Nakatishwa tamaa kwenda Pemba

Nakatishwa tamaa kwenda Pemba

Ricky Blair

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
463
Reaction score
1,009
Kila mtu ananikatisha tamaa kwenda kutembea Pemba kwamba pabaya, waislamu extremists sana, kufika huko ngumu sababu maboti makubwa kama ya Azam na mengine yanayokuja Unguja hayendi na pia upepo mkubwa sana na mawimbi kufika huko.

Aliyewahi kwenda au mwenyeji mnasemaje?
 
Hakuna speed bot zipo meli kubwa ambaz zinamilikiwa na Azam na campany nyengine.

Bahari upepo ni wakawaida tu watu wanasafiri kila leo.
 
Pemba ni mahali pazuri sana kutembelea na hata kuishi, watu wake hawana makuu, maisha ni rahisi, kuna mandhari nzuri sana, hali ya hewa ni nzuri, sehemu kubwa ya kisiwa ina rutuba na unaweza kulima chochote. Gharama za vyakula ni nafuu na vyakula vingi ni vya asili.

Bahari na fukwe zake hazijachafuliwa, hakuna msongamano wa watu wala magari. Masuala ya imani ni ya mtu binafsi, ni dhahiri kwamba idadi ya waislamu ni kubwa lakini kila mtu na maisha yake. Kuna wengi wasio waislamu na wanaendesha maisha yao bila usumbufu wowote.

Changamoto ya Pemba ni usafiri wake, usafiri wa uhakika ni ndege lakini bei zake zimechangamka, hivyo wengi hutumia usafiri nafuu wa meli kutokea Dar, Unguja au Tanga.

Nilikuwa huko mwishoni mwa mwaka jana na natamani sana nirudi tena.
 
Kila mtu ananikatisha tamaa kwenda kutembea Pemba kwamba pabaya, waislamu extremists sana, kufika huko ngumu sababu maboti makubwa kama ya Azam na mengine yanayokuja Unguja hayendi na pia upepo mkubwa sana na mawimbi kufika huko.

Aliyewahi kwenda au mwenyeji mnasemaje?
Pitia njia ya Tanga ni jirani sana na Pemba
 
"Siku nitafika pemba bint sultan khalfani.. nitembeze sehemu zote hadi mwisho..

Kuishi visiwani Mama kuna utamu wake"

Hii nyimbo naicheza hapa.....
 
"Wallahi sitabaki naenda pemba ndege naruka...

Nipae angani nikatishe bahari.. juu kwa juu nione, alafu nitue Pemba, Marashi nipokee Pemba ooh Pemba...

Naskia ni kuzuri, jioni kuna Upepo eti unanukia Marashi ya karafuuu..."
 
Kila mtu ananikatisha tamaa kwenda kutembea Pemba kwamba pabaya, waislamu extremists sana, kufika huko ngumu sababu maboti makubwa kama ya Azam na mengine yanayokuja Unguja hayendi na pia upepo mkubwa sana na mawimbi kufika huko.

Aliyewahi kwenda au mwenyeji mnasemaje?
Kuna vitu Hujaspecify mkuu kwa sababu Usafiri wa Pemba unategemea vitu kadhaa
  • Unaenda Pemba ukitokea wapi?
  • Je,Unaenda kwa nia nzuri au unaenda kutembea? Ushauri usijefanye Rijali au kidume pemba kuchukua wake au watoto wa watu utakiona cha mtema kuni,
  • Mkondo wa bahari au upepo inategmea pia unatokea wapi
Anyaei mkuu mimi ningekushauri chukua chopper tu ni nafuu na Inapunguza hofu yako
 
Kuna vitu Hujaspecify mkuu kwa sababu Usafiri wa Pemba unategemea vitu kadhaa
  • Unaenda Pemba ukitokea wapi?
  • Je,Unaenda kwa nia nzuri au unaenda kutembea? Ushauri usijefanye Rijali au kidume pemba kuchukua wake au watoto wa watu utakiona cha mtema kuni,
  • Mkondo wa bahari au upepo inategmea pia unatokea wapi
Anyaei mkuu mimi ningekushauri chukua chopper tu ni nafuu na Inapunguza hofu yako
Nilikuwa nataka kutokea Tanga ila naona muda umeniishia so itabidi nitokee from Unguja next time; hapo je? Nipe scenarios zote za from Tanga au from Unguja
 
Nilikuwa nataka kutokea Tanga ila naona muda umeniishia so itabidi nitokee from Unguja next time; hapo je? Nipe scenarios zote za from Tanga au from Unguja
From Tanga Mzee Unatumia njia ya Tanga Beach au kule sahare kuna Bandari za waswahili,Au unaenda kwa bandari ya kawaida..
bandari za waswahili ni 10k mpaka pemba!
Ila bandari halali ni 35k mpaka pemba
 
Kila mtu ananikatisha tamaa kwenda kutembea Pemba kwamba pabaya, waislamu extremists sana, kufika huko ngumu sababu maboti makubwa kama ya Azam na mengine yanayokuja Unguja hayendi na pia upepo mkubwa sana na mawimbi kufika huko.

Aliyewahi kwenda au mwenyeji mnasemaje?
Pemba si sehemu ya maana kutembelea au kwenda kuanza maisha......unafiki mwingi mno na ubaguzi wa nje nje kwa watu wa bara. Sikushauri uende huko hakufai hata kidogo ila kama wewe una asili ya ugaidi na mnafiki basi kutakufaa,
 
Back
Top Bottom