Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Wakili Gaspar Mwanalyela amejitokeza kuchukua fomu ya kugombea Urais kupitia Chadema ambapo moja ya vipaumbele vyake amesema atafumua mfumo wa elimu nchini na kusuka upya sambamba na kuahidi kutatua tatizo la ajira nchini.
Wakili huyo amesema, ameamua kugombea ili kurudisha matumaini kwa wananchi walio na hofu na wenye kukata tamaa.
Amesema, atafuata nyayo za Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, za kuanzisha vijiji vya ujamaa na kujitegemea na kwamba, atakwenda mbali zaidi kwa kuanzisha vijiji vya watalaamu.
Baba wa Taifa alianzisha vijiji vya ujamaa na kujitegemea. Tunapaswa kutengeza vijiji vya watalaamu wa madaktari, teknolojia na kilimo. vijiji hivi ni muhimu kuongeza ugunduzi na uvumbuzi.
Suala la vijiji vya ujamaa na kujitegemea vilivyoanzishwa na Mwalimu Nyerere, nabadilisha ili tuwe na muundo mzuri wa urithishanaji taaluma tutalijengea Taifa mustalabali mwema.
Ahadi yangu ni kutoa elimu juu ya kutambua haki na wajibu wao, sababu mtu hawezi kudai haki asiyofahamu na kutekeleza wajibu asiojua.
Hili litaenda sambamba na upatikanaji Katiba ya wananchi, kwa sababu ndani ya Katiba, mkataba wa kijamii unapatikana maana yake tukiwa na Katiba ya hovyo, taifa litakua la hovyo.
Nimeisikia wananchi wengi wakiwa wamekata tamaa, hata wengine wakipata mashaka wataingiaje kwenye uchaguzi huu.
Wapo wanaodhani hautakuwa wa maana na mantiki. Fursa hii ni adhimu, tuache woga tuingie ili tuendelee kudumu katika mustakabali wetu mwema.
Wakili huyo amesema, ameamua kugombea ili kurudisha matumaini kwa wananchi walio na hofu na wenye kukata tamaa.
Amesema, atafuata nyayo za Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, za kuanzisha vijiji vya ujamaa na kujitegemea na kwamba, atakwenda mbali zaidi kwa kuanzisha vijiji vya watalaamu.
Baba wa Taifa alianzisha vijiji vya ujamaa na kujitegemea. Tunapaswa kutengeza vijiji vya watalaamu wa madaktari, teknolojia na kilimo. vijiji hivi ni muhimu kuongeza ugunduzi na uvumbuzi.
Suala la vijiji vya ujamaa na kujitegemea vilivyoanzishwa na Mwalimu Nyerere, nabadilisha ili tuwe na muundo mzuri wa urithishanaji taaluma tutalijengea Taifa mustalabali mwema.
Ahadi yangu ni kutoa elimu juu ya kutambua haki na wajibu wao, sababu mtu hawezi kudai haki asiyofahamu na kutekeleza wajibu asiojua.
Hili litaenda sambamba na upatikanaji Katiba ya wananchi, kwa sababu ndani ya Katiba, mkataba wa kijamii unapatikana maana yake tukiwa na Katiba ya hovyo, taifa litakua la hovyo.
Nimeisikia wananchi wengi wakiwa wamekata tamaa, hata wengine wakipata mashaka wataingiaje kwenye uchaguzi huu.
Wapo wanaodhani hautakuwa wa maana na mantiki. Fursa hii ni adhimu, tuache woga tuingie ili tuendelee kudumu katika mustakabali wetu mwema.