Namna pekee ya kuzuia Corona virus kusambaa

Namna pekee ya kuzuia Corona virus kusambaa

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Covid-19 ugonjwa usababishwao na Corona virus hadi sasa hauna tiba wala chanjo. Waliopona ugonjwa huu wamepona si kwa kuwa walikuwa wakitibiwa Covid-19 bali zaidi kwa bahati zao na kudra za mwenyezi Mungu.

Ugonjwa huu unaua. Hata aliyeugua akapona, anaweza kuugua tena na tena, akapona tena au hata akafa. Bahati na kudra za mwenyezi Mungu huwa hazipo kila siku. Wanasema waswahili, "bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi."

Ni kwa sababu ya kutokuwa na tiba kamili ya ugonjwa huu, kwa maelfu ya watu waliokwisha ambukizwa: USA, Italy, Spain , nk, vifo vimekuwa vikiongezeka na vikipindukia hata zaidi ya 900 kwa siku kwa nchi kwa nchi na kwa siku kadhaa mfululizo sasa.

Tatizo kubwa zaidi na ugonjwa huu liko katika kasi yake ya maambukizi ambapo maelfu ya watu wanaweza kuambukizwa katika muda mfupi tu:

1. Mtu aliyeathirika ataambukiza wote anaohusishwa nao hata kwa ukaribu tu.

2. Kila aliyeambukizwa na aliyeathirika, naye ataambukiza wote atakaohusishwa nao hata kwa ukaribu wao tu.

3. Kila aliyeambukizwa, naye ataambukiza wote atakaohusishwa nao pia,hata kwa ukaribu wao tu.

4. Hii ambukizwa ambukiza huendelea hivyo kwa kasi ya mithili ya mlipuko wa bomu.

Kwa vile pia pana suala la hewa linalohusishwa kwenye kuenea au kuambukiza kwake, huu ugonjwa unamuweka kila mtu hatarini.

Ugonjwa huu unaambukizwa na kusambaa kisayansi ambapo njia pekee ya kisayansi ya kuudhibiti, imefahamika kuwa ni katika kupambana kuuvunja mlolongo na mnyororo wake wa maambukizi.

Rejea mada hii kutoka World Economic Forum (WEF) inayoangazia ufumbuzi pekee na kamili ya kuzuia maambukizi ya covid-19:

Why lockdowns can halt the spread of COVID-19

Muhimu kutumia muda kusoma na kuelewa.

Ubinafsi, itikadi, imani, kukurupuka, nk ni muhimu kukuweka pembeni, japo kwa muda.

Total lockdown pamoja na machungu yake ndiyo inayoweza kutuokoa na sisi pia ili kutokuangamia na gonjwa hili lisilo na tiba.

Mbaya zaidi ni kuwa muda wa total lockdown utakuwa mrefu zaidi kama tutachelewa mno kuanza kuitumia.

Kwa hisani (Mwana JF) "remote" katika picha ni uwezekano wa maambukizi ya yule mgonjwa wa kwanza (Tanzania Corona patient zero):

IMG_20200404_150834_400.jpg



NB: "Akili za kuambiwa changanya na za kwako". Mwisho wa kumnukuu.
 
Vipi kuna wagonjwa wengine WAMEPATIKANA?
Covid-19 ugonjwa usababishwao na Corona virus hadi sasa hauna tiba wala chanjo. Waliopona ugonjwa huu wamepona si kwa kuwa walikuwa wakitibiwa Covid-19 bali zaidi kwa bahati zao na kudra za mwenyezi Mungu.

Ugonjwa huu unaua. Hata aliyeugua akapona, anaweza kuugua tena na tena, akapona au hata akafa. Bahati na kudra za mwenyezi Mungu huwa hazipo kila siku. Wanasema waswahili bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi.

Ni kwa sababu ya kutokuwa na tiba kamili ya ugonjwa huu, kwa maelfu ya watu waliokwisha ambukizwa: USA, Italy na Spain vifo vimekuwa vikiongezeka na vikipindukia hata zaidi ya 900 kwa siku kwa nchi kwa nchi na kwa siku kadhaa mfululizo sasa.

