Thecoder
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 1,590
- 4,244
Maisha huwa yako na utangulizi kama ambavyo ilivyo kwenye vitabu mbalimbali, na lengo la utangulizi wa kwenye maisha huwa unamlengo sawa sawa na ule ambao upo au unawekwa kwenye vitabu vya kawaida.
Tofauti ya utangulizi wa kwenye vitabu na ule wa kwenye maisha ni kwamba kwenye vitabu huwa kuna kuwa na utangulizi mwanzoni mwa kitabu halafu ndio habari kamili inafuata ila kwenye maisha huwa kuna kua na utangulizi wa awali, ambao huu huwa ni utangulizi wa safari yako ya maisha kwa ujumla lakini pia huwa kuna utangulizi mdogo mdogo ambao huu huwa unatokea mara kwa mara kwenye maisha ya Kila mmoja na lengo lake likiwa ni kukupa njia ya kufanikisha mambo madogo madogo yanayohitajika kukamilika ili kufungua njia ielekeayo kwenye hatima yako.
Na lengo kuu la utangulizi uliopo kwenye kitabu cha maisha ya Kila mwanadamu ni kumuonesha namna atakavyopiga hatua kuelekea kwenye lile lengo kuu la kimungu ambalo lilifanya yeye awepo hapa duniani.
Kwahiyo kupitia ule utangulizi wa jumla, utakufanya uweze kujua ugumu na urahisi wa wewe kwenda kutimiza hatima yako.
Na kwakupitia utangulizi huu utakufanya uweze kuchagua njia za kupita kwa umakini mkubwa sana.
Sasa, utangulizi wa jumla huwa unapatikana kwenye familia au ukoo ambao wewe umezaliwa.
Kivipi?...
Ni hivi, kama ukoo au familia ambayo wewe umezaliwa, swala la pesa kwa watu wa ukoo au familia hiyo halijawahi kusumbua, basi hata wewe pindi utakapoanza harakati zako za kuelekea kwenye hatima yako swala la fedha linaweza lisiwe shida sana hasa kama utaziendea njia zako kwa uadilifu.
Na kama umezaliwa kwenye familia au ukoo fukara, ukoo ambao mtu tajiri ni yule ambae ako na kibanda cha vyumba vitatu Daslam, basi huu ni utangulizi ya kwamba kuna minyororo utatakiwa kuikata ili uweze kwenda beyond na asili ya ukoo wenu.
Kama umezaliwa kwenye familia ambayo, mtu aliyesoma zaidi ni yule ambae ameishia kidato cha nne, na huyo ndio mtu ambae huwa anatolewa mfano kwa vijana wote wanaotaka kufika mbali kielimu, na ikiwa hatima yako wewe imefungamana moja kwa moja na elimu, basi huo ni utangulizi ya kwamba ili uweze kufikia ile hatima yako ni lazima uvunje minyororo yote iliyokuwa inawazuia watu wa familia au ukoo wenu washindwe kufika mbali kielimu.
Kwahiyo utangulizi wa jumla wa namna unavyopaswa kupiga hatua zako ili uweze kuziendea ndoto zako kwa maana ya yale maisha ya hatima yako huwa unapatikana kwa kuangalia aina ya familia ambayo wewe umezaliwa kisha pima ndoto yako na familia uliyotoka inaweza kutimia kwa ugumu au kwa urahisi kiasi gani.
Kuna watu wametoka kwenye familia au koo za kidini sana koo ambazo zinaamini sana kwenye maadili yanayo waongoza na si vinginevyo, lakini watu hawa walikua na hatima zilizo nje ya maadili ya familia zao, unakuta mtu anakipaji cha kuimba muziki wa kidunia au anakipaji cha kuigiza na kadhalika, na ukiangalia jinsi familia au ukoo wake ulivyo ni ngumu kuweza kuruhusiwa kwenda kwenye huo upande, kwahiyo ili uweze kutimiza hatima yako ni lazima ukate ile minyororo yote inayosababisha watu wa familia au ukoo wako wasiamini kwenye vipawa vya upande huo ambao wewe unataka kutumika nao.
