Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 1,831
- 5,489
Mnamo mwaka 2019, Marehemu Rais Magufuli na na Rais wa Namibia, Geingob walikubaliana kuanzisha lugha ya Kiswahili katika shule za Namibia.
Mwezi huu, Wizara ya Elimu nchini Namibia ilitangaza kuwa Kiswahili hakitatolewa nchini Namibia na kufichua kuwa shule za Namibia zinapendelea lugha ya kichina inayojulikana kama 'Mandarin' kama mbadala wake.
Idadi ya Wachina nchini Namibia imeongezeka sana tangu uhuru.
Hivi majuzi mnamo mwaka 1998, Redio ya Kimataifa ya China iliripoti kuwa kulikuwa na Wachina 50 pekee wanaofanya biashara nchini Namibia, lakini kufikia 2005 idadi hiyo ilikuwa imeongezeka na kufikia zaidi ya 1,000. Ukadiriaji wa idadi ya wachina nchini Namibia kupitia Ubalozi wa Marekani wa 2009 uliootolewa na ofisi za kidiplomasia za Marekani uligundua kuna wachina waishio Namibia zaidi ya 3,000 au 4,000.
Wanasiasa wa upinzaji kama vile Jurie Viljoen wa Kikundi cha Monitor Action alitoa mashtaka kwamba utoaji vibali vya kazi kiholela umesababisha kuongezeka kwa wafanyakazi 40,000 wa kichina.
Wahamiaji wengi wa Kichina huanzisha biashara ndogo ndogo za rejareja hasa katika sekta ya nguo na vito. Kuwasili kwa wafanyabiashara kutoka china kumeleta malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara wa ndani kuhusu ushindani wa kibiashara na wasiwasi kuhusu ubora na usalama.
Hata hivyo, baadhi ya wananchi wa Namibia walikubali hali ya kuongezeka kwa Wachina katika sekta ya biashara za reja reja wakitaja manufaa ya kutengeneza ongezeko la ajira na kupunguza gharama za bidhaa.
Miaka ya 2000, biashara kati ya Uchina na Namibia ilikua kwa kasi, na kupanda kutoka dola milioni 75 mwaka wa 2003 hadi dola milioni 600 mwaka wa 2009. China City, kituo cha jumla na rejareja kilicho katika eneo la viwanda la kaskazini mwa mji mkuu 'Windhoek' takriban dakika 20 kutoka katikati mwa jiji hili, lilifunguliwa mwaka wa 1998 na Li Chengyuan (李澄原), mfanyabiashara kutoka Taiwan; kufikia mwaka wa 2005,
Wafanyabiashara walikuwa wakiagiza takriban makontena 1,000 ya bidhaa kwa mwaka kutoka China.
Eneo la Oshikango, mpakani na nchi ya Angola imekuwa kivutio maarufu kwa wafanyabiashara wa China wanaotarajia kunufaika na kupanua biashara ya mipakani. Kufikia 2004, mji ulikuwa na maduka 22 yanayomilikiwa na Wachina, na kupanuka hadi maduka 75 kufikia 2006.
Kutoka kuuza viatu na nguo, maduka haya yamepanua matoleo yao ya bidhaa na kujumuisha furniture, vifaa vya kielektroniki vya nyumbani, pikipiki, maua bandia na aina nyingine mbalimbali za bidhaa. Wamiliki wa maduka haya huingiza bidhaa zao kupitia bandari za Walvis Bay au Durban nchini Afrika Kusini, na kuzileta kwa reli ili zihifadhiwe katika ghala za dhamana, ambapo zinauzwa kwa wafanyabiashara wa Angola na kuuzwa Angola kwa kiasi kidogo, hivyo basi kuepuka kutoa ushuru wa forodha kwenda Angola.
Katika baadhi ya matukio ya kushangaza, wafanyabiashara hawa kutoka China wameanzisha na kufungua viwanda feki huko Oshikango ambavyo havizalishi bidhaa za ushindani wa kweli; kazi kuu ya viwanda hii ni kupata vibali vya kazi kwa Wachina kutoka nje ambao wanaweza kuja na kufanya kazi kama wasaidizi wa duka katika biashara za kuagiza bidhaa kuja Nambia na zingine kusafirisha nje ya nchi (Import/Export Businesses).
Kwa Afrika, Nchi inayoongoza kwa idadi kubwa ya Wachina ni Afrika kusini. Nchi nyinginezo ni kama Nigeria, Angola, Kenya, Zambia.
