Tafuta ndizi zako mzuzu mbivu,zisiwe zimeiva sana mpaka kulegea,au mbichi kama utapenda japo za kuiva huleta utam kwasababu ya ile sukari yake inatyotokana na kuiva kwa ndizi....
Zimenye vizuri,kama una mashine tumia kukatakata vipande vyembamba (virefu au vifupi fupi,au shape yoyote utakayo)unaweza tumia kisu japo mashine ni nzuri zaidi hasa kushape crips zako..
Ukimaliza zioshe vizuri ziache zichuje maji kabisa,ziwe kavu,.bandika mafuta yako ya kupikia kwenye karai au sufuria pana,yaache yapate moto sana,halafu weka vipande vyako vya crisps kwenye mafuta hayo,vikianza kubadilika rangi vigeuze geuze mpaka viwe brown na vikavu kabisaa
Vitoe kwenye mafuta na viweke kwenye chujio au tumia taulo yako ya jikoni kuchuja mafuta,.crisps zako zitakuwa tayari kwa kuliwa,kama ni kwa biashara unaweza kuzipaki kwenye vifungashio vyako zikiwa zimepoa..
NB:mafuta lazima yapate moto wa kutosha ili kuzifanya zisinyonye mafuta mengi,hazitapendeza zikiwa na mafuta mengi.