Ndio maana utaona ya kwamba, hatua ambazo Mimi nazipiga kuelekea kwenye hatima yangu huwa ni tofauti na zile ambazo wewe unapiga kuelekea kwenye hatima yako lakini pia ni tofauti na zile ambazo yule anapiga kuelekea kwenye hatima yake na hii yote huwa inatokana na aina ya utangulizi ambao tumepata kuusoma kwenye koo au familia zetu.
Na watu wengi wanachelewa kwenye maisha kwasababu huwa wanapuuzia hivi vitu, na kinachosababisha watu wengi wapuuzie hivi vitu ni kwamba wengi hawajui hatima za wao kuwa hapa ni zipi.
Ile kutokujua hupelekea mtu ashindwe kuchagua njia itakayo mpeleka huko kwa usahihi na badala yake anajikuta anaingia kwenye mtego ambao watu wengi wa familia au ukoo wake wameuingia na kujikuta anakua sawa na wengine ambao wako kwenye familia au ukoo huo.
Naelewa ya kwamba hivi ni vitu ambavyo tulitakiwa tuwe tunasaidiwa na wazazi wetu hasa kwa zile nyakati ambazo tulikua tupo chini yao, lakini si wazazi wote ambao wako na uelewa wa haya na badala yake wazazi wengi wako na uelewa sana na maswala ya shule kwasababu ni sheria na hii ni bila kujali hatima ya mtoto iko upande gani.
Na kama wewe ni miongoni mwa watu ambao hawakuwahi kuusoma utangulizi wa jumla wa maisha yao basi unaouwezo wa kuusoma huo utangulizi sasa hivi kisha anza Kutafakari ya kwamba hizo ndoto kubwa ambazo ziko ndani yako zina uwiano gani na watu wa ukoo au familia yako(hapa kuna code ya mambo mengi ya kiroho nitakuja kuisema nikipata wasaa).
Je, umeshawahi kuskia mtu yeyote kwenye ukoo wako amewahi kufikia kwenye kiwango cha ukubwa wa hiyo ndoto yako?
Kama ni hapana, unatakiwa ujiulize kwanini? Na hapa kwenye kwanini ndio unatakiwa utumie muda mrefu sana kwa maana hapa ndipo ambapo patakuchagulia njia za kupita na namna ambavyo unapaswa kupiga hatua zako ili uweze kuelekea huko unakotaka uelekee, kwasababu maji huwa yanakawaida ya kufuata mkondo na ili maji yasifuate ule mkondo uliozoeleka ni lazima uyachepushe(hauwezi kujua mkondo wa maji uliyopo kama haujui historia ya ukoo wenu).
Lakini nasema hivi, maisha ni complex puzzle ambayo huwezi kuisolve pasipo kuigawa kwenye vipande vidogo vidogo, na kwenye Kila kipande ambacho utakigawa huwa kinakua na utangulizi wake ambao huwa unatoa namna ya kwenda kuisolve hiyo puzzle, na hapa sasa ndio tunaenda kuipata ile aina ya pili ya utangulizi ambao huwa upo kwenye maisha ya Kila mwanadamu (kumbuka hapo juu nilizungumzia utangulizi wa jumla).
Sasa hapa, huwa kuna shida moja ambayo mara nyingi hujitokeza, ni kwamba dunia huendeshwa kwa nguvu kuu mbili ambazo hufanya haya maisha yazidi kuwa ya kufurahisha, na nguvu hizo ndio huwa tunaziita hasi na chanya(I don't care kama hauamini, ila endelea kusoma kwa maana kuna jambo nataka kusema na wewe).
Kwenye kila njia chanya ambayo utaitumia kusolve hiyo puzzle yako ndogo ambayo itakusaidia kupiga hatua kuelekea kwenye maisha ya hatima yako pia kuna njia hasi ambayo inafanana karibia kila kitu na hiyo chanya ila yenyewe ukiipita haitakusaidia kwenda mbele bali itakusaidia kurudi nyuma kwa hatua kadhaa wakati wa hayo mapambano ya kuelekea kwenye hatima yako.