CHANZO: Namibian Schools Favor Mandarin Over Kiswahili
Soma: Kiswahili Chapingwa kufundishwa mashuleni Namibia
Mwezi huu, Wizara ya Elimu nchini Namibia ilitangaza kuwa Kiswahili hakitatolewa nchini Namibia na kufichua kuwa shule za Namibia zinapendelea lugha ya kichina inayojulikana kama 'Mandarin' kama mbadala wake.
Idadi ya Wachina nchini Namibia imeongezeka sana tangu uhuru.
Hivi majuzi mnamo mwaka 1998, Redio ya Kimataifa ya China iliripoti kuwa kulikuwa na Wachina 50 pekee wanaofanya biashara nchini Namibia, lakini kufikia 2005 idadi hiyo ilikuwa imeongezeka na kufikia zaidi ya 1,000. Ukadiriaji wa idadi ya wachina nchini Namibia kupitia Ubalozi wa Marekani wa 2009 uliootolewa na ofisi za kidiplomasia za Marekani uligundua kuna wachina waishio Namibia zaidi ya 3,000 au 4,000.
Wanasiasa wa upinzaji kama vile Jurie Viljoen wa Kikundi cha Monitor Action alitoa mashtaka kwamba utoaji vibali vya kazi kiholela umesababisha kuongezeka kwa wafanyakazi 40,000 wa kichina.
Wahamiaji wengi wa Kichina huanzisha biashara ndogo ndogo za rejareja hasa katika sekta ya nguo na vito. Kuwasili kwa wafanyabiashara kutoka china kumeleta malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara wa ndani kuhusu ushindani wa kibiashara na wasiwasi kuhusu ubora na usalama.
Hata hivyo, baadhi ya wananchi wa Namibia walikubali hali ya kuongezeka kwa Wachina katika sekta ya biashara za reja reja wakitaja manufaa ya kutengeneza ongezeko la ajira na kupunguza gharama za bidhaa.
Miaka ya 2000, biashara kati ya Uchina na Namibia ilikua kwa kasi, na kupanda kutoka dola milioni 75 mwaka wa 2003 hadi dola milioni 600 mwaka wa 2009. China City, kituo cha jumla na rejareja kilicho katika eneo la viwanda la kaskazini mwa mji mkuu 'Windhoek' takriban dakika 20 kutoka katikati mwa jiji hili, lilifunguliwa mwaka wa 1998 na Li Chengyuan (李澄原), mfanyabiashara kutoka Taiwan; kufikia mwaka wa 2005,
Wafanyabiashara walikuwa wakiagiza takriban makontena 1,000 ya bidhaa kwa mwaka kutoka China.
Eneo la Oshikango, mpakani na nchi ya Angola imekuwa kivutio maarufu kwa wafanyabiashara wa China wanaotarajia kunufaika na kupanua biashara ya mipakani. Kufikia 2004, mji ulikuwa na maduka 22 yanayomilikiwa na Wachina, na kupanuka hadi maduka 75 kufikia 2006.
Kutoka kuuza viatu na nguo, maduka haya yamepanua matoleo yao ya bidhaa na kujumuisha furniture, vifaa vya kielektroniki vya nyumbani, pikipiki, maua bandia na aina nyingine mbalimbali za bidhaa. Wamiliki wa maduka haya huingiza bidhaa zao kupitia bandari za Walvis Bay au Durban nchini Afrika Kusini, na kuzileta kwa reli ili zihifadhiwe katika ghala za dhamana, ambapo zinauzwa kwa wafanyabiashara wa Angola na kuuzwa Angola kwa kiasi kidogo, hivyo basi kuepuka kutoa ushuru wa forodha kwenda Angola.
Katika baadhi ya matukio ya kushangaza, wafanyabiashara hawa kutoka China wameanzisha na kufungua viwanda feki huko Oshikango ambavyo havizalishi bidhaa za ushindani wa kweli; kazi kuu ya viwanda hii ni kupata vibali vya kazi kwa Wachina kutoka nje ambao wanaweza kuja na kufanya kazi kama wasaidizi wa duka katika biashara za kuagiza bidhaa kuja Nambia na zingine kusafirisha nje ya nchi (Import/Export Businesses).
Kwa Afrika, Nchi inayoongoza kwa idadi kubwa ya Wachina ni Afrika kusini. Nchi nyinginezo ni kama Nigeria, Angola, Kenya, Zambia.
CHANZO: Namibian Schools Favor Mandarin Over Kiswahili
Soma: Kiswahili Chapingwa kufundishwa mashuleni Namibia