Pole mpenzi wangu milcah.
Ila naomba nikueleze ukweli,hata kama utauma au hutaupenda.
NDIO UMEFANYA KOSA KUMUELEZA MWANAUME HISIA ZAKO,kwa lugha nyingine ni kwamba umemtongoza mwanaume.
Mwanaume ni kama simba,akitaka nyama nzuri inayomvutia ni lazima atoke jasho kuiwinda,muindaji anapopata kitoweo chake kwa shida hukidhamini na kukiona kitamu sana na ndio maana mwanamke unapowindwa hata kama unajua utakubali lazima uringe kidogo,uweke vipozi vya hapa na pale.
Kitoweo kinachopatikana bila kuwindwa huo ni mzoga na simba hali mizoga anamuachia fisi mla mizoga,simba anataka ahangaike na chake chenye uhai akiue mwenyewe na anywe damu fresh.
Wanaume wengi wakitongozwa na mwanamke wanamuona mwanamke huyo ni kimeo,malaya,anajirahisisha na kama ni wale wenye heshima zake anakukataa tena anakuogopa kama ni wale mafisi wasiojali mizoga anakukubali akishakufunua anakuacha na anakusema kwa wenzie.
Sijasema umefanya dhambi au vibaya bali nimesema umefanya kosa.
Wanawake hatutongozi bali tunasubiri tutongozwe.
Siku nyingine ukimpenda mwanaume,usifungue kinywa chako kumtongoza bali kama unaweze mtege yeye ndo aanze kukutongoza halafu ujifanye hata hukuwa na mpango naye ili upate nafasi ya kumringia kidogo,kijasho kkimtoka kidogo ndo unamkubali huku ukimwacha akiamin kuwa umemsumbua kweli kumbe ulimtega.