Nakukumbusha Waziri Ndalichako kwamba Cheo ni dhamana ya muda mfupi sana. Utaondoka na kukiacha kama wengine walivyokiacha

Nakukumbusha Waziri Ndalichako kwamba Cheo ni dhamana ya muda mfupi sana. Utaondoka na kukiacha kama wengine walivyokiacha

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
SERIKALI YAUTAKA UONGOZI WA UDSM KUWACHUKULIA HATUA VIONGOZI WA WANAFUNZI - Wazi ( 612 X 640 ).jpg


Kuna wakati ulipokuwa NECTA ulilalamikiwa kwamba hutumii weledi huku baadhi ya wadau wakitaka ung'olewe , tulikutetea sana kuliko maelezo , Kwa taarifa yako sisi ndio tulikupendekeza uteuliwe Waziri wa Elimu ili ukaweze kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya elimu nchini Tanzania ikiwemo changamoto ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu , angalia nyuzi zetu humu kabla ya uteuzi wako .

Lakini sasa mimi binafsi naanza kujuta kwa kushiriki kukupigia debe kutokana na matendo yako baada ya kulewa madaraka , madai halali ya wanafunzi umeamua kuyageuza kuwa ni makosa makubwa ya kufukuza watoto wa watu chuoni badala ya kutumia weledi , umeamua kutumia bunduki kuua mbu !

Utavuna unachopanda .
 
Mbunge mtalajiwa wa Jimbo huko kigoma


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ukiacha Mbowe kuna kiongozi yoyote hapa nchini ambaye alikaa au anaamini atakaa na cheo alichonacho maisha yake yote?
 
Back
Top Bottom