Ndugu zangu, kama mnavyofahamu mimi ni mfuatiliaji mwenye uchungu na mpira wetu wa Bongo na nilionyesha kutoridhishwa kwa kiwango kikubwa na hali ya utawala usio bora kutoka TFF ya Jamal Malinzi. Mimi ni muumini wa dhana ya utawala bora na kwa kiwango kikubwa eneo hili ndilo lililomwangusha Jamal Malinzi na wenzake, hata tulipopiga kelele kuponda uongozi wake wapo wengi hawakuelewa tunamaanisha nini.
Hata hivyo, ni bahati mbaya utawala wa Malinzi ulimuhusisha Wallace Karia kama Makamu wa Rais kwa hiyo doa hili la utawala usiozingatia maadili ya kiuongozi hawezi kulikwepa pia.
Lakini baada ya kuchunguza na kuwachambua wagombea nafasi ya Urais wa TFF na kulinganisha na hali halisi ya mahitaji ya mpira wetu, nimefikia uamuzi wa kumtakia kila la heri Wallace Karia ambaye sasa hivi ndiye anayekaimu Urais wa TFF. Na kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia, anapewa nafasi kubwa ya kuibuka kwa kishindo katika uchuguzi huu wa leo.
Zipo sababu kadhaa, na nitataja nne zinazompa turufu Wallace Karia kuibuka kidedea kwa sababu mpira wetu unamhitaji.
1. Wallace Karia ni TFF presidential material! Ana haiba ya uongozi kwa ngazi ya juu. Anazungumza kama kiongozi, ana act kama kiongozi, anajitambua kama kiongozi kwa ufupi ana hadhi ya kuongoza taasisi katika ngazi ya juu. Uzoefu wake kama kiongozi wa kiserikali kwa nafasi za ukurugenzi, na hata timu za mpira hasa Coastal Union, kuna mpa turufu ya dhidi ya wagombea wengine hususani Ali Mayai anayeonekana kuwa kipenzi cha wadau wengi.
2. Karia hajijiambatanisha sana na mapenzi ya timu zetu mbili kubwa na kongwe Simba na Yanga na anavyo anaonekana kuwa mtu anayeweza kuaminika na pande zote. Kusema ukweli hadi muda huu naandika haya sijui yuko mrengo gani japo hili sio muhimu sana. Kuwa shabiki na hata mnazi wa kupindukia wa timu hizi sio dhambi na wala haipaswi kuwa turufu ya mtu kuwa au kutokuwa kiongozi. Tatizo linakuja kwenye IMANI. Je unaweza kuaminika na pande zote kuwa utakuwa fair? Je rekodi zako za uongozi zimeacha alama gani huko nyuma? Nafasi ya kipekee kwa Karia ni ile hali ya kutokuwa maarufu miongoni mwa wapenzi wa Simba na Yanga - kunaweza kumpa nafasi nzuri zaidi ya kutekeleza majukumu yake bila pressure kutoka kwa timu hizi na wafuasi wao.
3. Hana kashfa ya utovu wa uadilifu. Huyu tayari amekuwa kiongozi na hata sasa ni kiongozi wa TFF inayomaliza muda wake na ambayo imelalamikiwa sana kwa vitendo vya rushwa, upendeleo, ukabila, upangaji matokeo na mambo yanayofanana na hayo lakini jamaa katoka akiwa 'Mr. Clean'! Unajua mtu anaweza kuwa mwadilifu au kujifanya mwadilifu pale anapokuwa hana madaraka au nafasi ya kupiga! Huyu ameshakuwa kiongozi lakini bado ametunza heshima yake. N ndio maana pamoja na kuwa alikuwa pamoja na akina Malinzi, ameprove kuwa hakuwa chanzo cha 'ujinga' wote uliokuwa uanfanyika. Inaonekana hakuwa 'insider' japo alikuwa na cheo cha juu. TFF inamhitaji mtu wa aina hii.
4. Sera zake zinaonyesha ni mtu anayejua tunahitaji nini. Wengi wanakariri vitu vilevile kama kutafuta udhamini, maendeleo ya soka la vijana na timu bora ya taifa. Haya ni matamko tu hata akina Malinzi walikuwa na matamko mazuri zaidi kuliko haya ya sasa lakni wamekwama kwa sababu hawakuonyesha watafanyaje. Pia hawakupima risk ya utekelezaji. Sasa sikiliza Karia anavyosema: UWAZI, UADILIFU NA UWAJIBIKAJI. karia amesema atafanya vitu vidogovidogo vinavyotekelezeka!!!! Katika dhana ya uongozi na operesheni tunaita continuous improvement.
Amesema ataanza na kujenga nidhamu ya muundo wa kitaasisi utakaotoa nafasi ya ushirikishwaji usio wa hila kwa kamati ya utendaji. Kwa lugha rahisi amesema TFF kama taasisi imekwama kwa sababu haikujenga nidhamu ya kitaasisi, ndio maana tuliona kamati zikilumbana, maamuzi yakitenguliwa, kushikana uchawi, chauguzi kuendeshwa kimizengwe, n.k.
Ni hadi ujenge taasisi imara ndipo unaweza kuvutia kuaminika na udhamini bomba amabo utakuwa nafasi ya kutekeleza programmu nyingine za kiufundi na kimaendeleo.
