Habarini Wadau,
Sio siri huwa ninampenda sana Hoyce Temu aliyekuwa Miss Tanzania nafikiri wa mwaka 1999.
Huyu dada amekuwa akionesha roho safi na upendo wa dhati kabisa kwa wasiojiweza na hasa watoto.
Katika kipindi chake cha "Mimi na Tanzania" Huwa anawashika, anawakumbatia na kuwajali watoto wenye matatizo makubwa kiafya kama vile ni wakwake wa kuwazaa.
Pia huwa anasisitiza wachangiwe na kupatiwa misaada mbalimbali.
Sikuwahi kujua kuwa kuna wadada wa kichaga wana roho nzuri hivi kwajinsi wanavyosemwa humu.
Mungu akutunze Dada Hoyce Temu na azidi kukupa moyo wa huruma.
AAMIN.