Mimi ni yule kijana uliyenipita na gari lako katika njia ya kwenda mbweni kunakijengwa kambi ya jeshi. Ulinipita kama mita hamsini hivi ukasimamisha gari ukatoa kichwa nje ukaniita, nikaitika, ukaniuliza kama naenda nikakujibu ndio...
Nikaja nikapanda ndani ya gari lako ukiwa wewe pekeyako, tukaongea kidogo huku tukiburudishwa na wimbo wa Nandy unaitwa one day sijui ule.....nikafika nilipotaka kwenda nikashuka....sasa nipo hapa nakusubiri upite tena (kama utarudi)...sina lengo lolote zaidi ya kukusubiri turudi wote...namba ya gari lako nimeikariri....nakusubiri hapa....