Tatizo kubwa zaidi na ugonjwa huu liko katika kasi yake ya maambukizi ambapo maelfu ya watu wanaweza kuambukizwa katika muda mfupi tu:

1. Mtu aliyeathirika ataambukiza wote anaohusishwa nao hata kwa ukaribu tu.

2. Kila aliyeambukizwa na aliyeathirika, naye ataambukiza wote atakaohusishwa nao hata kwa ukaribu tu.

3. Kila aliyeambukizwa, naye ataambukiza wote atakaohusishwa nao pia,hata kwa ukaribu wao tu.

4. Hii ambukizwa ambukiza huendelea hivyo kwa kasi ya mithili ya mlipuko wa bomu.

Kwa vile pia pana suala la hewa linalohusishwa kwenye kuenea au kuambukiza kwake, huu ugonjwa unamuweka kila mtu hatarini.

Ugonjwa huu unaambukizwa na kusambaa kisayansi ambapo njia pekee ya kisayansi ya kuudhibiti ugonjwa huu, imefahamika kisayansi kuwa katika kupambana kuuvunja mlolongo wa mnyororo wake wa maambukizi:

Rejea mada hii kutoka World Economic Forum (WEF) inayoangazia ufumbuzi pekee na kamili ya kuzuia maambukizi ya covid-19:

Why lockdowns can halt the spread of COVID-19

Muhimu kutumia muda kusoma kwanza kuelewa.

Ubinafsi, itikadi, imani, nk ni muhimu kujiweka pembeni. Total lockdown pamoja na machungu yake ndiyo iliyothibitishwa kisayansi kama njia pekee kwa sasa inayoweza kuyaokoa mataifa kuangamia na Corona.

Mbaya zaidi ni kuwa muda wa total lockdown utakuwa mrefu zaidi kama tutachelewa mno kuanza kuitumia.

Kwa hisani Mwana JF, remote katika picha ni uwezekano wa maambukizi na yule mgonjwa wa kwanza (Tanzania Corona patient zero):

View attachment 1408672


NB: "Akili za kuambiwa changanya na za kwako". Mwisho wa kumnukuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi kuna wagonjwa wengine WAMEPATIKANA?

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa vile hujaambiwa haina maana kuwa hawajaongezeka.

Nota bene hukuliona pale?

"Akili za kuambiwa changanya na za kwako".

Hivi hata umeisoma ile article ya WEF? Je hata umeiona? Na je umeielewa?

Au umekurupuka kudandia treni kwa mbele.

Mawazo yako Isabella tokea KIA, Arusha, Mount Meru hospitali na kote alikopita unaambiwa hakuambukiza mtu, na wewe unakubali? Labda kama alikuwa na malaria tu.

Angalia mkuu utauzwa mchana mchana.
 
Kwa MTU anayeijua Tanzania vizuri na maisha ya Watanzania yalivyo hawezi kushauri total lockdown, labda kama hana akili timamu.

Article ya WEF umeisoma?

Tunauvunja vipi huu mnyororo wa maambukizi?

Ni mtu ajabu tu ndiye anayeweza kudhani huu ugonjwa utakwisha wenyewe bila kuuvunja mnyororo wa maambukizi wa ugonjwa huu.

Mkuu nini njia mbadala? Au tusubirie kufa tu?
 
Masharti ya UKIMWI yalikua madogo sana.
1. Epuka ngono
2. Ama uwe na mpenzi mmoja mwaminifu na
3. Ukishindwa kabisa tumia kondom.
VERY SIMPLE bado watu walipukutika kwa starehe ya dakika tano tuh.
MASHARTI YA KIPINDUPINDU NDIO MADOGO ZAIDI
1. Epuka uchafu
2. Uwe msafi
3. Kula visafi
SASA HII
1. Epuka misongamano
2. Vaa mask
3. Usiwasalimie jirani
4. Unawe
5. Unywe maji
6. Usukutue na maji chumvi
7. Ukae nyumbani tu
8. Bar, sokoni, mpirani, kilabuni etc marufuku
9. Usisafiri
N.k
Niambie mtanzania na kunawa mikono wapi na wapi.
Kuvaa kondom tu tena zilitolewa bure na ikiuzwa ni mia watu wamekufa. Itakua sabuni, sanitaiza, maski nk?
 
Masharti ya UKIMWI yalikua madogo sana.
1. Epuka ngono
2. Ama uwe na mpenzi mmoja mwaminifu na
3. Ukishindwa kabisa tumia kondom.
VERY SIMPLE bado watu walipukutika kwa starehe ya dakika tano tuh.
SASA HII
1. Epuka misongamano
2. Vaa mask
3. Usiwasalimie jirani
4. Unawe
5. Unywe maji
6. Usukutue na maji chumvi
7. Ukae nyumbani tu
8. Bar, sokoni, mpirani, kilabuni etc marufuku
9. Usisafiri
N.k
Niambie mtanzania na kunawa mikono wapi na wapi.
Kuvaa kondom tu tena zilitolewa bure na ikiuzwa ni mia watu wamekufa. Itakua sabuni, sanitaiza, maski nk?

