Ndugu yangu hii ni kesi ya madai na huwa inaanzia mahakaman na kwisha huko huko mahakaman.
unaweza ukaitumia hiyo hati pamoja na maelezo mliyoandikishana locally kama ushahidi wako. kwa kuanzia inabidi umwandikie barua huyo jamaa (demanding letter) ikimkumbusha kuwa unamdai kiasi fulan hivyo awe amekulipa ifikapo tarehe fulan, akishindwa kukulipa kufikia tarehe hiyo mueleze kuwa utamfikisha mahakaman. asipolipa, nenda na hiyo copy ya barua mahakan kafungue kesi ya madai.
endapo utashinda kesi, mahakama itamuamuru huyo jamaa kukulipa ndan ya muda fulan na kwa namna ipi. akishindwa kulipa hapo hatua ya attachment inaweza kufuata, ambapo mali yake yanayoweza kukulipa yanaweza kuamuliwa kuuzwa na ukapewa pesa yako au hata kuchukua ww mali hiyo kama thaman zitaendana.
kama hana kitu chochote cha kukufidia ww, anaweza kufungwa lkn anakuwa civil prisoner ambapo akiwa gerezan ww utamhudumia kwa chakula, matibabu jambo ambalo litakugharim ww tena.
kias unachomdai ndicho kitachozingatiwa kes ufungulie mahakama ipi.