Okay iko hivi, unandoto ya kuja kuwa mfanyabiashara mkubwa na ukapambana kweli ukapata goal lako ukawa unauza hiko umachokiuza, huwa uko na kawaida ya kwamba mzigo ukiisha unaenda sehemu fulani kununua na kuujaza hapo goalini kwako ili biashara iendelee, kuna siku umekaa anakuja mtu anakwambia yuko na mzigo anauza na anakutajia bei fulani ambayo iko chini kuliko ile ambayo wewe unanunuliaga hizo bidhaa siku zote, unamuuliza kuhusu uhalali wa bidhaa hiyo anakuhakikishia kwa asilimia zote huku akikupa na mifano ya wafanya biashara wengine ambao huwa anafanya nao biashara mara kwa mara.
Unaona ni sawa unamwambia akuletee mzigo anauleta unauza unapata faida nzuri kwa maana bei iko chini kuliko kule ambako huwa umezoea kununua, anakuletea tena na tena ila siku moja isiyojulikana unashangaa polisi wanakuja kuvamia hapo goalini kwako wakisema unatuhumiwa kwa kununua bidhaa za magendo, unabaki tu kushangaa ila unaelekezwa vizuri na unaelewa, kisha kesi inahukumiwa na kuonekana uko na hatia na kupigwa fine ya pesa ambayo inaondoka na mtaji wako wote, kwahiyo unafunga zako duka unarudi zako mtaani kujitafuta upya.
Umeona sasa hiyo scenario, njia ya kwanza ambayo ulikua unaitumia kununua mzigo haikua na utofauti sana na njia ya pili ila moja ilikua kwenye upande chanya na moja ilikua kwenye upande hasi, moja ikiwa na lengo la kukupeleka mbele lakini moja ikiwa na lengo la kukurudisha nyuma (hii ni kitu ambayo unatakiwa uwe nayo akilini Kila siku kwenye hustling zako, ya kwamba always hasi na chanya huwa zipo karibu sana hasa unapopata njia ya kusolve puzzle fulani ya maisha yako).
Lakini pia unatakiwa uelewe ya kwamba, tulioitwa ni wengi ila wateuliwa ni wachache ya kwamba si kila mtu ataishi huku akiwa ameifikia hatima yake, kwa maana kuifikia hatima huwa inahitaji mtu mwenye uwezo mzuri wa kutumia mwili wake pamoja na milango yake ya fahamu kwa uzuri zaidi, mtu mnyenyekevu asiye mjivuni lakini anaelewa namna dunia inavyofanya kazi.
Kwa maana puzzle nyingi huwa zinaanza kusolviwa kuanzia unapokanyaga mguu wako chini ile asubuhi kutoka kitandani mwako, na kuanzia mtu wa kwanza unaekutana nae hadi mtu wa mwisho, ambao unawafahamu na ambao hauwafahamu ila umepata kuunganika nao kwa namna isiyo ya kawaida ili hali haujawahi kuonana nao tangu uzaliwe.
Hawa wote wameandaliwa kwaajiri ya kusolve puzzle fulani iliyo kwenye njia inayoelekea kwenye hatima yako na sio lazima iwe puzzle ya siku hiyo au kesho ila kuna siku moja kuna puzzle itakushinda kuisolve wewe binafsi ila ghafla utajikuta unakumbuka ulishawahi kukutana na mtu fulani na mliongea mambo ya namna hiyo, kwahiyo kama uliona anakushobokea na wewe hukumzingatia hapa ndio utaanza kujutia like ayaaaa alinipa namba ila sikuisave bhana😅 (kuwa na akili ya kutokuchukulia vitu au watu poa, hasa ambao wanakuja kwenye maisha yako kwa ghafla na mnajikuta mnakua na connection ya kuwafanya mjisahau kama ndio mmekutana Leo, lakini pia usisahau ya kwamba Kila kwenye chanya kuna hasi, kwahiyo hupaswi kumuamini mtu wa namna hiyo kwa haraka ila pia hautakiwi kumpuuza mtu wa namna hiyo kwa haraka cha zaidi mzingatie kwa asilimia zote kisha acha asili ifanye kazi yake).
