Namba 1 amejiaibisha yeye na chama chake

Namba 1 amejiaibisha yeye na chama chake

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2020
Posts
7,799
Reaction score
14,215
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kwanza naomba niseme kuwa ninaufahamu, na kuuelewa vizuri ule msemo unaosema kuwa nyani akitaka kufa "basi miti yote atayojaribu kuishika hutereza". Hivyo nafahamu fika kwamba ule muda wa mwenyekiti ambae pia ni namba 1 wa chama kufa kisiasa upo, lkn sikutegemea kama muda huo ndio umeshafikia sasa hivi mpaka nilipoanza kusikia, na kuona mwenyekiti huyo wa chama kikuu cha upinzani, aliewahi kujijengea heshima kubwa katika siasa za Tanzania akijiaibisha kwa kujibishana na wakili fulani kanjanja anaetokea katika mkoa wa Mbeya, huku akishindwa kuelewa na kutambua kwamba kwa cheo chake, hadhi yake, umri wake na hata ukubwa wa chama chake hakutakiwa kamwe kupoteza muda wake, energy yake, sauti yake na mimbari ile kumjibu huyo wakili kanjanja na mlevi wa gongo.

Ni nani mwenye akili timamu asiefahamu kuwa wakili kanjanja yule alitumwa na yule Dr aliekuwa anashindia mihogo akarushe jiwe gizani, ili aone au asikie nani atakaemjibu, na yeye Dr mihogo apate pa kutokea na pengine kurudi tena kutrend katika midomo ya watu?

Suala la bandari limekufa kibudu, maandamano wanayopanga bila baraka ya chama chochote cha upinzani kuwa nyuma yao pia yameshakufa kibudu kabla hata ya kuanza, hivyo njia ya mwisho kwa wao kurudi tena kutrend ni hiyo ya kuattack vyama na viongozi wa vyama ili kujipatia uchochoro wa kutokea katika magazeti, mitandao na vyombo mbali mbali vya habari.

Sipingi yule kanjanja kujibiwa, ila napinga mtu alietumika kumjibu. Kiongozi mkuu wa chama kikuu kupoteza muda wake kumjibu wakili kanjanja na mlevi ni kujiaibisha yeye na chama chake. Ndiomaana hata makamu wa chama hajaonesha kulipa uzito sana swala hilo, maana anaufahamu mtego uliotegwa na Dr mihogo hivyo kawapuuza. Kitendo cha kumjibu yule kanjanja ni sawa na mtu mzima kumpiga mtoto wa miaka mitatu makonzi eti kisa alikuzomea, na wakati ungetumia hata njia ya mkato kwa kumpa kazi hiyo mtoto wako wa miaka minne amshikishe adabu.

Kwa kawaida yule kanjanja na aliemtuma walitakiwa wajibiwe angalau na katibu mkuu, au mwenyekiti wa chama wa kanda au mkoa wake, au chawa wengine humu JF.

Namalizia kwa kusema kuwa kile ni kinyago mlichokichonga wenyewe na kutaka kukitumia kisiasa katika swala la bandari, na mambo mengine ya kisiasa, hivyo pamoja na kwamba kinyago hicho kinaonesha kuasi kambi, lkn bado hakina sifa wala levo ya kujibiwa na mwenyekiti na namba 1 wa chama.
 
Amefanya kwa upande wake, hata akiishia tu hapo lakini kuna benefits tumeshazipata kama nchi kutokana na uanaharakati wake. ameiokoa nchi pakubwa sana, tunamshukuru na Mungu ambariki kwa hilo. si unaona hadi wametangaza tender bandari ya bagamoyo? na ule mswada wa kijinga umetupwa kwenye kapu la takataka. sio mafanikio hayo?
 
amefanya kwa upande wake, hata akiishia tu hapo lakini kuna benefits tumeshazipata kama nchi kutokana na uanaharakati wake. ameiokoa nchi pakubwa sana, tunamshukuru na Mungu ambariki kwa hilo. si unaona hadi wametangaza tender bandari ya bagamoyo? na ule mswada wa kijinga umetupwa kwenye kapu la takataka. sio mafanikio hayo?
Na kweli benefit kwa upande wake na genge lake (wewe ukiwa mmoja wapo) mmepata.

Kulipwa viela vya kula na kurushiwa bando kwenye PM zenu na wakwepa kodi wa bandarini wakishirikiana na wapiga madili mbali mbali pale bandarini halikuwa swala dogo.

Ila bahati nzuri mmiliki wa nchi tulie nae ni makini, mjanja, mwenye upeo na anaeelewa mambo mengi zaidi ya huyo wakili kanjanja na wachumia tumbo wenzake.

Imagine kama kiongozi wa nchi angekubali kushikiwa akili na huyo kanjanja, hali ingekuaje pale bandarini.

Mkataba uko pale pale, asiependa kusikia au kuona hivyo ahamie Malawi.
 
Nakukumbusha, kuna mtumwa kule Haiti aligeuka kuwa rais wa nchi
Narudia tena... Kiongozi namba 1 wa chama kikuu cha upinzani kumjibu wakili kanjanja na mlevi ni kosa kubwa la kiufundi.

Yani kama ni mpira basi Dr mihogo na wakili kanjanja waishampiga mwenyekiti na chama chake goli la tobo.
 
Narudia tena... Kiongozi namba 1 wa chama kikuu cha upinzani kumjibu wakili kanjanja na mlevi ni kosa kubwa la kiufundi.

