Zanzibar 2020 Namba 9: Balozi Mstaafu Issa Suleimani Nassor achukua fomu ya kuombea Urais visiwani Zanzibar

Zanzibar 2020 Namba 9: Balozi Mstaafu Issa Suleimani Nassor achukua fomu ya kuombea Urais visiwani Zanzibar

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Zoezi la uchukuaji wa Fomu za kuwania nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM, lazidi kupamba moto ambapo Balozi Meja Jenerali Mstaafu Issa Suleimani Nassor wamefika Ofisini hapo kisiwandui kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo.

1592483890288.png


1592483913290.png
 
Juni 18, 2020
Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui
Unguja, Zanzibar
Tanzania

Balozi Major General (retired) Issa Suleiman Nassor achukua fomu kutia nia Urais SMZ 2020

Video toka Maktaba AFCON Egypt

Hili ni jina geni katika masikio ya wengi panapohusika siasa za Tanzania, lakini sio geni katika uwanja wa kijeshi. Major General Issa S. Nassor alifikia ngazi ya Mkuu wa Mafunzo na Operesheni wa JWTZ (Head of training and operations of the Tanzania People’s Defence Forces TPDF)

Jenerali Nassor amelitumikia Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa miaka mingi kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi nchini Misri kutoka mwaka 2017 hadi 2019. Makao yake yakiwa Cairo, Misri huku pia akiiwakilisha Tanzania katika nchi za Lebanon, Palestine, Libya, Iraq, Syria na Jordan. Major General Issa Suleiman Nassor aliwahi pia kuhudumu ktk Ubalozi wa Tanzania nchini India kama mwambata wa kijeshi Defence Attache ubalozini kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi wetu nchini Egypt (2017-2019).

Picha toka maktaba:
Oktoba 5, 2017.

Picha baada ya kuapishwa kwa Balozi H.E. Major General Mstaafu Issa Suleiman Nassor kuwa balozi wa Tanzania nchini Misri akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Rais John Pombe Joseph Magufuli na Mkuu wa Majeshi General Venace Mabeyo, Ikulu Dar es Salaam 05 October 2017.

Japo si jina kubwa katika siasa, duru visiwani Zanzibar zinamuelezea kama mtu asiye na mafungamano na siasa za makundi.

Naye anatajwa kubebwa na karata ya utiifu wake lakini hana umaarufu katika siasa za Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Hatima ya nafasi yake ikiwa ataingia katika kinyang'anyiro itaamuliwa na CCM yenyewe.
 
Zoezi la uchukuaji wa Fomu za kuwania nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM, lazidi kupamba moto ambapo Balozi Meja Jenerali Mstaafu Issa Suleimani Nassor wamefika Ofisini hapo kisiwandui kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo.

View attachment 1482457

View attachment 1482458
Huyu nae si akacheze na wajukuu tu
 
likuwa awe Mkuu wa Majeshi,wenzake wakamkwepesha na katupiwa kwenye ubalozi sijuwi kwa nini?
Sasa ndo wanataka kumpa Uraisi wa Zenji .
Ngoja awatende waliomtenda vibaya.
Kushinda kwa Kura Zanzibar hilo halipo, Lakini Akina jecha wanaweza kufanya Manuva kama kawaida yao
 
September 23, 2014

JK awapandisha saba JWTZ


NA MWANDISHI WETU
AMIRI Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo Maofisa saba wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kutoka cheo cha Brigedia hadi kuwa Meja Jenerali.

Hatua hiyo aliitekeleza kwa mujibu wa kanuni za majeshi ya ulinzi ya Tanzania ambazo zinatambulika kisheria.

Maofisa waliopandishwa vyeo ni Brigedia Jenerali Gaudence Milanzi, Brigedia Jenerali James Mwakibolwa, Brigedia Jenerali Ndetaulwa Zakayo na Brigedia Jenerali Venance Mabeyo.

Wengine ni Brigedia Jenerali Simon Mumwi, Brigedia Jenerali Issa Nassor na Brigedia Jenerali Rogastian Laswai, ambao wamekuwa na vyeo vya Meja Jenerali kuanzia Septemba 12, mwaka huu.

Katika tafrija ya kuwavisha vyeo vipya maofisa hao, iliyofanyika makao makuu ya jeshi eneo la Upanga, Dar es Salaam, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange, alimwakilisha Rais Kikwete.

Uteuzi huo pia umempandisha Meja Jenerali Gaudence Milanzi kuwa Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa (NDC).
Meja Jenerali Milanzi amechukua nafasi hiyo baada ya kustaafu kwa aliyekuwa Mkuu wa Chuo hicho, Luteni Jenerali Charles Makakala
 
Back
Top Bottom