MUHIMU: Kwako Karia baada ya kuapishwa tafadhali sana mkaribishe Ally Mayai Tembele, umtumie kwa kadiri ya uwezo wake maana huyu ni mmoja kati ya wagombea makini lakini anahitaji kuthibitishwa katika uzoefu
Hata hivyo, ni bahati mbaya utawala wa Malinzi ulimuhusisha Wallace Karia kama Makamu wa Rais kwa hiyo doa hili la utawala usiozingatia maadili ya kiuongozi hawezi kulikwepa pia.
Lakini baada ya kuchunguza na kuwachambua wagombea nafasi ya Urais wa TFF na kulinganisha na hali halisi ya mahitaji ya mpira wetu, nimefikia uamuzi wa kumtakia kila la heri Wallace Karia ambaye sasa hivi ndiye anayekaimu Urais wa TFF. Na kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia, anapewa nafasi kubwa ya kuibuka kwa kishindo katika uchuguzi huu wa leo.
Zipo sababu kadhaa, na nitataja nne zinazompa turufu Wallace Karia kuibuka kidedea kwa sababu mpira wetu unamhitaji.
1. Wallace Karia ni TFF presidential material! Ana haiba ya uongozi kwa ngazi ya juu. Anazungumza kama kiongozi, ana act kama kiongozi, anajitambua kama kiongozi kwa ufupi ana hadhi ya kuongoza taasisi katika ngazi ya juu. Uzoefu wake kama kiongozi wa kiserikali kwa nafasi za ukurugenzi, na hata timu za mpira hasa Coastal Union, kuna mpa turufu ya dhidi ya wagombea wengine hususani Ali Mayai anayeonekana kuwa kipenzi cha wadau wengi.
2. Karia hajijiambatanisha sana na mapenzi ya timu zetu mbili kubwa na kongwe Simba na Yanga na anavyo anaonekana kuwa mtu anayeweza kuaminika na pande zote. Kusema ukweli hadi muda huu naandika haya sijui yuko mrengo gani japo hili sio muhimu sana. Kuwa shabiki na hata mnazi wa kupindukia wa timu hizi sio dhambi na wala haipaswi kuwa turufu ya mtu kuwa au kutokuwa kiongozi. Tatizo linakuja kwenye IMANI. Je unaweza kuaminika na pande zote kuwa utakuwa fair? Je rekodi zako za uongozi zimeacha alama gani huko nyuma? Nafasi ya kipekee kwa Karia ni ile hali ya kutokuwa maarufu miongoni mwa wapenzi wa Simba na Yanga - kunaweza kumpa nafasi nzuri zaidi ya kutekeleza majukumu yake bila pressure kutoka kwa timu hizi na wafuasi wao.
3. Hana kashfa ya utovu wa uadilifu. Huyu tayari amekuwa kiongozi na hata sasa ni kiongozi wa TFF inayomaliza muda wake na ambayo imelalamikiwa sana kwa vitendo vya rushwa, upendeleo, ukabila, upangaji matokeo na mambo yanayofanana na hayo lakini jamaa katoka akiwa 'Mr. Clean'! Unajua mtu anaweza kuwa mwadilifu au kujifanya mwadilifu pale anapokuwa hana madaraka au nafasi ya kupiga! Huyu ameshakuwa kiongozi lakini bado ametunza heshima yake. N ndio maana pamoja na kuwa alikuwa pamoja na akina Malinzi, ameprove kuwa hakuwa chanzo cha 'ujinga' wote uliokuwa uanfanyika. Inaonekana hakuwa 'insider' japo alikuwa na cheo cha juu. TFF inamhitaji mtu wa aina hii.
4. Sera zake zinaonyesha ni mtu anayejua tunahitaji nini. Wengi wanakariri vitu vilevile kama kutafuta udhamini, maendeleo ya soka la vijana na timu bora ya taifa. Haya ni matamko tu hata akina Malinzi walikuwa na matamko mazuri zaidi kuliko haya ya sasa lakni wamekwama kwa sababu hawakuonyesha watafanyaje. Pia hawakupima risk ya utekelezaji. Sasa sikiliza Karia anavyosema: UWAZI, UADILIFU NA UWAJIBIKAJI. karia amesema atafanya vitu vidogovidogo vinavyotekelezeka!!!! Katika dhana ya uongozi na operesheni tunaita continuous improvement.
Amesema ataanza na kujenga nidhamu ya muundo wa kitaasisi utakaotoa nafasi ya ushirikishwaji usio wa hila kwa kamati ya utendaji. Kwa lugha rahisi amesema TFF kama taasisi imekwama kwa sababu haikujenga nidhamu ya kitaasisi, ndio maana tuliona kamati zikilumbana, maamuzi yakitenguliwa, kushikana uchawi, chauguzi kuendeshwa kimizengwe, n.k.
Ni hadi ujenge taasisi imara ndipo unaweza kuvutia kuaminika na udhamini bomba amabo utakuwa nafasi ya kutekeleza programmu nyingine za kiufundi na kimaendeleo.
MUHIMU: Kwako Karia baada ya kuapishwa tafadhali sana mkaribishe Ally Mayai Tembele, umtumie kwa kadiri ya uwezo wake maana huyu ni mmoja kati ya wagombea makini lakini anahitaji kuthibitishwa katika uzoefu