Yani kama ni mpira basi Dr mihogo na wakili kanjanja waishampiga mwenyekiti na chama chake goli la tobo.
Una akili ndogo huwezi kunielewa.

Huyo unayemwita wakili kanjanjs atawaumbua sana
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kwanza naomba niseme kuwa ninaufahamu, na kuuelewa vizuri ule msemo unaosema kuwa nyani akitaka kufa "basi miti yote atayojaribu kuishika hutereza". Hivyo nafahamu fika kwamba ule muda wa mwenyekiti ambae pia ni namba 1 wa chama kufa kisiasa upo, lkn sikutegemea kama muda huo ndio umeshafikia sasa hivi mpaka nilipoanza kusikia, na kuona mwenyekiti huyo wa chama kikuu cha upinzani, aliewahi kujijengea heshima kubwa katika siasa za Tanzania akijiaibisha kwa kujibishana na wakili fulani kanjanja anaetokea katika mkoa wa Mbeya, huku akishindwa kuelewa na kutambua kwamba kwa cheo chake, hadhi yake, umri wake na hata ukubwa wa chama chake hakutakiwa kamwe kupoteza muda wake, energy yake, sauti yake na mimbari ile kumjibu huyo wakili kanjanja na mlevi wa gongo.

Ni nani mwenye akili timamu asiefahamu kuwa wakili kanjanja yule alitumwa na yule Dr aliekuwa anashindia mihogo akarushe jiwe gizani, ili aone au asikie nani atakaemjibu, na yeye Dr mihogo apate pa kutokea na pengine kurudi tena kutrend katika midomo ya watu?

Suala la bandari limekufa kibudu, maandamano wanayopanga bila baraka ya chama chochote cha upinzani kuwa nyuma yao pia yameshakufa kibudu kabla hata ya kuanza, hivyo njia ya mwisho kwa wao kurudi tena kutrend ni hiyo ya kuattack vyama na viongozi wa vyama ili kujipatia uchochoro wa kutokea katika magazeti, mitandao na vyombo mbali mbali vya habari.

Sipingi yule kanjanja kujibiwa, ila napinga mtu alietumika kumjibu. Kiongozi mkuu wa chama kikuu kupoteza muda wake kumjibu wakili kanjanja na mlevi ni kujiaibisha yeye na chama chake. Ndiomaana hata makamu wa chama hajaonesha kulipa uzito sana swala hilo, maana anaufahamu mtego uliotegwa na Dr mihogo hivyo kawapuuza. Kitendo cha kumjibu yule kanjanja ni sawa na mtu mzima kumpiga mtoto wa miaka mitatu makonzi eti kisa alikuzomea, na wakati ungetumia hata njia ya mkato kwa kumpa kazi hiyo mtoto wako wa miaka minne amshikishe adabu.

Kwa kawaida yule kanjanja na aliemtuma walitakiwa wajibiwe angalau na katibu mkuu, au mwenyekiti wa chama wa kanda au mkoa wake, au chawa wengine humu JF.

Namalizia kwa kusema kuwa kile ni kinyago mlichokichonga wenyewe na kutaka kukitumia kisiasa katika swala la bandari, na mambo mengine ya kisiasa, hivyo pamoja na kwamba kinyago hicho kinaonesha kuasi kambi, lkn bado hakina sifa wala levo ya kujibiwa na mwenyekiti na namba 1 wa chama.
Na huu ni upuuzi kama mwingine, kama swala LA bandari halina wizi na madudu, kwanini watu wakitaka kufanya kongamano kulijadili, CCM inatuma kenge wa polisi wakapige watu? Ndani, ya CCM, hakuna anayeweza kulielezea,
Hawa kenge ni majizi harafu mbumbumbu,
 
Wewe hujaelewa shida ilipoanzia, shida sio ushirika wa chama cha siasa bali shida ilianza pale walipopanga bajeti bila kumshirikisha Mwamba
Kwahiyo kumbe mwamba katumiwa na wajanja bila malipo 🤣🤣🤣

Ok mkuu... nishaanza kuelewa game linapoelekea.
 
Una akili ndogo huwezi kunielewa.

Huyo unayemwita wakili kanjanjs atawaumbua sana
Atawaumbua kina nani?

Unamaanisha atawaumbua mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani na genge lake, au kina nani?
 
Na huu ni upuuzi kama mwingine, kama swala LA bandari halina wizi na madudu, kwanini watu wakitaka kufanya kongamano kulijadili, CCM inatuma kenge wa polisi wakapige watu? Ndani, ya CCM, hakuna anayeweza kulielezea,
Hawa kenge ni majizi harafu mbumbumbu,
Kwahiyo kwa vile polisi wametumwa kuzuia kongamano lao, ndio hasira za huyo wakili kanjanja ziishie kuwashambulia wakubwa wa vyama vya upinzani kwa vile hawamsapoti.

Hata hivyo lengo la uzi sio hilo kongamano, bali lengo ni kuonesha kushangazwa na mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini kukimbilia kumjibu huyo jamaa na wakati kuna watu wa chini yake ambao wangeifanya kazi hiyo.
 
Mleta mada anaumwa na malaria ya ubongo

Swala la bandari sio ishu ya Simba na yanga ni swala muhimu kabisa la kitaifa.
Swala hapa, imekuaje mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini akimbilie kumjibu jamaa, wakati kazi hiyo ingefanywa na watu wa chini yake na chawa wengine kama kina Mmawia nk?
 
Back
Top Bottom