Namba 13 - Mvaaji maarufu wa namba hiyo ni Michael Ballack.
Namba 13 inaaminiwa ni namba yenye mkosi zaidi duniani.
Michael Ballack amevaa namba 13 karibu maisha yote ya soka na hii ni mikosi yake:
1.Kufungwa Fainali ya World Cup 2002 ambapo Ujerumani alipoteza dhidi ya Brazil.
2.Kufungwa Fainali ya Champions League 2002, ambapo Bayer Leverkusen alifungwa 2-1 na Real Madrid, mtakumbuka lile goli maarufu la Zidane, ndilo goli la ushindi.
3. Kufungwa Fainali ya Euro 2008 ambapo Ballack na Ujerumani yake walifungwa na Spain Fainali.
4.Kufungwa Fainali ya Uefa Champions League, Ballack akiwa na Chelsea yake walifungwa na Man Utd kwa Matuta mwaka 2008.
5.Kuumia dakika za mwisho na kukosa World Cup ya mwaka 2010.