Wacha niishie hapa kwa Leo ila nitarudi ikiniladhim…
Tofauti ya utangulizi wa kwenye vitabu na ule wa kwenye maisha ni kwamba kwenye vitabu huwa kuna kuwa na utangulizi mwanzoni mwa kitabu halafu ndio habari kamili inafuata ila kwenye maisha huwa kuna kua na utangulizi wa awali, ambao huu huwa ni utangulizi wa safari yako ya maisha kwa ujumla lakini pia huwa kuna utangulizi mdogo mdogo ambao huu huwa unatokea mara kwa mara kwenye maisha ya Kila mmoja na lengo lake likiwa ni kukupa njia ya kufanikisha mambo madogo madogo yanayohitajika kukamilika ili kufungua njia ielekeayo kwenye hatima yako.
Na lengo kuu la utangulizi uliopo kwenye kitabu cha maisha ya Kila mwanadamu ni kumuonesha namna atakavyopiga hatua kuelekea kwenye lile lengo kuu la kimungu ambalo lilifanya yeye awepo hapa duniani.
Kwahiyo kupitia ule utangulizi wa jumla, utakufanya uweze kujua ugumu na urahisi wa wewe kwenda kutimiza hatima yako.
Na kwakupitia utangulizi huu utakufanya uweze kuchagua njia za kupita kwa umakini mkubwa sana.
Sasa, utangulizi wa jumla huwa unapatikana kwenye familia au ukoo ambao wewe umezaliwa.
Kivipi?...
Ni hivi, kama ukoo au familia ambayo wewe umezaliwa, swala la pesa kwa watu wa ukoo au familia hiyo halijawahi kusumbua, basi hata wewe pindi utakapoanza harakati zako za kuelekea kwenye hatima yako swala la fedha linaweza lisiwe shida sana hasa kama utaziendea njia zako kwa uadilifu.
Na kama umezaliwa kwenye familia au ukoo fukara, ukoo ambao mtu tajiri ni yule ambae ako na kibanda cha vyumba vitatu Daslam, basi huu ni utangulizi ya kwamba kuna minyororo utatakiwa kuikata ili uweze kwenda beyond na asili ya ukoo wenu.
Kama umezaliwa kwenye familia ambayo, mtu aliyesoma zaidi ni yule ambae ameishia kidato cha nne, na huyo ndio mtu ambae huwa anatolewa mfano kwa vijana wote wanaotaka kufika mbali kielimu, na ikiwa hatima yako wewe imefungamana moja kwa moja na elimu, basi huo ni utangulizi ya kwamba ili uweze kufikia ile hatima yako ni lazima uvunje minyororo yote iliyokuwa inawazuia watu wa familia au ukoo wenu washindwe kufika mbali kielimu.
Kwahiyo utangulizi wa jumla wa namna unavyopaswa kupiga hatua zako ili uweze kuziendea ndoto zako kwa maana ya yale maisha ya hatima yako huwa unapatikana kwa kuangalia aina ya familia ambayo wewe umezaliwa kisha pima ndoto yako na familia uliyotoka inaweza kutimia kwa ugumu au kwa urahisi kiasi gani.
Kuna watu wametoka kwenye familia au koo za kidini sana koo ambazo zinaamini sana kwenye maadili yanayo waongoza na si vinginevyo, lakini watu hawa walikua na hatima zilizo nje ya maadili ya familia zao, unakuta mtu anakipaji cha kuimba muziki wa kidunia au anakipaji cha kuigiza na kadhalika, na ukiangalia jinsi familia au ukoo wake ulivyo ni ngumu kuweza kuruhusiwa kwenda kwenye huo upande, kwahiyo ili uweze kutimiza hatima yako ni lazima ukate ile minyororo yote inayosababisha watu wa familia au ukoo wako wasiamini kwenye vipawa vya upande huo ambao wewe unataka kutumika nao.
