Mkuu brazaj , nimefuatilia mabandiko yako, naona una hoja za msingi sana.
Kwa vile serikali yetu imeamua kupuyanga hivyo hivyo, hapa ni kila mtu kuamua hatma yake na familia inayomzunguka.
Jifungie wewe mwenyewe na familia yako ili kutii masharti ya WHO. Hakuna haja ya kusubiri mpaka serikali itangaze zuio la jumla.
Jambo lingine la kuzingatia hapa ni kwamba, serikali inahamasisha watu kutii ushauri wa wataalam wa afya. Hivyo basi, pamoja na serikali kutokutangaza total lockdown... changanya na zako!
Ingawa una mwandiko mzuri, ni vyema ukapata ushuhuda huu utakusaidiaCovid-19 ugonjwa usababishwao na Corona virus hadi sasa hauna tiba wala chanjo. Waliopona ugonjwa huu wamepona si kwa kuwa walikuwa wakitibiwa Covid-19 bali zaidi kwa bahati zao na kudra za mwenyezi Mungu.
Ugonjwa huu unaua. Hata aliyeugua akapona, anaweza kuugua tena na tena, akapona tena au hata akafa. Bahati na kudra za mwenyezi Mungu huwa hazipo kila siku. Wanasema waswahili, "bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi."
Ni kwa sababu ya kutokuwa na tiba kamili ya ugonjwa huu, kwa maelfu ya watu waliokwisha ambukizwa: USA, Italy, Spain , nk, vifo vimekuwa vikiongezeka na vikipindukia hata zaidi ya 900 kwa siku kwa nchi kwa nchi na kwa siku kadhaa mfululizo sasa.
Tatizo kubwa zaidi na ugonjwa huu liko katika kasi yake ya maambukizi ambapo maelfu ya watu wanaweza kuambukizwa katika muda mfupi tu:
1. Mtu aliyeathirika ataambukiza wote anaohusishwa nao hata kwa ukaribu tu.
2. Kila aliyeambukizwa na aliyeathirika, naye ataambukiza wote atakaohusishwa nao hata kwa ukaribu wao tu.
3. Kila aliyeambukizwa, naye ataambukiza wote atakaohusishwa nao pia,hata kwa ukaribu wao tu.
4. Hii ambukizwa ambukiza huendelea hivyo kwa kasi ya mithili ya mlipuko wa bomu.
Kwa vile pia pana suala la hewa linalohusishwa kwenye kuenea au kuambukiza kwake, huu ugonjwa unamuweka kila mtu hatarini.
Ugonjwa huu unaambukizwa na kusambaa kisayansi ambapo njia pekee ya kisayansi ya kuudhibiti, imefahamika kuwa ni katika kupambana kuuvunja mlolongo na mnyororo wake wa maambukizi.
Rejea mada hii kutoka World Economic Forum (WEF) inayoangazia ufumbuzi pekee na kamili ya kuzuia maambukizi ya covid-19:
Why lockdowns can halt the spread of COVID-19
Muhimu kutumia muda kusoma na kuelewa.
Ubinafsi, itikadi, imani, kukurupuka, nk ni muhimu kukuweka pembeni, japo kwa muda.
Total lockdown pamoja na machungu yake ndiyo inayoweza kutuokoa na sisi pia ili kutokuangamia na gonjwa hili lisilo na tiba.
Mbaya zaidi ni kuwa muda wa total lockdown utakuwa mrefu zaidi kama tutachelewa mno kuanza kuitumia.
Kwa hisani (Mwana JF) "remote" katika picha ni uwezekano wa maambukizi ya yule mgonjwa wa kwanza (Tanzania Corona patient zero):
View attachment 1408672
NB: "Akili za kuambiwa changanya na za kwako". Mwisho wa kumnukuu.
Mkuu kama wewe huna za kwako utachanganya vipi na za wengine?
Kwa vile wewe huna za kwako basi tumia za wengine.
Uko sawa kabisa mkuu tumia za wengine. Hata wakikwambia sasa hivi ni asubuhi wewe ni kuwakubalia tu mkuu, huna namna.
Me nmekuelewa mkuu. Watakaopinga kwamba lock down haifai watuambie ni njia zipi zingine zinaweza kupunguza kasi ya kuenea kwa ugonjwa huu?
Na watuambie hizo njia zimetumika nchi gani na matokeo yakawaje?
Njia.nzuri ya kuvunja mnyonyoro wa hii virus ni kuwashawishi watu wakapime kwa hiyari..Mkuu hizo nchi unazozitaja hazina misongamano kama unayoiona masokoni, kwenye madaladala, ibadani nk kama makwetu.
Hawa pia wamechukua hatua mapema sana kabla ya gonjwa kulipuka vilivyo.
