Nalipiwa frem mwaka mmoja...nna mtaji milion tatu...ushauri..niweke biashara gani?

Nalipiwa frem mwaka mmoja...nna mtaji milion tatu...ushauri..niweke biashara gani?

sia1

Member
Joined
Mar 14, 2014
Posts
28
Reaction score
27
Asalaam wapendwa...niko dar maeneo ya kijitonyama..nna mtaji wa sh milion tatu...na kuna frem nalipiwa mwaka mzima sasa sijui nifungue biasha gani ambayo kila wiki nina uwezo wa kuongeza laki mbili...kwa muda wa mwaka mmoja...naomba ushauri...frm iko maeneo ya makazi ya watu...
 
  • Thanks
Reactions: BIR
Naomba ushauri...nna mtaji wa milion tatu...frem ya bure...na nna uwezo wa kuongexa laki mbili kila wiki...sasa naomba ushauri nifungue biasha gani...frem iko karibu na makazi ya watu
 
Asalaam wapendwa...niko dar maeneo ya kijitonyama..nna mtaji wa sh milion tatu...na kuna frem nalipiwa mwaka mzima sasa sijui nifungue biasha gani ambayo kila wiki nina uwezo wa kuongeza laki mbili...kwa muda wa mwaka mmoja...naomba ushauri...frm iko maeneo ya makazi ya watu...


Faida kubwa hivo huwez pata kwa wiki
Ukilinganisha na mtaji wako.

Fungua Duka la bidhaa na usimamie mwenyewe
 
No sio faida...ni laki mbili nitakuwa naongeza kwenye biashara...kila wiki naongeza laki mbili
 
Do your homework mkuu. Moja ya hatua za mwanzo katika kufungua biashara ni kuyasoma mazingira ya sehemu goli lako lilipo au linapotarajiwa kuwepo. Ni kitu gani kinakosekana huo mtaa/eneo? Usiende mahali kufungua saluni ya kiume wakati hapo mtaani tayari kuna saluni nne za kiume za nguvu; kuwa mbunifu na ufungue business ambayo kila mtu hapo mtaani atakuwa hana sehemu nyingine ya kwenda zaidi ya kwako. Pili,fanya utafiti kuhusu bidhaa upatikanaji wa bidhaa ambayo utakuwa unaiuza pamoja na bei ya wastani ya bidhaa hiyo kwa ujumla. Kwa mfano unataka kufungua bucha ufanye utafiti kujua ni wapi utakuwa unanunua nyama kwa ujumla, au kama ni kuletewa na meat vans na gharama yake. Pia lazima ujiulize na utafiti kuwa washindani wako watakuwa ni kina nani? na uwachunguze washindani wako na ujue mapungufu yao kisha uwe na kitu cha ziada kuwazidi wao.
Pia ni lazima ujue tabia za hao watu ambapo goli lako lipo ni kitu gani hawapendi, tabia zao katika manunuzi ya bidhaa unayotaka kuiuza, n.k.
Kwa ufupi mkuu sisi hatuwezi kukushauri ni biashara gani uanzishe kwa sababu hatujui taarifa zote hizo hapo juu na mengine mengi ambayo sijayataja(hobby yako,uvumilivu wako,n.k), lakini wewe taarifa hizo unazo na kwa ambazo huna ni kazi na wajibu wako kuzitafuta kabla ya kuanzisha hio biashara. All the best mkuu
 
Back
Top Bottom