Ndio maana utaona ya kwamba, hatua ambazo Mimi nazipiga kuelekea kwenye hatima yangu huwa ni tofauti na zile ambazo wewe unapiga kuelekea kwenye hatima yako lakini pia ni tofauti na zile ambazo yule anapiga kuelekea kwenye hatima yake na hii yote huwa inatokana na aina ya utangulizi ambao tumepata kuusoma kwenye koo au familia zetu.
Na watu wengi wanachelewa kwenye maisha kwasababu huwa wanapuuzia hivi vitu, na kinachosababisha watu wengi wapuuzie hivi vitu ni kwamba wengi hawajui hatima za wao kuwa hapa ni zipi.
Ile kutokujua hupelekea mtu ashindwe kuchagua njia itakayo mpeleka huko kwa usahihi na badala yake anajikuta anaingia kwenye mtego ambao watu wengi wa familia au ukoo wake wameuingia na kujikuta anakua sawa na wengine ambao wako kwenye familia au ukoo huo.
Naelewa ya kwamba hivi ni vitu ambavyo tulitakiwa tuwe tunasaidiwa na wazazi wetu hasa kwa zile nyakati ambazo tulikua tupo chini yao, lakini si wazazi wote ambao wako na uelewa wa haya na badala yake wazazi wengi wako na uelewa sana na maswala ya shule kwasababu ni sheria na hii ni bila kujali hatima ya mtoto iko upande gani.
Na kama wewe ni miongoni mwa watu ambao hawakuwahi kuusoma utangulizi wa jumla wa maisha yao basi unaouwezo wa kuusoma huo utangulizi sasa hivi kisha anza Kutafakari ya kwamba hizo ndoto kubwa ambazo ziko ndani yako zina uwiano gani na watu wa ukoo au familia yako(hapa kuna code ya mambo mengi ya kiroho nitakuja kuisema nikipata wasaa).
Je, umeshawahi kuskia mtu yeyote kwenye ukoo wako amewahi kufikia kwenye kiwango cha ukubwa wa hiyo ndoto yako?
Kama ni hapana, unatakiwa ujiulize kwanini? Na hapa kwenye kwanini ndio unatakiwa utumie muda mrefu sana kwa maana hapa ndipo ambapo patakuchagulia njia za kupita na namna ambavyo unapaswa kupiga hatua zako ili uweze kuelekea huko unakotaka uelekee, kwasababu maji huwa yanakawaida ya kufuata mkondo na ili maji yasifuate ule mkondo uliozoeleka ni lazima uyachepushe(hauwezi kujua mkondo wa maji uliyopo kama haujui historia ya ukoo wenu).
Lakini nasema hivi, maisha ni complex puzzle ambayo huwezi kuisolve pasipo kuigawa kwenye vipande vidogo vidogo, na kwenye Kila kipande ambacho utakigawa huwa kinakua na utangulizi wake ambao huwa unatoa namna ya kwenda kuisolve hiyo puzzle, na hapa sasa ndio tunaenda kuipata ile aina ya pili ya utangulizi ambao huwa upo kwenye maisha ya Kila mwanadamu (kumbuka hapo juu nilizungumzia utangulizi wa jumla).
Sasa hapa, huwa kuna shida moja ambayo mara nyingi hujitokeza, ni kwamba dunia huendeshwa kwa nguvu kuu mbili ambazo hufanya haya maisha yazidi kuwa ya kufurahisha, na nguvu hizo ndio huwa tunaziita hasi na chanya(I don't care kama hauamini, ila endelea kusoma kwa maana kuna jambo nataka kusema na wewe).
Kwenye kila njia chanya ambayo utaitumia kusolve hiyo puzzle yako ndogo ambayo itakusaidia kupiga hatua kuelekea kwenye maisha ya hatima yako pia kuna njia hasi ambayo inafanana karibia kila kitu na hiyo chanya ila yenyewe ukiipita haitakusaidia kwenda mbele bali itakusaidia kurudi nyuma kwa hatua kadhaa wakati wa hayo mapambano ya kuelekea kwenye hatima yako.