Mkuu hoja yako inaeleweka. Lakini tunauvunja vipi mnyororo wa maambukizi? Hapo ndipo ulipo mzizi wa fitina.

Angalia masokoni, kwenye madaladala, ibada nk.

Shughuli haziwezi kuendelea kama kawaida.
 
Masharti ya UKIMWI yalikua madogo sana.
1. Epuka ngono
2. Ama uwe na mpenzi mmoja mwaminifu na
3. Ukishindwa kabisa tumia kondom.
VERY SIMPLE bado watu walipukutika kwa starehe ya dakika tano tuh.
MASHARTI YA KIPINDUPINDU NDIO MADOGO ZAIDI
1. Epuka uchafu
2. Uwe msafi
3. Kula visafi
SASA HII
1. Epuka misongamano
2. Vaa mask
3. Usiwasalimie jirani
4. Unawe
5. Unywe maji
6. Usukutue na maji chumvi
7. Ukae nyumbani tu
8. Bar, sokoni, mpirani, kilabuni etc marufuku
9. Usisafiri
N.k
Niambie mtanzania na kunawa mikono wapi na wapi.
Kuvaa kondom tu tena zilitolewa bure na ikiuzwa ni mia watu wamekufa. Itakua sabuni, sanitaiza, maski nk?
Umefikiria mbali sana...kweli wewe ni great thinker
 
Taarifa za maambukizi zimekuwa tata kiasi zimewachanganya watu. Kwamba Isabella hakuambukiza jambo la kheri mno:

"Too good to be true".

IMG_20200404_150834_400.jpg


Kwingine updates ni 24 hours na ni factual.
 
Kwa MTU anayeijua Tanzania vizuri na maisha ya Watanzania yalivyo hawezi kushauri total lockdown, labda kama hana akili timamu.
Ni rahisi Rais Magufuli kuhamia chadema kuliko kutangaza total lockdown.
CHADEMA ni sumaku mkuu usiongee sana. Tulishawakaribisha mawaziri wakuu wawili. Membe yuko mlangoni anabisha hodi. CHADEMA habari nyingine kaka. Halafu hatununui watu wala madeni yao, wao ndio wanakuja na pesa zao nyingi.
 
Sisi tunamsikiliza ummy mwalimu.
SIO WATABIRI WA CORONA.
Kwa vile hujaambiwa haina maana kuwa hawajaongezeka.

Nota bene hukuliona pale?

"Akili za kuambiwa changanya na za kwako".

Hivi hata umeisoma ile article ya WEF? Je hata umeiona? Na je umeielewa?

Au umekurupuka kudandia treni kwa mbele.

Mawazo yako Isabella tokea KIA, Arusha, Mount Meru hospitali na kote alikopita unaambiwa hakuambukiza mtu, na wewe unakubali? Labda kama alikuwa na malaria tu.

Angalia mkuu utauzwa mchana mchana.
Screenshot_20200404-174031.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilichonitokea hapa kwajili ya kucheka hiyo namba 3 hadi 6 duh... haya bhana
Masharti ya UKIMWI yalikua madogo sana.
1. Epuka ngono
2. Ama uwe na mpenzi mmoja mwaminifu na
3. Ukishindwa kabisa tumia kondom.
VERY SIMPLE bado watu walipukutika kwa starehe ya dakika tano tuh.
MASHARTI YA KIPINDUPINDU NDIO MADOGO ZAIDI
1. Epuka uchafu
2. Uwe msafi
3. Kula visafi
SASA HII
1. Epuka misongamano
2. Vaa mask
3. Usiwasalimie jirani
4. Unawe
5. Unywe maji
6. Usukutue na maji chumvi
7. Ukae nyumbani tu
8. Bar, sokoni, mpirani, kilabuni etc marufuku
9. Usisafiri
N.k
Niambie mtanzania na kunawa mikono wapi na wapi.
Kuvaa kondom tu tena zilitolewa bure na ikiuzwa ni mia watu wamekufa. Itakua sabuni, sanitaiza, maski nk?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Covid-19 ugonjwa usababishwao na Corona virus hadi sasa hauna tiba wala chanjo. Waliopona ugonjwa huu wamepona si kwa kuwa walikuwa wakitibiwa Covid-19 bali zaidi kwa bahati zao na kudra za mwenyezi Mungu.

