Namna ya kupata hisa katika soko la hisa la Dar es salaam

wasiliana na registered brokers,solomon stock brockers,tsl,core securities etc.watakufungulia CSD account ambapo utawapa details zako za bank,then watakupa purchasing order form ambapo utajaza unataka chukua hisa ngapi na zipi watakupatia price utadeposit ktk akaunti yao,then wataweka order wakikununulia utapewa share certificate.
 
Na ukitaka kuziuza upate faida unaanzia wapi mkuu?mi mgeni pande hizi.
 
Na ukitaka kuziuza upate faida unaanzia wapi mkuu?mi mgeni pande hizi.

Unaenda kwa huyo broker uliyenunua hisa mwanzoni ukiwa na certificate yako ya kukuonyesha unamiliki hisa za hiyo kampuni, kitambulisho chako na namba ya akaunti ya benki..baada ya hapo ataziingiza sokoni na zikishauzwa hisa zako pesa zako zitaingizwa kwenye akaunti yako ya benki......ni zoezi rahisi sana...hisa zinalipa pale utakaponunua za kampuni sahihi.
 

Na kwa sasa hivi ni kampuni gani inafanya vizuri sokoni?
 
Na kwa sasa hivi ni kampuni gani inafanya vizuri sokoni?

Waweza angalia huu mchanganuo wa jinsi thamani ya hisa ya kampuni ilivyopanda tangu mwezi machi 2014 mpaka leo hii oktoba 18,2014.
Swissport 2700 leo hii inauzwa 5060 so imepanda kwa 85%
CRDB 320 leo hii inauzwa kwa 450 imepanda kwa 40%
NMB 2680 leo hii inauzwa kwa 4690 imepanda kwa 75%
TOL 310 leo hii inauzwa shilingi 500
TPCC(TWIGA CEMENT) 2500 leo hii 6010 imepanda kwa 140%
DCB ilikuwa 490 leo hii inauzwa 550 imepanda kwa 12%
Hizo ni baadhi tu .
Kwa mfano kama ulinunua hisa za swissport zenye thamani ya laki tano mwezi machi mwaka huu leo hii oktoba 2014 zina thamani ya 925000(laki tisa na elfu ishirini na tano) ikimaanisha umepata faida ya laki nne na elfu ishirini na tano...
Kazi ni kwako mkuu waweza nunua swissport,simba au twiga cement,crdb au nmb.
 
Kwa hiyo Mkuu unataka kuniambiaje Mimi ambaye nina hisa 400 za swissport, 250 za NMB, 250 za Tanga cement na 1000 za NICOL (ila hapa niliuvaa mkenge). Naweza kuziuza kwa bei hiyo uliyoonesha hapo juu? Jamaa Wa kodi nao vipi - maana hapo hakuna kukwepa!!
 

Mkuu vipi na hao ma broker wa hisa wanafaidikaje hapo,Endapo mimi nimeamua kuuza hisa zangu?
 
jamani mwenye huelewa makampuni ya gas na jinsi zilivyo na namna ya kupata hisa

kampuni ya gesi iliyo na moto kwa sasa sokoni ni swala ila usitegemee gawio siku za karibuni kwa kuwa wanachofanya kwa sasa ni utafutaji wa gesi, na wametangaza hasara kwa kuwa bado hawajaanza uzalishaji. bei yake sokoni inapelekeshwa na 'speculations', wa-tz wananunua kwa kuwa wana hamu ya kuwekeza kwenye gesi. utaratibu wa kupata hisa ni kama ilivyoelezwa hapo mwanzo. kampuni nyingine ni TOL, hawa wapo sokoni kitambo na performance yao ni nzuri.
 