Okay iko hivi, unandoto ya kuja kuwa mfanyabiashara mkubwa na ukapambana kweli ukapata goal lako ukawa unauza hiko umachokiuza, huwa uko na kawaida ya kwamba mzigo ukiisha unaenda sehemu fulani kununua na kuujaza hapo goalini kwako ili biashara iendelee, kuna siku umekaa anakuja mtu anakwambia yuko na mzigo anauza na anakutajia bei fulani ambayo iko chini kuliko ile ambayo wewe unanunuliaga hizo bidhaa siku zote, unamuuliza kuhusu uhalali wa bidhaa hiyo anakuhakikishia kwa asilimia zote huku akikupa na mifano ya wafanya biashara wengine ambao huwa anafanya nao biashara mara kwa mara.
Unaona ni sawa unamwambia akuletee mzigo anauleta unauza unapata faida nzuri kwa maana bei iko chini kuliko kule ambako huwa umezoea kununua, anakuletea tena na tena ila siku moja isiyojulikana unashangaa polisi wanakuja kuvamia hapo goalini kwako wakisema unatuhumiwa kwa kununua bidhaa za magendo, unabaki tu kushangaa ila unaelekezwa vizuri na unaelewa, kisha kesi inahukumiwa na kuonekana uko na hatia na kupigwa fine ya pesa ambayo inaondoka na mtaji wako wote, kwahiyo unafunga zako duka unarudi zako mtaani kujitafuta upya.
Umeona sasa hiyo scenario, njia ya kwanza ambayo ulikua unaitumia kununua mzigo haikua na utofauti sana na njia ya pili ila moja ilikua kwenye upande chanya na moja ilikua kwenye upande hasi, moja ikiwa na lengo la kukupeleka mbele lakini moja ikiwa na lengo la kukurudisha nyuma (hii ni kitu ambayo unatakiwa uwe nayo akilini Kila siku kwenye hustling zako, ya kwamba always hasi na chanya huwa zipo karibu sana hasa unapopata njia ya kusolve puzzle fulani ya maisha yako).
Lakini pia unatakiwa uelewe ya kwamba, tulioitwa ni wengi ila wateuliwa ni wachache ya kwamba si kila mtu ataishi huku akiwa ameifikia hatima yake, kwa maana kuifikia hatima huwa inahitaji mtu mwenye uwezo mzuri wa kutumia mwili wake pamoja na milango yake ya fahamu kwa uzuri zaidi, mtu mnyenyekevu asiye mjivuni lakini anaelewa namna dunia inavyofanya kazi.
Kwa maana puzzle nyingi huwa zinaanza kusolviwa kuanzia unapokanyaga mguu wako chini ile asubuhi kutoka kitandani mwako, na kuanzia mtu wa kwanza unaekutana nae hadi mtu wa mwisho, ambao unawafahamu na ambao hauwafahamu ila umepata kuunganika nao kwa namna isiyo ya kawaida ili hali haujawahi kuonana nao tangu uzaliwe.
Hawa wote wameandaliwa kwaajiri ya kusolve puzzle fulani iliyo kwenye njia inayoelekea kwenye hatima yako na sio lazima iwe puzzle ya siku hiyo au kesho ila kuna siku moja kuna puzzle itakushinda kuisolve wewe binafsi ila ghafla utajikuta unakumbuka ulishawahi kukutana na mtu fulani na mliongea mambo ya namna hiyo, kwahiyo kama uliona anakushobokea na wewe hukumzingatia hapa ndio utaanza kujutia like ayaaaa alinipa namba ila sikuisave bhana😅 (kuwa na akili ya kutokuchukulia vitu au watu poa, hasa ambao wanakuja kwenye maisha yako kwa ghafla na mnajikuta mnakua na connection ya kuwafanya mjisahau kama ndio mmekutana Leo, lakini pia usisahau ya kwamba Kila kwenye chanya kuna hasi, kwahiyo hupaswi kumuamini mtu wa namna hiyo kwa haraka ila pia hautakiwi kumpuuza mtu wa namna hiyo kwa haraka cha zaidi mzingatie kwa asilimia zote kisha acha asili ifanye kazi yake).
Wacha niishie hapa kwa Leo ila nitarudi ikiniladhim…