Namanga: Mawakala wa forodha pamoja na Wasafirishaji Wagoma

Namanga: Mawakala wa forodha pamoja na Wasafirishaji Wagoma

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Taarifa zaidi hii hapa

Mawakala wa Forodha pamoja na Wasafirishaji wenye magari zaidi ya 500 wa Tanzania wamefanya mgomo ikiwa ni siku ya pili katika mpaka wa Namanga uliopo katika Wilaya ya Longido Mkoani Arusha wakishinikiza kupunguzwa kwa utitiri wa kodi pamoja kutokea kwa sintofahamu kwenye mashine za EFD kwa Wafanyabiashara wanaosafirisha bidhaa kwenda nje ya Nchi.

Makamu Mwenyekiti wa Forodha katika mpaka wa Namanga, Alois Makyao amesema wamesitisha usafirishaji na kuomba mfumo kuwekwa sawa ikiwemo ucheleweshaji wa ukaguzi na kusema sasa magari zaidi ya 500 yameshindwa kwenda Kenya baada ya mgomo huo na kuiomba Serikali kuingilia jambo hilo kwa kuwa Serikali pamoja na Wafanyabiashara hao wanapoteza mapato kwa wap kuendelea kukaa hapo mpakani.

@AyoTV_ imemtafuta Meneja wa Forodha wa TRA katika mpaka wa Namanga Edwin Changwe ambapo amesema kuwa yeye hawezi kulizungumzia suala hilo kwa kuwa hayupo ofisini na kuhusu mgomo huo unaondelea hana taarifa zake, bado Ayo TV inaendelea kuzitafuta Mamlaka nyingine za Serikali ili kupata kauli yao.

Pia soma
- Taarifa kwa Umma kuhusu mgomo wa wasafirishaji Namanga
Screenshot_2024-07-25-20-54-32-1.png
Screenshot_2024-07-25-20-54-40-1.png

Screenshot_2024-07-25-20-54-49-1.png
 
Yaani watu wana mbinu nyingi za kujua kama dogo yuko kwa Madiba anajitibu hiyo issue akiyokuwa kaibeba akamuwekee mtu, bahati mbaya akaigusa mkononi na akashika mdomoni.

Haya, hatakuja kusuluhisha mpaka apone, Mungu akijaalia
 
Yaani watu wana mbinu nyingi za kujua kama dogo yuko kwa Madiba anajitibu hiyo issue akiyokuwa kaibeba akamuwekee mtu, bahati mbaya akaigusa mkononi na akashika mdomoni.

Haya, hatakuja kusuluhisha mpaka apone, Mungu akijaalia
Kila mtu anasema lake.......
 
Taarifa zaidi hii hapa

Mawakala wa Forodha pamoja na Wasafirishaji wenye magari zaidi ya 500 wa Tanzania wamefanya mgomo ikiwa ni siku ya pili katika mpaka wa Namanga uliopo katika Wilaya ya Longido Mkoani Arusha wakishinikiza kupunguzwa kwa utitiri wa kodi pamoja kutokea kwa sintofahamu kwenye mashine za EFD kwa Wafanyabiashara wanaosafirisha bidhaa kwenda nje ya Nchi.

Makamu Mwenyekiti wa Forodha katika mpaka wa Namanga, Alois Makyao amesema wamesitisha usafirishaji na kuomba mfumo kuwekwa sawa ikiwemo ucheleweshaji wa ukaguzi na kusema sasa magari zaidi ya 500 yameshindwa kwenda Kenya baada ya mgomo huo na kuiomba Serikali kuingilia jambo hilo kwa kuwa Serikali pamoja na Wafanyabiashara hao wanapoteza mapato kwa wap kuendelea kukaa hapo mpakani.

@AyoTV_ imemtafuta Meneja wa Forodha wa TRA katika mpaka wa Namanga Edwin Changwe ambapo amesema kuwa yeye hawezi kulizungumzia suala hilo kwa kuwa hayupo ofisini na kuhusu mgomo huo unaondelea hana taarifa zake, bado Ayo TV inaendelea kuzitafuta Mamlaka nyingine za Serikali ili kupata kauli yao.
View attachment 3051941View attachment 3051942
View attachment 3051943
Naona hili jambo tra walimalizana nao jana nimekutana na taarifa hii kwa umma naomba kushare
NAMANGA.jpeg
 
Back
Top Bottom