Asante kka kwa kuchukua muda wako kunijibu
 

Yap waweza kuziuza kwa bei hiyo au ya chini kuliko hiyo uamuzi ni wako.....mabroker huwa wanapata commision yao nayo huwa ni kati ya 2% hadi 5% ya thamani ya hisa ulizonunua au kuziuza( kama sikosei)......kuhusu kodi mara nyingi gawiwo(faida uliyoipata baada ya kuwekeza kwenye ununuzi wa hisa) ndo huwa linatozwa kodi.....epuka kununua hisa za kenya airways na precision air hapo utakuwa umeingia chaka la simba au hisa za kampuni ambazo na zenyewe huwa zinanunua hisa kwenye kampuni nyingine kama NICOL na takataka nyinginezo.
 
jamani mwenye huelewa makampuni ya gas na jinsi zilivyo na namna ya kupata hisa

Ipo TOL ambayo baada ya ku-restructure kampuni sasa hivi inafanya vizuri kwenye biashara kwani sasa hivi hawauzi tu oxygen bali na gesi nyinginezo ....swala wao ni watafutaji gesi asilia na mafuta bado hawajapata mafuta/gesi asilia ila watanzania wamenunua hisa zao Wakitegemea siku wakipata basi thamani ya hisa zao itapanda sana..thamani ya hisa za swala mpaka jana yaani oktoba 18,2014 ilishuka mpaka 1910 toka 2100 ilipokuwa awali wakati hisa zinauzwa kwa mara ya kwanza kampuni hiyo ilipoorodheshwa kwenye soko la hisa.
 
Ukihitaji hisa wasiliana na hawa hapa. Au tembelea http://dse.co.tz/ angalau mara mbili kwa siku kujua 'price fluctuation'.
Core Securities Ltd
P.O. Box 76800,
DAR ES SALAAM.
Offices:
Fourth Floor – Elite City Building,
Samora Avenue,
Tel: +255 22 2123103,
Fax: +255 22 2122562
E-mail: info@coresecurities.co.tz;
Website: www.coresecurities.co.tz
Orbit Securities Company Limited
P.O. Box 70254,
DAR ES SALAAM
Offices:
4th Floor, Golden Jubilee
Towers, Ohio Street,
Tel: 255 22 2111758, Fax: 255 22 2113067
E-mail: orbit@orbit.co.tz
SOLOMON Stockbrokers Limited
P.O. Box 77049,
DAR ES SALAAM
Offices:
Ground Floor - PPF House,
Samora Avenue/Morogoro Road.
Tel: 255 22 2124495/2112874,
Fax: 255 22 2131969
Mob: +255 714 269090 +255 764 269090
E-mail: solomon@simbanet.net
info@solomon.co.tz
Website: www.solomon.co.tz
Rasilimali Limited
P.O. Box 9373,
DAR ES SALAAM
Offices:
3rd Floor, CHC Building,
Samora Avenue,
Tel: 255 22 2111711
Fax: 255 22 2122883
Mob: +255 713 777818 / 784 777818 /
+255 754 283185
E-mail: rasilimali@africaonline.co.tz
Tanzania Securities Limited
P.O. Box 9821,
DAR ES SALAAM
Offices:
7th Floor, IPS Building
Samora Avenue/Azikiwe Street
Tel: 255 (22) 2112807,
Fax: 255 (22) 2112809
Mob: +255 718 799997 / +255 713 244758
E-mail: info@tanzaniasecurities.co.tz
Website: www.tanzaniasecurities.co.tz
Vertex International Securities Ltd
P.O. Box 13412,
DAR ES SALAAM.
Offices:
Annex Building - Zambia
High Commission,
Sokoine Drive/Ohio Street,
Tel: 255 22 2116382 Fax: 255 22 2110387
E-mail: vertex@vertex.co.tz.
operations@vertex.co.tz
Website: www.vertex.co.tz

[TD="colspan: 2"] Zan Securities Limited
P.O. Box 5366, Dar es salaam
P.O. Box 2138, Zanzibar
Offices:
Mezzanine Floor, Haidary Plaza, Dar es salaam
1st Floor, Muzammil Centre, Malawi Road, Zanzibar
Tel: +255 22 2126415, Fax: 255 22 2126414
Mob: +255 786 344767, +255 755 898425
E-mail: info@zansec.com [/TD]
 
Katika hao madalali wa Hisa, kampuni gani? Inafanya vizuri katika soko ukilinganisha na awa wengineo
 

JE, NINAWEZA KUNUNUA HISA ZA KAMPUNI TOFAUTI KWA KUTUMIA CDS MOJA NILIYOIPATA KWENYE KAMPUNI TOFAUTI???

Nisaidieni wataalamu wa fedha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…