Ugonjwa huu unaua. Hata aliyeugua akapona, anaweza kuugua tena na tena, akapona tena au hata akafa. Bahati na kudra za mwenyezi Mungu huwa hazipo kila siku. Wanasema waswahili, "bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi."

Ni kwa sababu ya kutokuwa na tiba kamili ya ugonjwa huu, kwa maelfu ya watu waliokwisha ambukizwa: USA, Italy, Spain , nk, vifo vimekuwa vikiongezeka na vikipindukia hata zaidi ya 900 kwa siku kwa nchi kwa nchi na kwa siku kadhaa mfululizo sasa.

Tatizo kubwa zaidi na ugonjwa huu liko katika kasi yake ya maambukizi ambapo maelfu ya watu wanaweza kuambukizwa katika muda mfupi tu:

1. Mtu aliyeathirika ataambukiza wote anaohusishwa nao hata kwa ukaribu tu.

2. Kila aliyeambukizwa na aliyeathirika, naye ataambukiza wote atakaohusishwa nao hata kwa ukaribu wao tu.

3. Kila aliyeambukizwa, naye ataambukiza wote atakaohusishwa nao pia,hata kwa ukaribu wao tu.

4. Hii ambukizwa ambukiza huendelea hivyo kwa kasi ya mithili ya mlipuko wa bomu.

Kwa vile pia pana suala la hewa linalohusishwa kwenye kuenea au kuambukiza kwake, huu ugonjwa unamuweka kila mtu hatarini.

Ugonjwa huu unaambukizwa na kusambaa kisayansi ambapo njia pekee ya kisayansi ya kuudhibiti, imefahamika kuwa ni katika kupambana kuuvunja mlolongo na mnyororo wake wa maambukizi.

Rejea mada hii kutoka World Economic Forum (WEF) inayoangazia ufumbuzi pekee na kamili ya kuzuia maambukizi ya covid-19:

Why lockdowns can halt the spread of COVID-19

Muhimu kutumia muda kusoma na kuelewa.

Ubinafsi, itikadi, imani, kukurupuka, nk ni muhimu kukuweka pembeni, japo kwa muda.

Total lockdown pamoja na machungu yake ndiyo inayoweza kutuokoa na sisi pia ili kutokuangamia na gonjwa hili lisilo na tiba.

Mbaya zaidi ni kuwa muda wa total lockdown utakuwa mrefu zaidi kama tutachelewa mno kuanza kuitumia.

Kwa hisani (Mwana JF) "remote" katika picha ni uwezekano wa maambukizi ya yule mgonjwa wa kwanza (Tanzania Corona patient zero):

View attachment 1408672


NB: "Akili za kuambiwa changanya na za kwako". Mwisho wa kumnukuu.
Me nmekuelewa mkuu. Watakaopinga kwamba lock down haifai watuambie ni njia zipi zingine zinaweza kupunguza kasi ya kuenea kwa ugonjwa huu?

Na watuambie hizo njia zimetumika nchi gani na matokeo yakawaje?
 
Pana miito kadhaa kuondoa jitihada za kupambana na Corona kutoka mikononi kwa nchi. Ukiona hivyo ujue kuna ukakasi kameshaonekana.

Hapa katika kutambua jitihada zao wenzetu wanasonga:

IMF yaunga mkono juhudi zao katika lockdown. Nani watakufa njaa iwapo hata kwa uji tu mtu ata survive hata zaidi ya mwezi?:

IMF approves $109m to cushion Rwanda against covid-19 impact

Tushirikiane kuitaka serikali kutambua tukijizatiti kW raslimali zetu hata na wengine watatuunga mkono.

Corona haitaondoka yenyewe bila jitihada chungu kabisa za makusudi.
 
Me nmekuelewa mkuu. Watakaopinga kwamba lock down haifai watuambie ni njia zipi zingine zinaweza kupunguza kasi ya kuenea kwa ugonjwa huu?

Na watuambie hizo njia zimetumika nchi gani na matokeo yakawaje?

Mkuu inasikitisha wanafanya siasa kwenye masuala serious haya.

Hawana mbadala. Wala hawaoni pana mnyororo wa kuvunjwa imebakia tu mtanzania hawezi labda kama wanasema pia mtanzania afe tu.
 
Sisi tumemuachia Mungu.😃

Tukisema tuweke lockdown nchi nzima tutakufa kwa njaa kuliko hata COVID-19 yenyewe.
 
Back
Top Bottom