uchumi ,udumishaji wa tamaduni za kitanzania na utokomezaji wa ubaguzi wa aina zote ikiwemo ubaguzi wa rangi,kabila,dini,elimu na jinsia(na hapa nitoe mfano?)

Mapungufu yapo kwenye Katiba hii kama zilivyo katiba nyingine kwenye nchi mbalimbali ulimwenguni lakini hayafanani na mapungufu yaliyomo kwenye katiba hizo pia hayotoshi kusema kwamba katiba husika haifai na hivyo ibadirishwe.Mapungufu husika yanaweza kuondolewa kwa kufanyiwa marekebisho madogo pale inapobidi kwa maslai makubwa ya Taifa na si kwa kundi au kikundi cha Watu fulani kwa maslai yao binafsi.

Nahitimisha kwa kuwashurukuru na kuwapongeza wote wanaojivunia,wanaona na kuamini kwamba Katiba ya URT ya mwala 1977 siyo kikwazo cha Utamaduni, Demokrasia na Maendeleo ya Watanzania kwa sasa na siku za mbeleni.

Naomba kuwasilisha,

ARTICLE.
 
Kwahiyo mtu akiwa rais anakuwa Mungu?
 
Ikiwa alipata Urais sawa na Katiba husika si Mungu bali kwa Waaminio ni Mwakilishi wa Mungu na maandiko matakatifu hayahojiwi wala hayaruhusiwi kubadarishwa hata herufi rejea vitabu vitakatifu unavyovifahamu.
 
Ikiwa alipata Urais sawa na Katiba husika si Mungu bali kwa Waaminio ni Mwakilishi wa Mungu na maandiko matakatifu hayahojiwi wala hayaruhusiwi kubadarishwa hata herufi rejea vitabu vitakatifu unavyovifahamu.
Nukuu hilo fungu hapa.
 
Ikiwa alipata Urais sawa na Katiba husika si Mungu bali kwa Waaminio ni Mwakilishi wa Mungu na maandiko matakatifu hayahojiwi wala hayaruhusiwi kubadarishwa hata herufi rejea vitabu vitakatifu unavyovifahamu.
Unadhani nchi hii wote ni Wakristo? Niletee nukuu ya fungu katika Buddhism.
 
Unadhani nchi hii wote ni Wakristo? Niletee nukuu ya fungu katika Buddhism.
Bila bila ndugu yangu nadhani utakuwa umetoka bila bila kwani ukisoma between the lines kwenye uzi wangu hakuna mstari ambao umegusa dhehebu lolote la dini! niliandika rejea vitabu vitakatifu unavyovifahamu kwani vyote vimegusia masuala ya utawala wa juu kwenye mipaka ya nchi.
 
rasim ya katiba mpya haina mapungufu ya kuifanya isipitishwe but ina marekebisho.ambayo hata juzi warioba jay alitusomea kifungu mojawapo kwa ufupi mkuu.sasa wewe kazana ya miaka kenda
 
rasim ya katiba mpya haina mapungufu ya kuifanya isipitishwe but ina marekebisho.ambayo hata juzi warioba jay alitusomea kifungu mojawapo kwa ufupi mkuu.sasa wewe kazana ya miaka kenda
Bablemuba!Hakuna andiko linaloandikwa na mwanadamu ambalo halina mapungufu.Rasimu ya Katiba mpya unayoizungumzia pia ina Mapungufu makubwa, hata hivyo sitayazungumzia mapungufu husika kwa kuwa hayahusiani na uzi huu.Katiba ni sheria Mama hivyo haiwezi kujumuisha kila kitu.Mapungufu ya kikatiba siyo busara na weledi yakarekebishwa kwa kuibadirisha Katiba husika bali ni busara na weledi kuifanyia marekebisho Katiba husika pale inapoonekana ina mapungufu kwa kufanya marekebisho kwenye sehemu yenye mapungufu kwenye katiba husika, kutunga sheria,Kanuni,miongozo ,Waraka au viongozi wa ngazi za juu kwenye utawala husika kutoa maelekezo kwa surbordinates wao.
 
mkuu.upo sahihi na sina maana kwamba rasimu ndio itakayo pitishwa ila bunge lake ndilo lenye namna ya kufanya ili tuipate.pia hata kabla haijapitishwa tutailetewa tena kaka ili isije ikatugeukia na tukaanza kupungua magego.ila ulazima wake upo mkuu.sikupingi sana mana kila mtu ana mtazamo wake juu ya hili taifa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…