Nakata kujenga ghorofa kufika 2026

Njugu mawe

Member
Joined
Sep 8, 2023
Posts
33
Reaction score
33
Nikiwa naendelea na makusanyo ya pesa yangu, ya kufikia ndoto ya ujenzi wa ghorof, nimepata ramani hii na kiwanja changu ni Mita 16 kwa 14.

Je wakuu hii Ramani hapa inakaa kwa ukubwa wa kiwanja hicho?

Pia wataalamu wa ujenzi naomba kufahamu kusimamisha jengo hilo bila madirisha, milango wala decoration yoyote itanigharamu kiasi gani ukiondoa hela ya fundi, maana mafundi nitawapata kwa gharama binafsi,

Malengo yangu jengo lisimame kwanza.
Ushauri wenu tafadhari

Picha
 
Kwanza, hakikisha unapata michoro yoye kwa umoja wake, hapa namaanisha michoro ya msanifu majengo (Architectural drawings) hiyo ambayo tayari unayo, structural drawings na service drawings.

Pili, ipeleke michoro hiyo kwa mkadiriaji majengo (quantity surveyor) ili upate mahitaji ya jumla ya jengo lako. Na hapo ndio utajua unatakiwa kujiandaa kwa ukubwa gani.

Tatu na mwisho, weka mkakati wa kukusanya pesa kulingana na makadirio au zaidi ya makadirio yaliyo tolewa na quantity surveyor, kwasababu vitu hupanda bei.

Naamini maelezo haya yatasaidia kwa namna moja au nyingine.

0621003092
Ni namba kwaajili ya kupata ushauri wa bure kuhusu ujenzi.


Cheers 🥂
 

Attachments

  • 48FE9267-99B4-4430-B223-748C3F95B910.jpeg
    337.5 KB · Views: 20
Nataka ramani ambayo ghorofani ni chumba kimoja tu, na sebure kubwa ya mimi na mke wangu
 
Reactions: BRN
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…