Hata hivyo Japan hawa hapa:
Japan's coronavirus containment strategy faces breaking point
Sweden nao wana visa si chini ya 4000 na vifo mia kidogo ndiyo kudunda huko?:
Sweden response to coronavirus outbreak divides opinion
Mkuu ingependeza zaido mkaonyesha namna ya kuuvunja mnyororo wa maambukizi ya ugonjwa huu kabla hali haijawa mbaya zaidi.
Unachokiombea HAKITAFANIKIWA..
Tanzania tunaendelea vizuri na mapambano.
najua unatamani wagonjwa waongezeke ili uone kane ulitabiri.
na kwambia hivi hapa Tanzania hata wagonjwa 50 hawatafika..
Sent using Jamii Forums mobile app
Lockdown inazidisha wagonjwa kwa muono wangu..Rwanda ana 102.
Kenya ana 126
Sauzi ana 1585..
Uganda ana 48.
Hawa wote walitumia lock down au wanaendelea kutumia.
LAKINI JIULIZENI WANA PUNGUZA WAGONJWA AU WANAONGEZA?
Sent using Jamii Forums mobile app
Good idea! Mtu akusaidieje ikiwa ulishapuuza aliyokushauri? Rwanda wapo smarter!Pana miito kadhaa kuondoa jitihada za kupambana na Corona kutoka mikononi kwa nchi. Ukiona hivyo ujue kuna ukakasi kameshaonekana.
Hapa katika kutambua jitihada zao wenzetu wanasonga:
IMF yaunga mkono juhudi zao katika lockdown. Nani watakufa njaa iwapo hata kwa uji tu mtu ata survive hata zaidi ya mwezi?:
IMF approves $109m to cushion Rwanda against covid-19 impact
Tushirikiane kuitaka serikali kutambua tukijizatiti kW raslimali zetu hata na wengine watatuunga mkono.
Corona haitaondoka yenyewe bila jitihada chungu kabisa za makusudi.
Njia.nzuri ya kuvunja mnyonyoro wa hii virus ni kuwashawishi watu wakapime kwa hiyari..
Kumpima mgonjwa wakati tayari ana symptoms ni kupoteza resources kwani inasemekana mgonjwa anaweza kuambukiza wengine kabla hajaonyesha dalili za kuwa na huu ugonjwa..
Lockdown inazidisha wagonjwa kwa muono wangu..
Theory ya kuwa MIONZI ya jua inapunguza Kasi ya uambukizaji inawezekana kuwa ni kweli
Mpaka.sasa.Tanzania ndio yenye wagonjwa kidogo ukifanananisha na nchi nyengine za East AfricaHiyo mionzi ya jua iko Tanzania tu? Siyo serikali ya Tanzania imekubaliana kupunguza idadi ya maambukizi kwa maneno tu bila kujali hali halisi? Kama hii ndiyo mionzi yenyewe unayoisema nitakubaliana nawe.
Hivi yule waziri aliyesemekana kuathirika keshaonekana hadharani?
Akili za kuambiwa muhimu kuchanganya na zingine ndiyo maana sikusahau kuweka ile NB.
total lockdown kwa ajili ya haka ka ugongwa ka mafua, maleria kwa mwaka inaua watanzania zaidi ya laki , leo kafa mtu mmoja tujifungie ndani, huo ni uwendawazimu
Mpaka.sasa.Tanzania ndio yenye wagonjwa kidogo ukifanananisha na nchi nyengine za East Africa
kwa mantiki hiyo Model ya Tanzania ya kuzuia mamhukizi unafanya kazi
Tanzania wameungana na Japan na Sweden kwa kutumia njia ya Sina moja kuzuia hizi virusi visisambae kwa haraka..
Hoja yako mfu!!!!!!..China ugonjwa ulikoanzia walianza na wagonjwa watatu (3), leo ugonjwa umekua Pandemic!..nyie mlio na wagonjwa 20..mnajidai kutembelea vifua mbele!...mnatia huruma
Model ya Tanzania ni kuwafanya watu waendelea na maisha,..wasifungiwe ndani,kusiwe na Total lockdown,kUnaonaje uwashauri kabisa wote wasumbukao na mizigo ya corona hasa USA, Italy, Spain, nk pia hata Uganda, Kenya, Rwanda, South Africa nk waachane na matatizo wafuatane na model ya Tanzania?
Ninaamini una maana model ya Tanzania ni kuweka msemaji kama Ummy. Si kuwa na taarifa huru.
Model ya Tanzania ni kuwafanya watu waendelea na maisha,..wasifungiwe ndani,kusiwe na Total lockdown,k
Imekuwa proved kuwa nchi zote zilizoweka Quarantine wagonjwa wanaongezeka badala ya kupungu
Sweden na Japan ni mfano mzuri wa kuigwa