Namna ya kutengeneza Keki ya lozi

Namna ya kutengeneza Keki ya lozi

Gorgeousmimi

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
9,296
Reaction score
7,683
Mahitaji:
  • Mayai 8
  • 250g sukari
  • 300g lozi zilizosagwa tumia blender kusaga na machine ya kusagia viungo
  • Kijiko kimoja cha chai cha mdalasini ulosagwa
  • Vanila kijiko kimoja cha chai
  • Maganda ya limau na chungwa yalosagwa
  • Icing sugar

Jinsi ya kutayarisha:

  1. Tenganisha viini vyai kutoka kwenye weupe wa yai.
  2. Piga weupe wa yai mpaka ukazane.
  3. Tumia bakuli jingine kupiga viini vya yai,sukari na vanilla
  4. Changanya mdalasini,maganda ya limau na chungwa pamoja na lozi
  5. Mwisho changanya mchanganyiko wako na weupe wa yai uloupiga fanya kama unafold in taratibu usikoroge kwa nguvu.
  6. Tumia bati la keki la mduara size ya kati lipake siagi kabla hujaweka mchanganyiko wako
  7. Choma keki yako kwenye 175 degrees kwa muda wa dakika 45
  8. Keki ikishapoa nyunyuizia Icing sugar juu.
keki ya lozi.jpg keki ya lozi 2.jpg

Jinsi ya kutenganisha kiini cha yai kutoka kwenye ute wa yai:

  • Unahitaji mabakuli mawili moja la kuwekea viini na jingine ute wa yaivunja yai
  • Vunja yai,weka bakuli chini ya yai ukiliwa unalitenganisha weka kiini cha yai kwenye ganda moja wapo na fanya kama unalichuja ili ute umwagikie kwenye bakuli na unaweza kulipokeza kwenye ganda la pili mpaka ute wote umwagikie bakulini
  • Weka kiini cha yai kwenye bakuli jingine.
  • Njia nyingine ni kutumia mikono.Unavunja yai kisha unatenganisha kiini na ute kwa kutumia mikono yako.
egg whites from egg yolk.jpg
 
Hivi nawezaje tenganisha viini na ute wa kawaida wa yai

Nimeweka juu hapo kwenye post ya keki na picha ipo pia.Unavunja yai na kuliweka kwenye mkono.Bakuli likiwa kwachini ili yte upite kati kati ya vidole na fanya kama unapokeza kutoka kwenye kiganja cha mkono mmoja kwenda kwenye kingine mpaka kiini kiwe hakina ute.Au kama hutaki kuchafuka mikono unatumia maganda ya mayai.Tactic nyingine unaweza kuona kwenye video nimeweka attachment.
 
Last edited by a moderator:
Asante sana mpendwa gorgeousmimi kwa recipe yako nzuri, bila shaka keki hii itakuwa tamu sana. I cant wait to taste it. Ila naomba unitoe ushamba mpendwa, lozi ndio nini na inapatikana wapi?
 
Asante sana mpendwa gorgeousmimi kwa recipe yako nzuri, bila shaka keki hii itakuwa tamu sana, I cant wait to taste it. Ila naomba unitoe ushamba mpendwa, lozi ndio nini na inapatikana wapi?
Karibu sana Young Master.Lozi ni jamii ya nuts my dia na zinapatikana katika duka lolote la nafaka.
Kwa kiingereza zinaitwa ALMONDS!
loz 2.jpeg
 
Last edited by a moderator:
gorgeousmimi kwahio hatuweki unga hata kidogo zaidi ya huo wa lozi ...na bp je?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom